Sunteți pe pagina 1din 145

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TUME YA MABADILIKO YA KATIBA

TAARIFA YA UTAFITI KUHUSU MADARAKA YA


RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Taarifa Nambari 1

DISEMBA, 2013
YALIYOMO

SEHEMU YA KWANZA .................................................................. 1

1.1 MADARAKA YA RAIS NA SABABU ZAKE ................................. 1

1.2 HISTORIA FUPI YA MADARAKA YA RAIS ................................ 9

1.3 HITIMISHO........................................................................... 13

SEHEMU YA PILI ........................................................................ 15

2.1 MAMLAKA YA KUTOA MISAMAHA ........................................ 15

2.2 UZOEFU WA NCHI NYINGINE .............................................. 22

2.3 TATHMINI NA MAPENDEKEZO ............................................. 25

2.4 MAPENDEKEZO ................................................................... 31

SEHEMU YA TATU ..................................................................... 33

3.1 MAMLAKA YA KUTANGAZA HALI YA HATARI ....................... 33

3.2 MWISHO .............................................................................. 39

SEHEMU YA NNE ....................................................................... 41

4.1 NAFASI YA RAIS WAKATI WA UCHAGUZI ............................. 41

4.2 MAPENDEKEZO ................................................................... 44

SEHEMU YA TANO ..................................................................... 46

5.1 UDHIBITI WA MADARAKA YA RAIS NA UWAJIBIKAJI........... 46

5.2 MAPENDEKEZO ................................................................... 61

SEHEMU YA SITA....................................................................... 64

6.1 KINGA YA RAIS KUSHTAKIWA.............................................. 64

6.2 MAPENDEKEZO ................................................................... 80

SEHEMU YA SABA...................................................................... 83

7.1 MAMLAKA YA UTEUZI .......................................................... 83


i
7.2 UZOEFU WA NCHI NYINGINE .............................................. 86

7.3 MAPENDEKEZO ................................................................... 87

SEHEMU YA NANE ................................................................... 114

8.1 MUHTASARI WA MAPENDEKEZO ...................................... 114

BIBLIOGRAFIA ......................................................................... 122

ii
VIFUPISHO

Ag J Acting Judge
AICC Arusha International Conference Centre
All ER All England Reports
CCM Chama cha Mapinduzi
CDA Capital Development Authority
DAWASA Dar es Salaam Water and Sewerage Authority
EA East Africa Law Reports
EACA Eastern Africa Court of Appeal Reports
EWURA Energy and Water Utilities Regulatory Authority
IFM Institute of Finance Management
JKT Jeshi la Kujenga Taifa
JWTZ Jeshi la Wananchi wa Tanzania
LRT Law Reports of Tanzania
Mf. Mfululizo
MSD Medical Store Department
NACTE National Council for Technical Education
NECTA National Examinations Council of Tanzania
NEMC National Environmental Management Council
NSSF National Social Security Fund
PPRA Public Procurement Regulatory Authority
PSPF Public Service Pensions Fund
QB Queen’s Bench Reports
RE Revised Edition
SSRA Social Security Regulatory Authority
STAMICO State Mining Corporation
SUMATRA Surface and Marine Transport Authority
TACAIDS Tanzania Commission for Aids
TAKUKURU Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa
TCAA Tanzania Civil Aviation Authority
TCRA Tanzania Communications Regulatory Authority
TEMCO Tanzania Election Monitoring Committee
TIC Tanzania Investment Centre
TLR Tanzania Law Reports
TPDC Tanzania Petroleum Development Corporation
TRA Tanzania Revenue Authority
Uk. Ukurasa

iii
VETA Vocational Education and Training Authority
W.L.R. Weekly Law Reports

iv
Katiba na Sheria Zilizorejewa

Katiba

Katiba ya Finland, 1999.

Katiba ya India ya Mwaka, 2007.

Katiba ya Jamhuri ya Afrika Kusini, 1996.

Katiba ya Jamhuri ya Kenya, 2010.

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977.

Katiba ya Jamhuri ya Tanganyika, 1962.

Katiba ya Jamhuri ya Zambia, 1991.

Katiba ya Marekani, 1787.

Katiba ya Muda ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1965.

Katiba ya Namibia, 1990.

Katiba ya Ufaransa, 1958.

Katiba ya Uganda, 1995.

Katiba ya Uhuru ya Tanganyika, 1961.

Katiba ya Zanzibar, 1979.

Katiba ya Zanzibar, 1984.

Katika ya Jamhuri ya Ufilipino, 1987.

Katika ya Jamhuri ya Kiislam ya Iran, 1979.

Katika ya Jamhuri ya Zanzibar, 1963.

v
Mikataba ya Kimataifa

The European Convention on Human Rights and Fundamental


Freedoms (ECHR).

The International Covenant on Civil and Political Rights (ICCPR).

The American Convention on Human Rights (ACHR).

Sheria

The Air-Tanzania Corporation (Re-organisation and Vesting of


Assets and Liabilities) Act, 2002.

The Anti-Money Laundering Act, Cap 423.

The Atomic Energy Act, Cap 188.

The Bank of Tanzania Act, Cap 197.

The British Defence of the Realm Act, 1914.


The British Defense of the Realm Act, 1914.

The Cashewnut Industry Act, 2009.

The Cereals and Other Produce Act, 2009.

The College of Wildlife Management Act, Cap 209 [RE 2002].

The Crops Laws Miscellaneous Amendments) Act, 2009.

The Dar es Salaam Institute of Technology Act, Cap 144 [RE 2002].

The Dar es Salaam Water and Sewerage Authority (Amendment)


Act, 2001.

The Education Fund Act, Cap 412 [RE 2002].

The Election Expenses Act, 2010.

The Emergency Powers Act, Cap 221 [RE 2002].

The Energy and Water Utilities Regulatory Authority Act, 2001.

The Environmental Management Act, Cap 191.

vi
The Fair Competition Act, Cap 285.

The Fertilizers Act, 2009.

The Gaming Act, Cap 41.

The Institute of Accountancy Arusha Act, Cap 240 [RE 2002].

The Institute of Finance Management Act, Cap 91 [RE 2002].

The Institute of Rural Development Planning Act, Cap 174 [RE


2002].

The Insurance Act, 2009.

The Judiciary Administration Act, 2011.

The Kariakoo Market Corporation Act, Cap 132 [R.E 2002].

The Labour Institutions Act, Cap 300.

The Land Act, Cap 113 [R.E 2002].

The Law Reform Commission Act, Cap.171 [R.E 2002.

The Local Authorities Pensions Fund Act, Cap 407.

The Medical Stores Department Act, Cap 70 [RE 2002].

The Meteorology Act, Cap 157 [RE 2002].

The Mining Act, 2010.

The Muhimbili National Hospital Act, Cap 150 [R.E 2002].

The Mwalimu Nyerere Memorial Academy Act, Cap 93.

The National Council for Technical Education Act Cap 129 [R.E
2002].

The National Examinations Council of Tanzania, Cap 107 [RE


2002].

The National Housing Corporation Act, Cap 295 [RE 2002].

The National Land Use Planning Commission Act, Cap 116 [R.E
2002.

The National Parks Act, Cap 282 [R.E 2002].

vii
The National Social Security Act, Cap 50 [RE 2002].

The National Social Welfare Training Institute Act, Cap 110 [R.E
2002].

The Newspapers Act, Cap. 229 [RE 2002].


The Ngorongoro Conservation Area Act, Cap 284 [RE 2002].

The Non-Governmental Organisations Act, Cap 56.

The Ocean Road Cancer Institute Act, Cap 86 [R.E 2002].

The Parole Boards Act, Cap 400 [RE 2002].

The Petroleum (Exploration and Production) Act, Cap 328 [R.E


2002].

The Planning Commission Act, Cap 314 [R.E 2002].

The Political Parties Act, Cap 258 [R.E 2002].

The Presidential Affairs Act, Cap 9 [R.E 2002].

The Prevention and Combating of Corruption Act, Cap 329 [R.E


2002].

The Public Code of Ethics Act, Cap 398 [R.E 2002].

The Public Finance Act, Cap 348 [R.E 2002].

The Public Procurement Act, 2011.

The Public Service Act, 2002.

The Public Service Pensions Fund Act, Cap 371 [R.E 2002].
The Social Security (Regulatory Authority Act, 2008.

The Special Tribunals Act Cap 126 [R.E 2002].

The Surface and Marine Transport Regulatory Authority Act, 2001.

The Tanzania Civil Aviation Authority Act, 2003.

The Tanzania Commission for Aids Act, 2001.

The Tanzania Commission for Science and Technology Act, Cap 226
[R.E 2002].

The Tanzania Communications Regulatory Authority Act, Cap 172.

viii
The Tanzania Institute of Education Act, Cap 142 [R.E 2002].

The Tanzania Investment Act, Cap 38 [R.E 2002].

The Tanzania Revenue Authority Act, Cap 339 [R.E 2002].

The Tanzania Trade Development Authority Act, 2009.

The Tanzania Wildlife Research Institute Act, Cap 260 [R.E 2002].

The Tax Revenue Appeals Act, Cap 408 [R.E 2002].

The Tropical Pesticides Research Institute Act, Cap 161 [R.E 2002].

The U.S War Powers Act, 1973.

The Universities Act, Cap 346.

The Vocational Education and Training Act, Cap 82 [R.E 2002].

The Wildlife Conservation Act. 2009.

The Workers’ Compensation Act, 2008.

Sheria Ndogo (Subsidiary Legislation)

The Arusha International Conference Centre (Establishment) Order,


[G.Ns. Nos.51 of 1983, 470 of 1987 and115 of 1995].

The Capital Development Authority (Establishment) Order, [G.N.


Nos.230 of 1973, 230 of 1984 and 32 of 2001].

The Kibaha Education Centre (Establishment) Order, [G.N. No. 2 of


1970].

The Mzinga Corporation (Establishment) Order, [G.N. No. 219 of


1974].

The National Development Corporation (Establishment) Order, [G.N.


No. 90 of 1969].

The National Institute for Productivity (Establishment) Order, [G.N.


No. 124 of 1974].

The State Mining Corporation (Establishment) Order, [G.N. No. 163 of


1972].

ix
The State Motor Corporation (Establishment) Order, [G.Ns. Nos.72 of
1974 and 82 of 1975].

The Tanzania Legal Corporation (Establishment) Order. G.Ns. Nos.32


of 1971, 162 of 1972, 96 of 1976 and 366 of 1985].

The Tanzania Petroleum Development Corporation (Establishment)


Order, [G.N. No. 90 of 1969].

The Tanzania Petroleum Development Corporation (Establishment)


Order, [G.Ns. Nos.140 of 1969 and 43 of 1985].

The Tanzania Wildlife Corporation (Establishment) Order, [G.Ns.


Nos.231 of 1974 and 389 of 1990].

The Uyole Agricultural Centre (Establishment) Order, [G.N. No. 70 of


1976].

Kesi Zilizorejewa

Attorney-General and two others v Aman Walid Kabourou [1996]


TLR 156.

Clinton v Jones (95-1853), 520 U.S. 681 (1997).

Council of Civil Service Unions v Minister for Civil Service [1984] 3 All
ER 935.

Ferri v Ackerman, 444 U.S. 193 (1979).

James Funke Gwagilo v Attorney General [1994] TLR 73.

Jamhuri dhidi ya Juma Kulambalimbali [1974] LRT n. 41.

Marbury v Madison, (1803).

Mwalimu Paul John Mhozya v Attorney General (No. 1) [1996] TLR


130.

Mwandu Kashindye v Dalaly Peter Kafumu and two others, High


Court of Tanzania (Tabora Registry) (sitting at Nzega) Miscellaneous
Civil Cause NO. 10 OF 2011(unreported).

Nixon v Fitzgerald, 457 U.S. 731 (1982).

Patman Garments Industries Ltd v Tanzania Manufacturers Ltd.


[1981] TLR 303.

x
Permanent Secretary (Establishments) and another v Hilal Hamed
Rashid and 4 others [2005] TLR 121.

R. v Secretary of State for the Home Department, ex parte Bentley,


[1994] Q.B. 349.

Reg. v Bow Street Magistrate, ex parte Pinochet [1998]3 W.L.R.1 456.

Reg. v Bow Street Magistrate, exparte Pinochet (No. 3) [1999] 2


W.L.R. 827.

Rex v Palamba s/o Fundikila, 14 EACA 96.

Said Juma Muslim Shekimweri v Attorney-General [1997] TLR 3.

Tumukunde dhidi ya Mwanasheria Mkuu na Mwingine [2005] 2 EA


291.

United States v Branscum, No., LRP-CR-96-49 (ED Ark., June 7,


1996).

United States v Fromme, 405 F. Supp. 578 (ED Cal. 1975).

United States v McDougal, 934 F. Supp. 296 (ED Ark. 1996).

United States v Nixon, 418 U.S. 683 (1974).

xi
xii
UTANGULIZI

Maelezo ya Ujumla
Hii ni taarifa ya utafiti uliofanywa kuhusiana na madaraka ya Rais
wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania. Katiba na sheria
mbalimbali zimempa Rais mamlaka ya aina mbalimbali yakiwemo
mamlaka ya kuigawanya nchi katika mikoa, kuwaweka watu
kizuizini, kuwafukuza watu kutoka eneo moja kwenda eneo lingine
(deportation), kulivunja Bunge, kutunga sheria ndogo, kuanzisha
au kuzifuta ofisi za umma, na madaraka mengine mengi. Hata
hivyo, utafiti ulilenga vipengele vya madaraka ya Rais ambavyo
vimejitokeza katika maoni ya wananchi. Vipengele hivyo ni
madaraka ya uteuzi, madaraka ya kutangaza hali ya hatari,
madaraka ya kutoa misamaha ya adhabu, uwajibikaji na udhibiti
wa madaraka ya Rais, na nafasi ya Rais wakati wa uchaguzi.

Katika utafiti wa masuala kadhaa yanayohusu madaraka ya Rais,


imeonekana kuwa sheria zenye asili ya Uingereza (common law)
hazina msaada mkubwa. Sheria hizo zimetoka kwenye utamaduni
ambao haujui kabisa taasisi ya Urais. Mahakama ya Juu ya
Marekani (The Supreme Court) katika shauri la Nixon v Fitzgerald,
457 U.S. 731 (1982) ilisema sheria zenye asili ya Uingereza
(common law) zilikua katika nchi ambayo hakuna kabisa taasisi ya
Urais haziwezi kuisaidia Mahakama inapoamua suala linalohusu
madaraka ya Urais. Ni kwa sababu hiyo Mahakama ya Mamwinyi
(House of Lords) wakati ikiamua shauri lililohusu kinga ya
kutoshtakiwa kwa Rais wa Chile (Jenerali Pinochet) ilisema kuwa
sheria kuhusu kinga ya Rais haieleweki vizuri. Kwa sababu hiyo
kwa kiasi kikubwa Majaji waliamua kutumia sheria za kimataifa
kuamua. Ukweli ni kwamba Dola ya Uingereza inajua utawala wa
kifalme na siyo utawala wa jamhuri. Ni kutokana na sababu hii
utafiti umejaribu kutafuta msaada zaidi katika sheria za Marekani
sehemu ambayo taasisi ya Urais imekua.

Historia Fupi
Kama ilivyoelezwa hapo juu, Rais wa Tanzania anayo mamlaka
mengi. Kwa kiwango kikubwa mamlaka hayo ni matokeo ya
historia ya nchi. Tanzania ilitawaliwa na Waingereza mara baada ya
Vita Kuu ya Pili ya Dunia mwaka 1918 mpaka ilipopata uhuru
mwaka 1961. Wakati wote huo, mwakilishi wa Mfalme wa
Uingereza, Gavana alikuwa na mamlaka yote ya Mkuu wa Nchi,
Mkuu wa Serikali na Amiri-Jeshi-Mkuu. Gavana alitawala kama
alivyopenda ili kufikia malengo ya ukoloni. Gavana alikuwa ni
mwajiri mkuu mwenye uwezo wa kuunda na kufuta ofisi kadiri
alivyoona inafaa, alikuwa na uwezo wa kuajiri na kufukuza
watendaji wa Serikali. Gavana aliteua Mawaziri Majaji na watendaji
wa Mahakama. Ardhi yote ilitangazwa kuwa ni mali ya umma chini
ya udhamini wa Gavana kwa niaba ya Mfalme wa Uingereza.
Madaraka mengine yalikuwa ni kusamehe wafungwa, kuhamisha
watu kutoka sehemu moja ya nchi kwenda sehemu nyingine.
Gavana alikuwa na uwezo wa kutoa amri ya watu kuhamishwa
kutoka ndani ya nchi kwenda nje ya nchi1.

Tanganyika ilipata uhuru mwaka 1961. Baada ya Uhuru,


madaraka ya Mkuu wa Nchi na Mkuu wa Serikali yalitenganishwa.
Gavana aliiendelea kuwa Mkuu wa Nchi na Amiri-Jeshi-Mkuu kwa
niaba ya Malkia wa Kiingereza. Kiongozi wa Serikali alikuwa ni
Waziri Mkuu, ambaye alikuwa ni kiongozi wa chama kilichopata
Wabunge wengi kwenye Uchaguzi Mkuu2. Gavana alikuwa na
madaraka ya kuteua Wabunge na wajumbe wa Tume ya uchaguzi.
Kwa idhini ya Gavana, Bunge lilizuiliwa kuandika muswada juu ya
utozaji wa kodi kwa namna yoyote ile isipokuwa kupunguza;
kuagiza malipo au matumizi ya fedha yafanywe kutokana na Mfuko
Mkuu wa Hazina ya Serikali au mfuko mwingine wowote
ikifahamika kwamba fedha iliyomo katika mifuko hiyo
haikupangiwa ipangiwe kufanyika kwa ajili ya matumizi hayo;
kufuta au kusamehe deni lolote linalotakiwa lilipwe na Serikali au
kutoa hoja ya kushughulikia mambo yaliyotajwa hapo juu3.

Gavana alikuwa pia na uwezo wa kuvunja Bunge;kuanzisha na


kufuta ofisi za umma; kuteua mawaziri na naibu mawaziri kutoka
miongoni mwa Wabunge; kuteua na kufukuza maofisa wa umma4;
kusamehe wafungwa au kuwabadilishia adhabu kwa kadiri

1 The Tanganyika Order in Council, 1920; Tanganyika (Legislative Council) Order


in Council, 1926
2 Kifungu cha 41 cha The Tanganyika (Constitution) Order in Council, 1961.
3 Kifungu cha 37 (a) na (b) cha The Tanganyika (Constitution) Order in Council,

1961.
4 Kifungu cha 54.

xiv
anavyoona inafaa1; kuteua Majaji akiwemo Jaji Mkuu na Tume ya
Utumishi wa Mahakama.2

Mwaka 1962, kulikuwa na mabadiliko ya Katiba yaliyoifanya


Tanganyika kuwa Jamhuri chini ya Rais. Madaraka ya Mkuu wa
Nchi na Mkuu wa Serikali yaliunganishwa na kuwekwa chini ya
Rais. Hivyo, Rais akawa Mkuu wa Nchi, Kiongozi wa Serikali na
Amiri-Jeshi-Mkuu. Madaraka ya Rais yaliongezwa katika
mabadiliko yaliyofuata ya Katiba na kuundwa ama kurekebishwa
kwa sheria mbalimbali. Madaraka hayo yaliimarika zaidi baada ya
kuundwa kwa Jamhuri ya Muungano baada ya iliyokuwa Jamhuri
ya Tanganyika kuungana na Jamhuri ya Zanzibar kuungana na
baada ya kuundwa kwa Katiba ya ya kudumu ya Jamhuri ya
Muungano ya Mwaka 1977.

Rais wa Kwanza wa Tanzania, Julius Nyerere akizungumzia


madaraka ya Rais alishawahi kunukuliwa akisema kuwa
“madaraka ya Rais ni makubwa kiasi cha kuweza kumfanya awe
dikteta kama angetaka”.3 Lakini madaraka hayo yalikuwa muhimu
kwa kuwa Tanzania ilihitaji Serikali yenye nguvu ili iweze kufanya
kazi kwa ufanisi na kuzuia upinzani na vikwazo mbalimbali katika
ujenzi wa Taifa.4 Tanzania ilihitaji kukimbia wakati wengine
wanatembea katika kukabiliana na changamoto za ujenzi wa Taifa
ili kujiletea maendeleo.5 Hivyo, ni vizuri mamlaka ya Rais
yaangaliwe kwa katika muktadha wa historia hii.

Taarifa
Taarifa hii ya utafiti imegawanywa katika sehemu kuu nane
zifuatazo: madaraka ya Rais na sababu zake, mamlaka ya kutoa
misamaha (prerogative of mercy), mamlaka ya kutangaza hali ya
hatari, nafasi ya Rais wakati wa uchaguzi, udhibiti wa madaraka ya
Rais na uwajibikaji, kinga ya Rais kushtakiwa, mamlaka yake ya
uteuzi na muhtasari wa mapendekezo.

1 Kifungu cha 55, Kama ilivyo juu.


2 Kifungu cha 59, Kama ilivyo juu.
3 Peter, C. M. (2000). Constitution Making in Tanzania: The Role of the People in

the Process. Dar es Salaam: University of Dar es Salaam.


4 Prempeh, K. (2008). Presidential Power in Comparative Perspective: The

Puzzling Persistence of Imperial Prseidency in Post-Authoritarian Africa. 35


Hastings Constitutional Law Quarterly 761, 784-795.
5 Nukuu ya Rais wa kwanza wa Tanzania “We must run while others walk”

kutoka kwa Mkandawire, T.(2011). Running While Others Walk: Knowledge and
the Challenge of Africa’s Development in Africa Development, Vol. XXXVI, No. 2,
2011, pp. 1– 36.
xv
Katika kuangalia madaraka ya uteuzi ya Rais utafiti ulipitia sheria
mbalimbali. Kwa kweli orodha ya wateule wa Rais ni ndefu. Orodha
hiyo ipo mwishoni mwa sehemu ya saba ya Taarifa hii. Katika
kuangalia madaraka mengine kama madaraka ya kutoa misamaha,
kutangaza hali ya hatari, utafiti ulijielekeza kujua ni kwa nini
kiongozi wa nchi anapewa madaraka kama hayo, namna
yanavyotekelezwa, changamoto na hatimaye mapendekezo ya
namna Katiba mpya inavyoweza kushughulikia changamoto hizo.
Kwa mfano, kuna maoni kuwa Rais aondolewe madaraka ya kutoa
misamaha ya adhabu (prerogative of mercy). Rais amepewa
madaraka ya kutoa misamaha (prerogative of mercy) ya adhabu kwa
“mtu yeyote” anayetumikia “adhabu yoyote” kuhusiana na “kosa
lolote.” Anaweza akapunguza adhabu kwa masharti au bila
masharti; anaweza akaibadilisha adhabu kuwa tahafifu au kuifuta
yote kabisa. Utafiti ulijaribu kuangalia na hatimaye kupendekeza
namna ya kuboresha utekelezaji wa madaraka hayo.

Hali kadhalika kuna maoni kuwa kinga ya Rais ya kutoshtakiwa


ifutwe. Utafiti ulijaribu kuangalia mantiki au falsafa ya kinga ya
kushtakiwa ambayo Rais amepewa na Katiba. Katika kufanya hivyo
utafiti ulifanya marejeo ya mashauri mbali mbali ya huko Marekani
ambako taasisi ya Urais imekuwepo kwa muda wa miaka mingi.
Nia na madhumuni ilikuwa ni kujua hasa misingi na falsafa ya
kinga ya kushtakiwa kwa kiongozi wa nchi.Vile vile utafiti
umejaribu kuangalia falsafa na mwelekeo wa sasa kuhusiana na
kinga ya kiongozi wa nchi. Mwishoni katika kila sehemu utafiti
umetoa mapendekezo katika muktadha wa falsafa, misingi pamoja
na changamoto zinazoikabili Taifa letu kwa sasa.

Aidha, kuna maoni mengi kuwa madaraka ya Rais yadhibitiwe na


kwamba kuwe na uwajibikaji. Utafiti umeangalia jinsi mihimili ya
Bunge na Mahakama inavyoweza kuyadhibiti mamlaka ya Rais na
changamoto zilizopo. Vile vile, nafasi ya wananchi katika
kuyadhibiti madaraka hayo imeangaliwa. Mwishowe, utafiti umetoa
mapendekezo ya namna Katiba mpya inavyoweza kuyadhibiti
madaraka ya Rais na kuongeza uwajibikaji.

Sehemu ya nane ya Taarifa hii ina muhtasari wa mapendekezo yote


yalitolewa katika kila sehemu. Nia na madhumuni ni kumpa
msomaji unafuu wa kufanya marejeo kwa haraka pindi anapohitaji.
Misingi au sababu ya mapendekezo hayo imeainishwa katika
matini kuu (main text).

xvi
SEHEMU YA KWANZA

1.1 MADARAKA YA RAIS NA SABABU ZAKE

1.1.1 Utangulizi
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Mkuu wa Nchi,
Kiongozi wa Serikali na Amiri-Jeshi-Mkuu.1 Majukumu haya
yanamfanya awe na madaraka makubwa ambayo wakati mwingine
yamezua hoja kuwa madaraka hayo ni makubwa sana kwa mtu
mmoja na yanahitaji kupunguzwa. Mkuu wa nchi ni kiongozi
mwenye madaraka ya kisiasa na kiutawala ya ngazi ya juu katika
nchi. Kiongozi wa nchi ni mtendaji mkuu wa kisiasa katika nchi,
mara nyingi akiongoza baraza la mawaziri. Sehemu hii itaainisha
madaraka yanayoambatana na nafasi hizi. Kwa kuanzia, sehemu
hii itaainisha aina kuu za wakuu wa nchi zilizopo katika dunia ya
sasa kabla ya kuangalia majukumu ya kiasili ya mkuu wa nchi bila
kujali mfumo wa kisiasa wa nchi. Kisha, sehemu hii itazungumzia
majukumu ya kiasili ya kiongozi wa serikali. Mwisho, sehemu hii
itaangalia asili ya Madaraka ya Rais kama yalivyo leo hii katika
katiba ya Tanzania.

1.1.2 Aina za Wakuu wa Nchi


Wakuu wa nchi huchukua sura mbalimbali kulingana na mifumo
ya siasa za nchi, hata hivyo tunaweza kuwaweka wakuu wa nchi
katika aina kuu nne. Kwanza, kuna mkuu wa nchi ambaye hana
madaraka ya kiutendaji, madaraka yake huwa ni ya kinadharia
zaidi, na utumiaji wa madaraka yake huwa ni alama tu (ceremonial
and symbolic roles). Kwenye mfumo huu, madaraka ya kiutendaji
yamewekwa kwa kiongozi wa serikali ambaye huwa ni mtu tofauti
na mkuu wa nchi. Mara nyingi, mkuu wa nchi hutumia madaraka
yake mbalimbali kwa mfano kufanya uteuzi wa watendaji wakuu
wa serikali, kulingana na ushauri wa kiongozi wa serikali. Nchi
ambazo zinafuata mfumo huo ni pamoja na nchi zinazofuata
mfumo wa kibunge kama vile Uingereza, Ujerumani, Israeli, India
na Italia na Uhispania. Wakati nchi zenye mfumo wa kifalme kama
Uingereza na Uhispania Mkuu wa Nchi huwa ni Mfalme au Malkia,

1 Ibara ya 33 (2) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977.


1
katika Jamhuri kama vile Ujerumani, Israeli, India na Italia Mkuu
wa Nchi huitwa Rais.

Pili, kuna mkuu wa nchi ambaye hana madaraka yeyote hata yale
ya kinadharia. Nafasi yake kubwa ni kuwa alama ya nchi na
mshikamano wa watu wa Taifa husika. Nchi zinazofuata mfumo
huo ni pamoja na Japan na kwa kiwango fulani Sweden. Mathalan,
ibara ya 1 ya Katiba ya Japan inatamka kuwa Mfalme wa Japan ni
alama ya nchi na mshikamano wa wananchi, “The Emperor shall be
the symbol of the State and of the unity of the People, deriving his
position from the will of the people with whom resides sovereign
power. " 1

Tatu, kuna mkuu wa nchi ambaye anachangia madaraka na


Kiongozi wa Serikali. Katika mfumo huu, kunakuwa na Rais
ambaye ni Mkuu wa nchi mwenye kuchangia madaraka ya
kiserikali na Waziri Mkuu. Kwa kawaida, Waziri Mkuu anateuliwa
na Rais kutoka kwenye chama chenye wabunge wengi. Waziri
Mkuu huwajibika kwa Rais na Bunge. Ufaransa imekuwa ikifuata
mfumo huu tangu kuanzishwa kwa katiba ya Mwaka 1958. Finland
ni mfano mwingine wa nchi zinazofuata mfumo huu.

Mwisho, aina ya nne ni pale ambapo Rais ni Mkuu wa Nchi na


Mkuu wa Serikali. Marekani ni nchi ya kwanza kuwa na mfumo
huo. Nchi zingine ambazo zimefuata mfumo huo ni pamoja na
Brazil, Venezuela na Mexico.

1.1.3 Mkuu wa Nchi


Kama ilivyobainishwa kwenye utangulizi, dhana ya mkuu wa nchi,
inatumika kubainisha kiongozi mwenye kushika nafasi ya juu
kuliko zote katika nchi huru na mwenye madaraka ya moja kwa
moja au yasiyo ya moja kwa moja (direct or implied powers) ya
kufanya kazi zinazohitaji mamlaka ya juu katika nchi. Madaraka ya
mkuu wa nchi yanaweza kutofautiana kulingana na aina ya mkuu
wa nchi iliyopo kwenye nchi lakini pia kulingana na katiba ya nchi.
Hata hivyo, majukumu ya kiasili ya mkuu wa nchi ni pamoja na
kuwa mwakilishi mkuu wa wananchi, mtendaji mkuu, Amiri-Jeshi-
Mkuu na mwanadiplomasia mkuu. Kwa kiingereza, Mkuu wa nchi

1 The Constitution of Japan of 1946


2
ni, “chief public representative, chief executive, commander-in-chief of
armed forces na chief-diplomat.”1

1.1.4 Mwakilishi Mkuu wa Wananchi


Mkuu wa nchi amepewa madaraka ya kuwakilisha nchi na watu
wake katika masuala mbalimbali ndani na nje ya nchi. Kwa
jukumu hili, mkuu wa nchi ni nembo inayoishi ya Taifa lake.
Aliyekuwa Rais wa Zamani wa Ufaransa, Charles de Gaulle, aliwahi
kutamka kuwa Rais wa Ufaransa kama Mkuu wa Nchi lazima
awakilishe na kubeba tunu za kitaifa ndani na nje ya nchi. Kwa
Kiingereza, "the head of state must embody the spirit of the nation
for the nation itself and the world".2 Kwa sababu hiyo mkuu wa
nchi ni alama ya utaifa na umoja wa nchi. Kanada wanamuita
Mkuu wao wa nchi, ambaye ni Malkia wa Uingereza, kuwa ni alama
ya nchi na ni nembo ya uaminifu, umoja na mamlaka ya Wakanada
wote. “The Queen personifies the state and is the personal symbol of
allegiance, unity and authority for all Canadians.” Kwa sababu
hiyo, wabunge, mawaziri, wakuu wa majeshi na watumishi wa
umma hula kiapo cha utii kwake.3

Kama alama ya Taifa, miongoni mwa alama zingine kama bendera,


sarafu na noti za fedha, katika nchi nyingi, picha ya mkuu wa nchi
huwekwa kwenye ofisi za Serikali, mahakamani, majengo ya umma,
maktaba n.k. Mkuu wa nchi pia hushiriki kwenye dhifa mbalimbali
za kitaifa ndani na nje ya nchi kwa niaba ya wananchi wote. Kwa
wadhifa huo huo, mkuu wa nchi, pia hupokea wageni muhimu wa
kitaifa kwenye dhifa za kitaifa. Pia, akiwa mwakilishi wa wananchi
wote, mkuu wa nchi hutoa nishani za kitaifa kama njia ya
kutambua mchango uliotukuka katika masuala ya nchi kwa baadhi
ya raia na hata kwa wageni. Mfano: Ibara ya 87, kifungu cha 8 cha
Katiba ya Italia kinasema: President shall confer the honorary
distinctions of the Republic. Maana yake, Rais atatoa nishani
zilizotukuka kwa niaba ya Jamhuri. Pia, kwa niaba ya wananchi,
Rais amepewa mamlaka ya kuwa mkuu wa nchi na kutoa
misamaha ya huruma kwa watu waliotiwa hatiani kwa makosa
mbalimbali. Mfano, Ibara ya 60(2) ya Katiba ya Ujerumani,

1 Palmer, M., (1997), Comparative Politics: Political Economy, Political Culture, and
Political Interdependence, F.E. Peacock Publishers, Inc. Soma pia, Hauss, C.,
(1999), Comparative Politics: Domestic Responses to Global Challenges, 3rd
Edition, Wadsworth.
2 Charles de Gaulle, Mémoires de guerre, tome 1, Plon, 1954.
3 The Queen's role in Canada, Royal Household. Retrieved on 2013-08-01.

3
inasema: “The President shall exercise the power to pardon
individual offenders on behalf of the Federation; wakati Ibara ya 17
ya Katiba ya Ufaransa inasema: The President of the Republic is
vested with the power to grant individual pardons.” Tafsiri ya katiba
hizi mbili ni kuwa Rais amepewa madaraka ya kusamehe watu
waliotiwa hatiani kwa niaba ya nchi.

Akiwa ni mwakilishi mkuu wa wananchi, mkuu wa nchi, hasa kwa


nchi zinazofuata mfumo wa kibunge, ana majukumu ya ki-ishara
(symbolic role) kufungua Bunge wakati linapoanza na kulivunja
Bunge muda wake unapoisha. Pia, nchi nyingi zimempa madaraka
ya kuwa mkuu wa nchi na madaraka ya kusaini miswada ya sheria
kabla ya kuwa sheria.1

1.1.5 Mtendaji Mkuu wa Nchi (chief executive)


Mkuu wa nchi ni mtendaji mkuu wa nchi mwenye majukumu ya
kufanya maamuzi makubwa ya kitaifa na kutoa uongozi kwa nchi.2
Kwa jukumu hilo, mkuu wa nchi huteua serikali na kusimamia
utendaji wake. Pale, ambapo mkuu wa nchi hana mamlaka ya
kiutendaji madaraka ya kiutendaji huwapo kinadharia zaidi.
Kwenye nchi zenye mkuu wa nchi mtendaji, mamlaka ya juu ya
kidola huwa mikononi mwake.

Pamoja na kuteua kiongozi wa serikali, kwa kawaida mkuu wa nchi


huteua viongozi muhimu wa mahakama kama majaji na watendaji
wengine wa nafasi za juu katika uongozi wa umma. Utaratibu huu
huwa bayana zaidi kwenye nchi kama Uingereza ambapo mkuu wa
nchi ni tofauti na kiongozi wa serikali. Kwenye nchi zinazofuata
mfumo huo, kwa kawaida mamlaka ya uteuzi huwa ni alama tu
(ceremonial) kwani uteuzi hufanyika kulingana na mapendekezo ya
kiongozi wa serikali. Katika mifumo hiyo, uteuzi wa kiongozi wa
serikali huwa ni alama tu kwani mteuliwa huwa kwa kawaida ni
kiongozi wa chama chenye wabunge wengi. Mkuu wa nchi pia
huwaondoa madarakani wateule wake katika nafasi zao kwa
kufuata ushauri wa kiongozi wa serikali. Kwenye nchi zinazofuata

1 Sykes, Patricia Lee (1989). The President as Legislator: A "Superepresenator"


Presidential Studies Quarterly, Vol. 19, No. 2, Counsel for the New President
(SPRING1989), pp. 301-315.
2 Ferguson, Margaret Robertson (2003). Chief Executive Success in the Legislative

Arena, State Politics & Policy Quarterly, Vol. 3, No. 2 (Summer, 2003), pp. 158-
182.

4
mfumo wa Kirais kama Marekani na Brazil ambapo mkuu wa nchi
vilevile ni kiongozi wa serikali, mkuu wa nchi hufanya uteuzi kwa
nafasi za juu za uongozi wa umma kama vile mawaziri na majaji
kama anavyoona yeye, isipokuwa, kwa baadhi ya nchi kama
Marekani uteuzi wake huthibitishwa na Bunge.

Ni kawaida kwa katiba za nchi kutamka bayana kuwa mkuu wa


nchi ndiye mtendaji mkuu. Hali hii inakuwa wazi zaidi katika nchi
kama Marekani na Brazil ambapo mkuu wa nchi pia ni mkuu wa
serikali. Kwa mfano, Ibara ya 2, Kifungu cha 1 cha Katiba ya
Marekani kinasema: “The executive Power shall be vested in a
President of the United States of America.” Maana yake ni kuwa,
madaraka ya kiutendaji yatakuwa chini ya Rais wa Marekani. Vivyo
hivyo, Ibara ya 76 , kifungu 1 Katiba ya Brazil imetamka kuwa: The
Executive Power is exercised by the President of the Republic,
assisted by the Ministers of State. Maana yake ni kuwa: Madaraka
ya Kiutendaji yatakuwa chini ya Rais wa Jamhuri, akisaidiwa na
Mawaziri wa Nchi.

Lakini, hata katika mifumo ya siasa ambapo mkuu wa nchi hana


madaraka ya kiutendaji kama vile India, bado mamlaka hayo
huwekwa kwake na huchukuliwa kuwa serikali inatekeleza
madaraka hayo kwa niaba ya mkuu wa nchi. Ibara ya 53(1) ya
Katiba ya India inasema kuwa: “The executive power of the union
shall be vested in the President and shall be exercised by him either
directly or indirectly through the officers subordinate to him in
accordance to the Constitution.” Maana yake, madaraka ya
kiutendaji ya Serikali yatakuwa chini ya Rais na yatatumiwa na
yeye moja kwa moja au kwa kutumia maofisa watakao kuwa chini
yake kulingana na Katiba.

1.1.6 Mwanadiplomasia Mkuu (Chief Diplomat)


Mkuu wa nchi ndiye mhusika mkuu katika mahusiano ya nchi
yake na mataifa mengine. Mkuu wa nchi anatambulisha mabalozi
wa nchi yake kupitia hati za utambulisho wao kwa wakuu wa nchi
wanakotumwa (Letter of Credence). Pia, Mkuu wa nchi, hupokea
hati za utambulisho wa mabalozi wa nchi zingine kwenye nchi
yake. Bila kupata vibali hivyo mabalozi hawawezi kupewa hadhi za
kibalozi. Majukumu ya Mkuu wa nchi kuhusiana na suala hilo
yamewekwa kwenye Mkataba wa Vienna. Ibara ya 14 ya Mkataba

5
wa Vienna inatambua kuwa mabalozi wa nchi za kigeni ni lazima
wakubalike na mkuu wa nchi inayowapokea.

Pia, mkuu wa nchi ana madaraka ya kuingia kwenye mikataba


mikubwa ya kimataifa kwa niaba ya nchi (High contracting party in
international treaties). Mkuu wa nchi anaweza kusaini mwenyewe
au anaweza kukasimu madaraka ya kusaini mikataba hiyo kwa
maafisa wa serikali kama mawaziri au mabalozi.

Ibara ya 59(1) ya Katiba ya Ujerumani inasema: “The Federal


President shall represent the Federation in its international relations.
He shall conclude treaties with foreign states on behalf of the
Federation. He shall accredit and receive envoys”. Inamaanisha
kuwa, Rais wa Shirikisho atawakilisha Shirikisho kwenye
mahusiano ya kimataifa. Ataingia kwenye mikataba na mataifa ya
kigeni kwa niaba ya shirikisho. Atatoa vibali na kupokea mabalozi
wa nchi zingine.” Ibara ya 14 ya Katiba ya Ufaransa inatamka
kuwa: “The President of the Republic shall accredit ambassadors and
envoys extraordinary to foreign powers; foreign ambassadors and
envoys extraordinary shall be accredited to him.” Maana yake ni
kuwa Rais wa Jamhuri atatoa hati za utambulisho kwa mabalozi
kwa mamlaka za nje; mabalozi na wawakilishi wa nje watapewa
vibali naye.

1.1.7 Amiri-Jeshi-Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama katika


Nchi
Mkuu wa nchi ni kiongozi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama.
Mkuu wa nchi hufanya maamuzi kuhusu masuala muhimu
kuhusiana na majeshi ya ulinzi na usalama kama vile kazi na
majukumu yao, vifaa walivyo navyo na kuingia ama kutoka vitani.
Hivyo, wakuu wa vikosi vya majeshi ya ulinzi na usalama
wanapaswa kupokea amri kutoka kwa mkuu wa nchi. Hata hivyo,
kwa nchi ambayo, mkuu wa nchi siyo mtendaji, madaraka yake juu
ya majeshi hutegemea ushauri wa kiongozi wa serikali. Hiyo ina
maana, kihalisia, madaraka kamili ya kijeshi huwa kwa kiongozi wa
serikali. Amiri-Jeshi-Mkuu pia, huwapandisha vyeo maafisa wa
jeshi na kuwapa nishani kutambua mchango wao kwa nchi.

Hivyo, kwa kawaida, katiba hutamka kuwa mkuu wa nchi ni Amiri-


Jeshi-Mkuu hata katika nchi ambazo mkuu wa nchi siyo mtendaji.
Mfano, ibara ya 87 ya Katiba ya Italia, kifungu cha 4 inasema

6
kuwa: The President is the commander-in-chief of the armed forces,
shall preside over the Supreme Council of Defense established by
law, and shall make declarations of war as have been agreed by
Parliament. Maana yake ni kuwa, Rais atakuwa ni Amiri
JeshiMkuu, akiongoza baraza la Ulinzi lililowekwa kisheria na
kwamba Rais atatangaza vita kadiri ya maamuzi ya Bunge. Vile vile
katika katiba ya Kanada, inatamka kuwa Amiri-Jeshi-Mkuu wa
Majeshi yote ya Kanada yatakuwa chini ya Malkia.1

Mkuu wa nchi anakuwa ni kamanda mkuu si tu wa majeshi yaliyo


chini ya serikali kuu bali hata migambo inapoitwa kutoa huduma
kwa nchi. Ibara ya II, Kifungu cha 2 cha Katiba ya Marekani
kinasema:

The President shall be Commander in Chief of the Army and Navy of


the United States, and of the Militia of the several States, when
called into the actual Service of the United States. Maana yake ni
kuwa, Rais atakuwa Kamanda Mkuu wa Majeshi ya Marekani, na
Migambo ya Majimbo mbalimbali, pale yanapoitwa kutoa huduma
kwa Marekani.

1.1.8 Kiongozi wa Serikali


Kwa kawaida, kiongozi wa serikali ni mtendaji mkuu wa serikali
(chief of the executive branch) mwenye jukumu la kusimamia
uendeshaji wa shughuli za serikali. Nafasi ya kiongozi wa serikali
huwa bayana kwenye nchi zinazotenganisha nafasi ya Mkuu wa
Nchi na kiongozi wa serikali. Mara nyingi pia, kiongozi wa serikali
huwa pia ni kiongozi wa chama tawala (au ushirikiano wa vyama).
Hata hivyo, majukumu ya mkuu wa nchi hutegemea katiba ya nchi
husika. Kwa mfano, ibara ya 74 ya Katiba ya Ethiopia
inaorodhesha majukumu ya Waziri Mkuu, ambaye ndiye kiongozi
wa serikali kuwa ni pamoja na kuwa mtendaji mkuu wa serikali,
mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri na Amiri-Jeshi-Mkuu;
kupendekeza majina ya mawaziri kwa Bunge. Mengine ni pamoja
na kusimamia utekelezaji wa sheria, sera, mipango na maamuzi ya
bunge. Waziri Mkuu, pia huongoza baraza la mawaziri, anatekeleza
sera ya nchi juu ya mambo ya nchi. Hali kadhalika, waziri mkuu,
anasimamia utawala wa Serikali ya Muungano, anateua watumishi
wa serikali ya Muungano.

1 Ibara ya III, Kifungu cha 15 cha the Constitution Act, 1867.


7
Pale ambapo mkuu wa nchi na kiongozi wa serikali wanachangia
madaraka ya kiserikali kama ilivyo kwa nchi za Ufaransa na
Finland, madaraka ya kiongozi huwa ni kuongoza shughuli za kila
siku za serikali ndani na nje ya bunge. Katiba hubainisha
madaraka ya kiongozi wa serikali na yale ya mkuu wa nchi. Mfano,
Kifungu cha 57 cha Katiba ya Finland inabainisha madaraka ya
Rais, akiwa mkuu wa nchi na pia mwenye madaraka ya kiserikali
wakati madaraka ya waziri mkuu kama kiongozi wa serikali
yamewekwa kwenye kifungu cha 66. Wakati majukumu ya Rais ni
pamoja na kumteua waziri mkuu na mawaziri, kuitisha bunge
wakati wa dharura, Majukumu ya Waziri Mkuu ni kuelekeza Hata
hivyo, mara nyingi, mkuu wa nchi huwa ni pamoja na ulinzi na
sera ya mambo ya nje. Kwenye, mifumo ambayo nafasi ya mkuu
wa nchi na kiongozi wa serikali zimeunganishwa kama vile
Marekani na Brazili, majukumu ya mkuu wa nchi na kiongozi wa
serikali huwekwa pamoja kwenye katiba kwa kuwa hayo huwa
chini ya mtu mmoja.

Katika kusimamia utekelezaji wa shughuli za kila siku za serikali,


kiongozi wa serikali hupewa majukumu ya kufanya uteuzi wa
watendaji mbalimbali na kusimamia utendaji wao. Pia, kiongozi wa
serikali, huwajibika kupeleka miswaada ya kutengeneza sheria
bungeni na kusimamia utekelezaji wa sheria za nchi. Kiongozi wa
serikali anawajibika kuwa na majukumu mengine ambayo ni
pamoja na kufanya maamuzi ya kisera kwa nchi.

1.1.9 Hali ilivyo Tanzania


Ibara ya 33(2) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
1977 inatamka kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
ni Mkuu wa Nchi, Kiongozi wa Serikali na Amiri-Jeshi-Mkuu. Vivile
kama ilivyo, kwenye mifumo ya kibunge, utamaduni uliopo ni kuwa
Rais pia huwa ni kiongozi wa chama chake. Ibara ya 34 inaeleza
kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano ana madaraka yote juu ya
Serikali ya Jamhuri ya Muungano na yale yahusuyo Tanzania Bara.
Madaraka hayo ya Rais anaweza kuyatekeleza yeye mwenyewe au
kwa kukasimu kwa watu wengine. Nafasi zote zilizotajwa hapo juu,
kama itakavyoonekana kwenye taarifa zinaambatana na madaraka
makubwa Kwa Rais. Hapa chini Taarifa inajaribu kudodosa ni kwa
nini Rais alipewa madaraka makubwa kiasi hicho.

8
Kama ilivyotajwa hapo juu, pamoja na Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kuwa ni Mkuu wa Nchi, Kiongozi wa
Serikali na Amiri-Jeshi-Mkuu, utamaduni wa chama tawala (CCM)
umekuwa pia ukimpa Rais kofia ya kuwa ni Kiongozi Mkuu wa
Chama chake. Kama tulivyoona miongoni mwa majukumu ya
Mkuu wa nchi ni pamoja na kuwa nembo ya umoja na
mshikamano wa wananchi wote (A symbol of national unity and
solidarity). Hivyo, ingawa utamaduni wa Rais kuwa pia kiongozi wa
chama unaweza kuwa ulifaa katika mfumo wa chama kimoja,
ndani ya mfumo wa vyama vingi, utaratibu unaweza ukaathiri
nafasi ya Rais kama alama ya umoja na mshikamano wa wananchi
wote. Mfano, Rais anapotembelea eneo fulani la nchi huku akiwa
amevaa nembo za chama chake, ni rahisi kwa wananchi wasio
wanachama wa chama chake kujisikia kuwa siyo kiongozi wao.
Kama Mkuu wa nchi Rais anapaswa kuwa alama ya umoja na
mshikamano wa kitaifa, na kiongozi wa wananchi wote katika
muda wote.

Pili, kwa kuwa Rais ni Mkuu wa nchi na Kiongozi wa Serikali, Rais


ana majukumu mengi, hivyo inafaa asiwe kiongozi wa chama ili
aweze kuelekeza nguvu na muda wake katika kuendesha serikali
na kuiongoza nchi. Siasa za chama zifanywe na watu wengine wa
chama chake. Mathalan, mfumo huu unatumika katika nchi ya
Marekani ambako taasisi ya Urais imekomaa. Hivyo,
inapendekezwa kuwa ingawa Rais atapendekezwa na chama chake,
Katiba imzuie kushika nafasi za uongozi wa chama.

1.2 HISTORIA FUPI YA MADARAKA YA RAIS

1.2.1 Katiba ya Uhuru, 1961


Muda mfupi baada ya uhuru utaratibu wa kikatiba ulikuwa tofauti
na sasa. Kama ilivyoelezwa katika Mapendekezo ya Serikali ya
Kuanzishwa kwa Jamhuri ya mwaka 1962, Tanganyika ilikuwa
nchi yenye utawala wa Ufalme (Monarchy) kwa sababu Malkia wa
Uingereza (akiwakilishwa na Gavana) alikuwa ni Mkuu wa Nchi.1
Vilevile, kwa mujibu wa Katiba ya Uhuru [The Tanganyika

1Government of Tanganyika, Proposals of the Tanganyika Government for a


Republic, Government Printer, Dar es Salaam, p.1.
9
(Constitution) Order-in-Council, 1961] Gavana alikuwa ni Amiri-
Jeshi-Mkuu. Waziri Mkuu alikuwa ni Kiongozi wa Serikali tu.

1.2.2 Katiba ya Jamhuri ya Mwaka 1962


Katiba ya Jamhuri ya Mwaka 1962 ilifanya mabadiliko makubwa
sana. Mamlaka yote yaliyokuwa chini ya Gavana na yale ya Waziri
Mkuu yaliunganishwa na kuwa chini ya Rais wa Jamhuri. Kwa
mfano, Ibara ya 3 ya Katiba ya Jamhuri iliainisha hivi;

(1) There shall be a President of Tanganyika who shall


be the Head of State and Commander-in-Chief of the
Armed Forces.
(2) The executive power of the Republic is vested in the
President.
(3) Except as may be otherwise provided by law, in the
exercise of his functions, the President act in his own
discretion and shall not be obliged to follow advice
tendered by any other person.

Ibara hii inaainisha kuwa Rais ni Mkuu wa Nchi na Amiri-Jeshi-


Mkuu. Madaraka ya kiutendaji pia yalikuwa kwake. Ibara hiyo pia
ilitamka kuwa Rais atatekeza madaraka yake kufuatana na hiari na
busara yake na hatolazimika kufuata ushauri wa mtu mwingine
yeyote. Kama anavyosema Wambali, Katiba ya Jamhuri ya Mwaka
1962 ilimpa Rais madaraka mengi yanayofanana na yale aliyokuwa
nayo Gavana kabla ya Uhuru.1

Katiba ya Jamhuri ya Mwaka 1962 ilianzisha Ofisi ya Rais na


kuainisha madaraka yake kwa ujumla. Madaraka mengine
yamekuwa yakifafanuliwa na kuongezwa na Katiba zilizofuata
pamoja na sheria nyingine kutoka na mahitaji ya nyakati husika.
Hivyo, madaraka ya Rais pia yameainishwa katika sheria nyingi.
Mfano, madaraka ya kuwaweka watu kizuizini, kuwahamisha watu
kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine, kutoa msamaha
kwa wafungwa, kuwateua watu kushika nafasi mbalimbali za
serikali, kusaini miswada ya sheria, kulivunja Bunge, kutangaza
hali ya hatari, na kadhalika.

1 Wambali, Michael K.B., “The Historical Overview of the Constitutional Reforms


towards Limited Leadership in Tanzania”, in Commonwealth Law Bulletin, Vol. 34
No.2 (June 2008), pp.277-296, at p.279-280.
10
1.2.3 Sababu za Rais kupewa madaraka makubwa

Inafaa kujiuliza, kwa nini Rais wa Jamhuri ya Muungano amepewa


madaraka mapana sana? Sababu kadhaa zinaweza kutolewa katika
kujibu swali hili. Kwanza, moja ya changamoto ambayo iliikumba
Serikali ya TANU mara baada ya uhuru ilikuwa ni viongozi wake
kuwa na fikira au mtazamo wa kuishi kama ambavyo Wakoloni
walikuwa wakiishi. Coulson aliandika kuwa baada ya uhuru
viongozi wengi na watumishi wa Serikali walitaka “kuvuna
matunda ya uhuru.”1 Walifikiria kusafiri kwenye magari mazuri
kama waliyokuwa nayo Wakoloni; wengine walitaka mishahara
mizuri kama ambavyo Wazungu walikuwa wakilipwa; wanajeshi
nao walitaka vyeo vikubwa kama vile vya maofisa wa kijeshi
wazungu na madai hayo yalisababisha maasi ya mwaka 1964.2
Aidha, vyama vya wafanyakazi viliendesha migomo kudai maslahi
bora.3 Wakati wa Mwafrika kupata kila alichokuwa akikipata
Mzungu na wengine kabla ya uhuru ulikuwa umefika! Ili kudhibiti
hali hii ilibidi kuwa na Rais mwenye mamlaka makubwa ili
kuwadhibiti viongozi na watumishi hawa kinidhamu.

Pili, ujenzi wa umoja wa taifa (nation-building) umekuwa ikitajwa


kuwa ni sababu muhimu ya kuanzishwa kwa ofisi ya Rais mwenye
madaraka mengi. Mwalimu Nyerere alisema kuwa makabila mengi
ya Tanganyika yalikuwa hayajawahi kuwa katika utawala wa aina
moja mpaka walipokuja Wakoloni.4 Hivyo, kulikuwa na umuhimu
wa kuwa na Serikali yenye mamlaka thabiti ili iweze kuleta umoja
wa kitaifa.5 Kuhusiana na hili, alisema;

“… the very nature of the new [African] countries themselves:


they are usually countries without natural unity. Their
"boundaries" enclose those artificial units carved out of Africa

1 Coulson, Andrew, (1982), Tanzania: A Political Economy, Oxford University


Press, New York, pp. 135-144.
2 Mazrui, Ali A., “Anti-Militarism and Political Militancy in Tanzania”, in The

Journal of Conflict Resolution, Vol. 12, No. 3 (Sep., 1968), pp. 269-284, p.273.
3 Coulson, Andrew, (1982), Tanzania: A Political Economy, Oxford University

Press, New York, p.135.


4 Nyerere, Julius, “One-Party Government”, in Transition, No. 75/76, The

Anniversary Issue: Selections from Transition, 1961-1976 (1997), pp. 156-161, at


pp.159-160.
5 Kama ilivyo hapo juu.

11
by grabbing colonial powers without any consideration of
ethnic groups or geographical realities, so that these countries
now include within their borders tribal groups which, until the
coming of the European powers, had never been under one
government…”1

Katika nukuu hii Mwalimu Nyerere alisema kuwa nchi nyingi za


Afrika zilikuwa na changamoto ya kutokuwa na umoja kwa sababu
zina wananchi wenye asili tofauti. Changamoto kubwa ilikuwa ni
kuyaunganisha makabila mbalimbali na kuyafanya yajione kuwa
ni nchi moja. Ili kufanikisha hili kiongozi wa Serikali mwenye
madaraka mapana zaidi alihitajika. Hivyo, kujenga umoja wa kitaifa
vilevile ndiyo sababu kuu ya kuanzishwa kwa mfumo wa
demokrasia ya chama kimoja cha siasa mwaka 1965. Mwalimu
Nyerere alisema kuwa katika nchi changa iliyokuwa inajaribu
kujenga umoja wa kitaifa na kuleta maendeleo tofauti na
demokrasia ya kupingana havikuwa na nafasi.2 Kutokana na
msimamo huu, kama anavyoeleza Coulson, vyama vya Wafanyakazi
vilidhibitiwa; haki ya kugoma iliondolewa; viongozi wa kijadi
waliondolewa na nafasi zao kushikwa na watumishi walioteuliwa
kutoka Serikali Kuu; mashirika ya umma yenye viongozi wa juu
walioteuliwa na Rais yalianzishwa; na viongozi wa chama wakawa
na nguvu.3 Mabadiliko haya yaliifanya Serikali Kuu na Rais kuwa
na mamlaka ya kudhibiti mambo mengi kwa nia ya kuleta
maendeleo ya haraka na kujenga umoja wa kitaifa.

Tatu, sababu nyingine ambayo imeelezwa ni kuleta maendeleo na


kuboresha maisha ya wananchi. Kuhusiana na sababu hii
Mapendekezo ya Kuanzishwa kwa Jamhuri ya Mwaka 1962,
pamoja na mambo mengine, yanataja sababu ya Mabadiliko;

Tanganyika is a young nation, faced with tremendous


problems of nation-building and economic development. Our
nationalism is a young nationalism, born of the desire to unite
and free ourselves from the shackles of colonialism. While we
must guard against narrow, exclusive form of nationalism,
which can lead to dangerous international rivalries, we need

1Kama ilivyo hapo juu.


2Kama ilivyo hapo juu, uk. 158.
3 Coulson, Andrew, (1982), Tanzania: A Political Economy, Oxford University

Press, New York, p.4.


12
to foster our sense of nationhood within the larger context of
African family of nations and the international community. We
are also faced with tremendous problem of achieving the rapid
economic development of our country in order to raise the
standard of living of our people. A sense of nationhood, and
the need to mobilize the physical and spiritual resources of the
country in the task of development are inseparable.
Government believes that our Republican Constitution should
be such as to enanble our country to meet these challenges.1

Nukuu hii inaeleza kuwa Katiba ya Jamhuri ya Mwaka 1962,


ambayo ndiyo iliyoanza kuainisha mamlaka makubwa kwa ofisi ya
Rais, lengo kubwa ilkuwa ni kujaribu kufanikisha masuala
makubwa mawili. Kwanza, kujenga umoja wa kitaifa (nation-
building) na pili, kuleta maendeleo ili kuboresha hali ya maisha ya
wananchi ambayo ilikuwa chini. Mfano, kutokana na madaraka
hayo Rais aliweza kuamuru watu wahamishwe kwenda kwenye vijiji
vya ujamaa ili waeze kupata huduma za elimu na afya.2

1.3 HITIMISHO
Sehemu hii imeainisha madaraka ya Rais kwa ujumla. Imejaribu
kuonyesha baadhi majukumu makuu ya kiasili (traditional roles)
yanayoambatana na ofisi ya Rais. Rais ni Mkuu wa Nchi, Kiongozi
wa Serikali na Amiri-Jeshi-Mkuu. Kama mkuu wa nchi baadhi ya
majukumu ya Rais ni pamoja na kuwa mtendaji mkuu wa Serikali,
mwanadiplomasia mkuu, mwakilishi mkuu wa wananchi, n.k.
Ingawa majukumu ya viongozi wa nchi yanafanana, utawala na
aina ya uongozi unatokana na utamaduni, historia, na mazingira
ya nchi husika. Hivyo, madaraka ya sasa yanaakisi changamoto,
mazingira na historia ya nchi.

Kama ilivyoelezwa, Katiba ya Jamhuri ya Mwaka 1962 (The


Republican Constitution, 1962) ndiyo iliyoanzisha taasisi ya Urais.
Iliondoa mfumo wa utawala wa kifalme uliowekwa na Katiba ya
Uhuru ya Mwaka 1961. Katiba ya Jamhuri ya Mwaka 1962 ndiyo
iliyoainisha mamlaka makubwa ya Rais. Vilevile madaraka mengine

1 Government of Tanganyika, Proposals of the Tanganyika Government for a


Republic, Government Printer, Dar es Salaam, pp.1-2.
2 Angalia Pratt, Cranford, “Julius Nyerere: Reflections on the Legacy of His

Socialism”, in Canadian Journal of African Studies / Revue Canadienne des


Études Africaines, Vol.33, No. 1 (1999), pp. 137-152, p.139.
13
mengi ya Rais yameainishwa na sheria nyingi za kawaida. Katiba ya
sasa na sheria nyingi zinazoainisha madaraka ya Rais zilitungwa
wakati wa uongozi wa Mwalimu Nyerere. Waandishi kama Pratt na
Coulson wanasema alipewa madaraka yote hayo ili kumuwezesha
kukabiliana na changamoto zilizokuwepo wakati huo. Pratt
anaziainisha changamoto hizo katika mafungu manne: (i) kukuza
uchumi na kuboresha maisha ya wananchi, (ii) kuwa na udhibiti
wa mwelekeo wa uchumi wa taifa, (iii) kuwa na demokrasia
shirikishi lakini bila migawanyiko chini ya uongozi wake na TANU,
na (iv) kujenga jamii yenye usawa kiuchumi ambayo watu wote
wangefaidika na maendeleo yanayopatikana.1 Inaweza kuelezwa
kuwa hizi ndizo zilikuwa ndoto kuu au malengo makuu ya
Mwalimu Nyerere na Serikali yake. Ili aweze kufanikisha au kufikia
malengo hayo ilibidi apewe madaraka makubwa — madaraka
ambayo yangemuweza yeye na Serikali kufanya maamuzi magumu
na makubwa kwa haraka. Hivyo, Serikali iliweza kubinafisisha
mabenki, kutaifisha ardhi, kutaifisha majumba, kufuta tawala za
kijadi zilizokuwa na mwelekeo wa kikabila, kufuta vyama vya siasa
na kubakisha chama kimoja tawala, kufuta serikali za mitaa
mwaka 1972, kuhamisha wananchi na kuwapeleka katika vijiji vya
ujamaa ili wawe karibu huduma za zahanati na shule, n.k.

1 Kama ilivyo hapo juu, k. 138-139.


14
SEHEMU YA PILI

2.1 MAMLAKA YA KUTOA MISAMAHA


(PREROGATIVE OF MERCY)

2.1.1 Hoja
Kuna hoja kuwa madaraka ya Rais ya kuwasamehe wafungwa na
kupunguza adhabu zao yaondolewe. Sababu kadhaa zinatolewa
katika kuunga mkono hoja hii. Kwanza, kuna watu wanafikiri kuwa
madaraka hayo hayana maana kwa sababu wanaosamehewa ni
watu ambao walipewa adhabu kwa mujibu wa sheria. Pili, kuna
wengine wanafikiria kuwa madaraka hayo yamekuwa yakitumiwa
vibaya na kwa upendeleo fulani. Tatu, kuna maoni kuwa rushwa
hutolewa huko magerezani ili wahusika wapendekezwe kupewa
msamaha au wapunguziwe adhabu na Rais. Nne, kuna watu
wanaona kuwa kuwasamehe watu waliopewa adhabu na
Mahakama kwa mujibu wa sheria, Rais huingilia utendaji wa
Mahakama. Tano, kuna maoni kuwa msamaha umekuwa
ukiwaachilia wahalifu hatari ambao huleta matatizo makubwa
katika jamii.

2.1.2 Mamlaka ya Kusamehe Makosa katika Katiba ya Jamhuri


ya Muungano wa Tanzania
Ibara ya 45 ya Katiba ya sasa inampa Rais madaraka ya kusamehe
au kupunguza adhabu kwa watu waliopewa adhabu au
wanaotumikia adhabu (prerogative of mercy). Kwa jinsi ibara hii
ilivyoandikwa, madaraka haya ni mapana sana. Rais amepewa
madaraka ya;

 kutoa msamaha kwa mtu yeyote aliyepatikana na hatia


mbele ya Mahakama kwa kosa lolote, na aweza kutoa
msamaha huo ama bila ya masharti au kwa masharti;

 kumwachilia kabisa au kwa muda maalum mtu yeyote


aliyehukumiwa kuadhibiwa kwa ajili ya kosa lolote ili mtu
huyo asitimize kabisa adhabu hiyo au asitimize adhabu hiyo
wakati wa muda huo maalum;

15
 kuibadilisha adhabu yoyote aliyopewa mtu yeyote kwa kosa
lolote iwe adhabu tahafifu;

 kufuta adhabu yote au sehemu ya adhabu yoyote aliyopewa


mtu yeyote kwa ajili ya kosa lolote au kufuta adhabu yote au
sehemu ya adhabu ya kutoza, au kuhozi (au kuchukua) kitu
cha mtu mwenye hatia ambacho vinginevyo kingechukuliwa
na Serikali ya Jamhuri ya Muungano.

Madaraka haya ni makubwa na mapana sana. Ibara ya 45 (2) ya


Katiba imetoa mamlaka kwa Bunge kutunga sheria ambayo
itaelekeza namna Rais atakavyotekeleza mamlaka hayo lakini
mpaka sasa sheria hiyo haijatungwa. Hata hivyo, kwa namna
ambavyo ibara ya 45 ya Katiba inatoa madaraka mapana ni vigumu
kutunga sheria inayodhibiti madaraka hayo. Mathalan, sheria
haiwezi kusema Rais hatawasamehe watu waliofanya makosa fulani
kwa sababu Katiba inampa madaraka ya kutoa msamaha
kuhusiana na “kosa lolote.” Aidha, sheria ikisema Rais
hatawasamehe wahalifu wa aina fulani itakuwa inakinzana na
Katiba kwa sababu Katiba imempa Rais madaraka ya kumsamehe
“mtu yeyote” anayekabiliwa na “adhabu yoyote.” Hivyo, ni vigumu
kutunga sheria kudhibiti mamlaka ya Rais ya kusamehe,
kupunguza au kufuta kabisa “adhabu yoyote” inayomkabili “mtu
yeyote” kuhusiana na “kosa lolote.”

2.1.3 Dhana ya Madaraka ya kutoa msamaha


Hapa Tanzania utaratibu wa kiongozi wa nchi kuwa na madaraka
ya kutoa misamaha kwa watu wanaotumikia adhabu umerithiwa
kutoka kwa wakoloni wa kiingereza. Kwa utaratibu na utamaduni
wa Kiingereza ulioanza karne ya 16, Mfalme amepewa madaraka
kumhurumia mtu yeyote aliyepewa adhabu yoyote.1 Ni “mamlaka
ya kipekee” ya kuhurumia watu na kutoa misamaha (prerogative of
mercy or clemency). Kwa maneno mengine, Kama anavyosema
Hood Phillips, mamlaka ya namna hii ni “mabaki ya madaraka ya
kifalme.”2 Yalikuwa ni madaraka ya kipekee (privilege) aliyopewa
Mfalme ambaye siyo tu alikuwa ni mtawala bali pia nchi (the realm)

1 Harold J. Krent, “Conditioning the President's Conditional Pardon Power”, in


California Law Review, Vol. 89, No. 6 (Dec., 2001), pp. 1665-1720, p.1671.
2 Kama alivyonukuliwa na M.Travis, “The Prerogative of Mercy in New Zealand”,

on
http://homepages.ihug.co.nz/~ttpbst/me/writing/mercy.htm
16
ilichukuliwa kuwa ni yake. Kama anavyoeleza David Tait, kwa
kawaida Mfalme alitoa msamaha siku ya sherehe ya kutawazwa
kwake (coronation) au wakati wa sikukuu zingine za umma.1
Utamaduni huu umeigwa na kufuatwa katika nchi nyingi ikiwemo
Tanzania ambapo Rais hutoa msamaha wakati wa sikukuu ya
Muungano (Aprili 26) na uhuru (Desemba 9).

Kwa kawaida ya utamaduni wa Kiingereza, madaraka haya huwa


hayadhibitiwi. Kama anavyoeleza Mwanafalsafa wa Kiingereza,
John Locke, ni madaraka ya kufanya mazuri bila kuongozwa na
sheria (“For Prerogative is nothing but the Power of doing publick2
good without a Rule”).3 Kama ilivyokwisha kuelezwa hapo juu,
sababu ya Mfalme au Malkia kutofungwa na sheria ilitokana na
utamaduni uliokuwa unamwona Mfalme kuwa ndiye anamiliki nchi
au dola (the realm), Serikali ilikuwa ni yake, Mahakama na Majaji
ni wake, magereza na vyombo vingine pia vilikuwa ni vyake. Mfalme
alikuwa na madaraka makubwa sana ambayo hayakudhibitiwa.4

2.1.4 Sababu za mamlaka ya kutoa msamaha wa huruma


Kuna sababu nyingi ambazo zinatambuliwa katika kuhalalisha
uwepo wa madaraka ya kutoa msamaha. Mojawapo ya sababu hizo
ni kama ifuatavyo;

 Sababu za kiubinadamu zinahitaji kuwe na mamlaka ya


kusamehe kwa sababu sheria za kijinai zinaweza kuwa za
kikatili5;

 Bunge linapotunga sheria linaweza kushindwa kuzingatia


mazingira maalum ambayo yanaweza kumfanya mtu kufanya
kosa kwa namna ambayo inahitaji huruma6;

1David Tait, “Pardons in perspective: The role of forgiveness in criminal justice”,


on http://www.canberra.edu.au/ncf/events/pardonsperspective.pdf.
2 Neno hili “Publick” ni neno “public”. Inaelekea karne ya 16 lilikuwa likiandikwa

hivyo.
3 John Locke, Two Treatises of Civil Government, 425 kama iliyonukuliwa katika

John Harrison, “Pardon as Prerogative”, in Federal Sentencing Reporter, Vol. 13,


No. 3-4, Pardon Power and Sentencing Policy(November/December 2000 -
January/February 2001), pp. 147-149, pp. 47 & 149.
4 Alex Carroll, (2009), Constitutional and Administrative Law, Pearson Education

Limited, Harlow, p.247.


5 Harold J. Krent, “Conditioning the President's Conditional Pardon Power”, in

California Law Review, Vol. 89, No. 6 (Dec., 2001), pp. 1665-1720, p.1673-4.
6 James Iredell alinukuliwa akisema: "[T]here may be many instances where,

though a man offends against the letter of the law, yet peculiar circumstances in
17
 Rais anaweza kutumia madaraka ya msamaha kumwondolea
adhabu mtu au watu fulani ambao kufungwa kwao au
adhabu yao ni chanzo cha maandamano, machafuko au uasi
ili kurudisha amani na utulivu au kuleta mwafaka kati ya
Serikali na kundi fulani1;

 Rais aweza kutumia mamlaka ya msamaha wa adhabu ili


kudhibiti madaraka ya kiMahakama na Bunge.2

 Kwa kupitia madaraka ya msamaha wa adahabu, Rais aweza


kusahihisha makosa yaliyofanywa katika mfumo wa utendaji
haki (criminal justice system) hasa pale inapotokea mtu asiye
na hatia anatiwa hatiani kimakosa3;

 Rais anaweza kuwasamehe watu ambao inaonekana


wamejutia makosa yao, wanaojituma na kuonyesha tabia
nzuri wakiwa gerezani4;

 Kwa sababu za kibinadamu Rais aweza kuwasamehe watu


fulani kutokana na umri wao, afya mbaya au vigezo vingine
vinavyofaa5;

 Katika Tanzania misamaha mingi imetolewa kwa lengo la


kupunguza msongamano wa wafungwa na mahabusu
magerezani.

2.1.5 Historia fupi ya madaraka ya kutoa msamaha


Wakati wa ukoloni mamlaka ya kutoa misamaha Tanganyika
yalikuwa chini ya Gavana na Zanzibar yalikuwa chini ya Sultanii.
Hali ilindelea hivyo mara baada ya uhuru. Kifungu cha 55 cha
Katiba ya Uhuru wa Tanganyika [The Tanganyika (Constitution)
Order in Council 1961] kilimpa Gavana madaraka ya kutoa

his case may entitle him to mercy. It is impossible for any general law to foresee
and provide for all possible cases that may arise .... ." [Harold J. Krent,
“Conditioning the President's Conditional Pardon Power”, in California Law
Review, Vol. 89, No. 6 (Dec., 2001), pp. 1665-1720, p.1674].
1 Harold J. Krent, “Conditioning the President's Conditional Pardon Power”, in

California Law Review, Vol. 89, No. 6 (Dec., 2001), pp. 1665-1720, p.1674.
2 Kama ilivyo juu, p.1674.
3 Kama ilivyo juu, p. 147.
4 Kama ilivyo juu.
5 Kama ilivyo juu.

18
misamaha. Tofauti na Katiba ya sasa ambayo haijaweka mipaka
yoyote, Katiba ya Uhuru ilimtaka Gavana ashauriwe na Waziri
mahsusi kabla ya kutekeleza mamlaka ya kutoa msamaha.1
Vilevile, kabla ya kufanya uamuzi kuhusiana na kesi za kijeshi
Gavana alitakiwa ashauriane na Waziri mwingine.2 Hali kadhalika
Katiba hiyo ilianzisha Kamati ya Ushauri (Advisory Committee)
ambayo pia iliwajibika kumshauri Gavana kuhusiana na misamaha
ya huruma.3

Katiba ya Jamhuri ya Mwaka 1962 (The Republican Constitution,


1962), iliyahamisha mamlaka ya kutoa msamaha kutoka kwa
Gavana kwenda kwa Rais.4 Mabadiliko mengine yaliyofanywa na
Katiba ya Jamhuri ni kuondoa vipengele vyote ambavyo vilimtaka
Gavana ashauriwe na Waziri pamoja na Kamati ya Ushauri.
Madaraka yote yaliachwa kwa Rais mwenyewe. Hata hivyo, Katiba
hiyo, kama ilivyo Katiba ya sasa, ililipa Bunge mamlaka ya kutunga
sheria itakayosimamia utekelezaji wa mamlaka ya kutoa misamaha
ya adhabu5 lakini Bunge halikutunga sheria mahsusi inayoelekeza
namna madaraka ya kutoa misamaha yatakavyotekelezwa. Hata
hivyo, Sheria ya Masuala ya Urais (The Presidential Affairs Act6)
iliyotungwa mwaka 1962 ina kifungu kimoja kinachoanzisha
Kamati ya Ushauri kuhusu misamaha ambayo inamjumuisha
Waziri atakayeteuliwa na Rais, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na
wajumbe wasiopungua watatu ambao wote watateuliwa na Rais.

Katiba ya muda ya Mwaka 1965 (The Interim Constitution of


Tanzania, 1965)7 haikujumuisha masharti yoyote ya kudhibiti
madaraka ya kutoa misamaha isipokuwa tu madaraka hayo
yalipanuliwa kumwezesha Rais kutoa misamaha ya adhabu kwa
upande wa Zanzibar kuhusiana na masuala ya muungano.8
Utaratibu huu uliendelea katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania ya Mwaka 1977 kama ilivyoelezwa hapo juu.

Kwa upande wa Zanzibar, Katiba ya Nchi ya Zanzibar ya Mwaka


1963 (The Constitution of the State of Zanzibar, 1963) ilimpa Sultani

1 Kifungu cha 55(2) cha Katiba ya Uhuru ya 1961.


2 Kama ilivyo juu, Kifungu cha 55(3).
3 Kama ilivyo juu, Kifungu cha 56.
4 Ibara ya 19 ya Katiba ya Jamhuri, 1962.
5Kama ilivyo juu, Ibara ya 19 (2).
6 Cap 9 [RE 2002].
7 Ibara ya 22 (1) na (2) ya Katiba ya Muda ya Mwaka 1965.
8 Kama ilivyo juu, Ibara ya 22 (3).

19
mamlaka ya kusamehe adhabu kwa huruma (prerogative of mercy).
Tofauti na Katiba ya Uhuru ya Tanganyika, Katiba ya Nchi ya
Zanzibar ya Mwaka 1963 haikumtaka Sultani ashauriane na mtu
wala chombo chochote kile. Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1979
ilimpa Rais wa Zanzibar mamlaka mapana kutoa misamaha ya
adhabu.1 Rais alipewa mamlaka ya kutoa misamaha kwa masharti
au bila masharti kwa “mtu yeyote” aliyetiwa hatiani na “Mahakama
yoyote” kuhusiana na “kosa lolote.”2 Kama ilivyokuwa Katiba ya
Nchi ya Zanzibar ya Mwaka 1963, Katiba ya Zanzibar ya Mwaka
1979 haikumtaka Rais ashauriwe na mtu au chombo chochote.
Uamuzi uliachwa kwake yeye mwenyewe.

Katiba ya sasa ya Zanzibar (Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1984)


inampa Rais wa Zanzibar madaraka mapana ya kutoa misamaha
kama ilivyo Katiba ya Jamhuri ya Muungano.3 Lakini tofauti na
Katiba ya Muungano, Katiba ya Zanzibar imeunda “Kamati ya
Ushauri kwa Rais” ambayo inaundwa na Mwanasheria Mkuu wa
Serikali na wajumbe watano watakaoteuliwa na Rais.4 Katiba ya
sasa ya Zanzibar inajaribu kuyadhibiti mamlaka aliyopewa Rais ila,
kama ambayo tumegusia hapo kabla, tatizo ni kuwa wajumbe wote
wa Kamati ya Ushauri wanateuliwa na Rais mwenyewe. Kwa hiyo
kuna walakini katika suala la uhuru wa wajumbe. Aidha, Rais
halazimiki kufuata ushauri wa wajumbe.

2.1.6 Utaratibu wa sasa na matatizo yake


Kwa utaratibu uliopo, kwanza Rais hupeleka barua inayoainisha
vigezo vya kutoa msamaha / kupewa msamaha kwa Waziri wa
Mambo ya Ndani. Waziri huipeleka barua hiyo kwa Wakuu wa
Magereza mbalimbali. Baada ya kupata barua inayoainisha vigezo
hivyo, Wakuu wa Magereza mabalimbali hupendekeza wafungwa
wanaofaa kupewa misamaha ya aina mbalimbali. Majina hayo
hupelekwa kwa Waziri wa Mambo ya Ndani na hatimaye kwa Rais.
Sheria ya Masuala ya Kirais (the Presidential Affairs Act5,)
imeanzisha “Kamati ya Kumshauri Rais kuhusu Misamaha ya
Huruma.”6 Kamati hii huundwa na Waziri atakayeteuliwa na Rais,
Mwanasheria Mkuu, na wajumbe wengine wasiopungua watatu

1 Ibara ya 20 ya Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1979.


2 Kama ilivyo juu, Ibara ya 20 (1).
3 Ibara ya 59 ya Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1984.
4 Kama ilivyo juu, Ibara ya 60.
5 Cap 9 [RE 2002].
6 Kifungu cha 3 cha Sheria ya Masuala ya Kirais, Sura ya 9.
20
wala wasiozidi wanne ambao watateuliwa na Rais.1 Rais ndiye
huongoza mikutano ya Kamati hii.2 Kwa mujibu wa Sheria ya
Masuala ya Urais, Rais “anaweza” kutaka ushauri wa Kamati
kuhusiana na utekelezaji wa mamlaka yake ya kutoa misamaha
kwa mujibu wa ibara 45 ya Katiba.3 Hii ina maana kuwa Rais
halazimiki kutafuta ushauri wa Kamati kuhusiana na masuala
mengi yahusuyo madaraka yake ya kutoa misamaha; ni hiari yake.
Isipokuwa kuna suala moja tu ambalo sheria inamlazimisha
kutafuta ushauri wa Kamati, Rais analazimika kuwasilisha taarifa
kuhusu mtu aliyehukumiwa kunyongwa kwenye kikao cha Kamati
ili aweze kushauriwa ingawa hawajibiki kufuata ushauri wa
Kamati.4

Kwa kawaida Rais husamehe idadi kubwa ya wanaotumikia


adhabu katika sikukuu ya Muungano (26 Aprili) na Uhuru (9
Disemba). Majina ya watu wanaopata msamaha hutangazwa
kwenye Gazeti la Serikali ingawa kwa hali halisi wananchi wa
kawaida huwa hawawezi kuyaona majina hayo kwa sababu Gazeti
la Serikali huwa halisomwi na watu wengi nje ya Serikali.
Kinachotokea ni kwamba wananchi wa kawaida huambiwa idadi tu
ya watu ambao wamesamehewa na Rais.

Ingawa hakuna utaratibu uliowekwa kisheria, kumekuwa na


kawaida ya watu wanaotumikia adhabu (hasa hasa adhabu ya
kifungo na wale wanaosubiria adhabu ya kifo kutekelezwa dhidi
yao) wao wenyewe au kupitia ndugu zao, mawakili, na watu
wengine, kumwandikia Rais ili kumwomba awape msamaha. Ni
vigumu kujua ni kwa namna gani maombi kama hayo
hushughulikiwa kwa sababu hakuna habari.

Kwa kifupi utaratibu uliopo sasa una matatizo yafuatayo;

1 Kama ilivyo juu, Kifungu cha 3(1).


2 Kama ilivyo juu, Kifungu cha 3 (2).
3 Kama ilivyo juu, Kifungu cha 3 (4).
4 Kifungu cha 3 (3) cha Sheria ya Masuala ya Urais, Sura ya 9; Ibara ya 37 (1) ya

Katiba inaeleza kuwa “Mbali na kuzingatia masharti yaliyomo katika Katiba hii
na katika sheria za Jamhuri ya Muungano katika utendaji wa kazi na shughuli
zake, Rais atakuwa huru na hatalazimika kufuata ushauri atakaopewa na mtu
yeyote, isipokuwa tu pale anapotakiwa na Katiba hii au na sheria nyingine yoyote
kufanya jambo lolote kulingana na ushauri anaopewa na mtu au mamlaka
yoyote.”
21
 Katiba imetoa madaraka mapana sana kwa Rais yanayofanya
udhibiti wa madaraka hayo usiwezekane. Rais amepewa
madaraka ya kusamehe, kubadilisha, au kupunguza “adhabu
yoyote” aliyopewa “mtu yeyote” kuhusiana na “kosa lolote.”
Katiba haielekezi Rais atoe sababu yoyote kuhusu maamuzi
yake. Madaraka haya hayaendani kabisa na utamaduni wa
utawala wa sheria au falsafa ya sasa inayotaka kuwe na
“utawala wa kikatiba” (constitutionalism) ambao hakuna mtu
anayepewa madaraka yasiyo na mipaka.

 Hakuna utaratibu wa kudhibiti utekelezaji wa madaraka ya


kutoa msamaha. Kamati ya Ushauri imeundwa na watu
ambao wote wameteuliwa na Rais mwenyewe. Wajumbe wa
Kamati siyo watu huru ambao wanaweza kumzuia Rais kutoa
msamaha pale wanapoona haifai kutoa msamaha. Aidha,
Rais halazimiki kuitisha kikao cha Kamati ya Ushauri na
hata akiitisha halazimiki kufuata ushauri wa wajumbe wa
Kamati.

 Hakuna utaratibu wa kujua huko magerezani kama


wanaoorodheshwa kupata msamaha ni kweli wanastahili,
wala watu wanaostahili hawaachwi kuorodheshwa.
Utaratibu huu ni “rutuba” ya kumea kwa rushwa.

 Hakuna uwazi mkubwa kwa namna ambayo madaraka ya


kutoa msamaha hutekelezwa. Hii inafanya iwe vigumu kwa
vyombo vya habari na wananchi kujua ni akina nani hasa
wamepewa msamaha.

2.2 UZOEFU WA NCHI NYINGINE


2.2.1 Marekani
Katiba ya Marekani imempa Rais wa nchi hiyo madaraka ya kutoa
msamaha.1 Kama ilivyo kwa Tanzania na nchi zingine katika
Jumuiya ya Madola, madaraka haya ya Katiba ya Marekani

1 Ibara ya 11, kifungu cha 2 cha Katiba ya Marekani inaeleza, “The President
shall be commander in chief of the Army and Navy of the United States, and of
the militia of the several states, when called into the actual service of the United
States; he may require the opinion, in writing, of the principal officer in each of
the executive departments, upon any subject relating to the duties of their
respective offices, and he shall have power to grant reprieves and pardons for
offenses against the United States, except in cases of impeachment.”
22
yalifuata mtindo wa Mfalme wa Uingereza kutoa misamaha na kwa
hiyo Rais wa Marekani hajawekewa mipaka katika kutekeleza
mamlaka hayo.1 Ili kujua ni kwanini Katiba ya Marekani iliweka
utaratibu wa namna hii ni vizuri kudodosa kidogo kilichotokea
ndani ya mkutano wa kikatiba (constitutional convention) wa Mwaka
1787. Inaelezwa kuwa kulikuwa na ubishani mkali miongoni mwa
wajumbe kuhusiana na suala hili.2 Kuna wajumbe hawakutaka
Rais apewe madaraka hayo ya “kifalme.” Kuna wengine walitaka
Rais apewe mamlaka lakini yadhibitiwe. Lakini Alexander Hamilton,
mjumbe aliyetaka mfumo wa Urais wenye nguvu (strong presidency)
kama Mfalme, na anayeelezewa kuwa alikuwa mzungumzaji mahiri,
alisimama na kunena;

“Humanity and good policy conspire to dictate, that


the benign prerogative of pardoning should be as little
as possible fettered or embarrassed…one man
appears to be a more eligible dispenser of mercy of the
government than a body of men”.3

Maneno haya yanaweza kutafsiriwa kama ifuatavyo: “Sababu za


ubinadamu na sera nzuri zikijumuishwa pamoja zinaelekeza kuwa
mamlaka ya kipekee na yenye nia njema ya kutoa misamaha
yasidhibitiwe kama itakavyowezekana. Mtu mmoja anafaa zaidi
kutoa huruma ya Kiserikali kuliko kikundi cha watu.” Hamilton
alikuwa akipinga hoja ya wajumbe wengine waliotaka madaraka
hayo yadhibitiwe na kwamba Katiba imlazimishe Rais
kuwashirikisha watu wengine katika maamuzi. Hamilton alikuwa
akiaminika sana, maneno yake yalizika kabisa uwezekano wa
kudhibitiwa kwa mamlaka ya Rais kutoa misamaha. Yeye alitaka
Rais mwenye mamlaka mengi na mapana kama Mfalme wa

1 Harold J. Krent, “Conditioning the President's Conditional Pardon Power”, in


California Law Review, Vol. 89, No. 6 (Dec., 2001), pp. 1665-1720, p.1671.
2 Angalia John Dinan, “The Pardon Power and the American State Constitutional

Tradition”, in Polity, Vol. 35, No. 3 (Apr., 2003), pp. 389-418, p. 404. Vile vile
angalia David Tait, “Pardons in perspective: The role of forgiveness in criminal
justice”, p.5, on http://www.canberra.edu.au/ncf/events/pardonsperspective.pdf
3 John Dinan, “The Pardon Power and the American State Constitutional
Tradition”, in Polity, Vol. 35, No. 3 (Apr., 2003), pp. 389-418, p. 404. Vile vile
angalia David Tait, “Pardons in perspective: The role of forgiveness in criminal
justice”, p.5, on
http://www.canberra.edu.au/ncf/events/pardonsperspective.pdf.
23
Uingereza. Kwa sababu hiyo Katiba ya Marekani inatoa madaraka
mapana ya kutoa msamaha yasiyodhibitiwa.1

Hivyo, madaraka hayo yamekuwa yakitumiwa na ma-Rais wengi wa


nchi hiyo kama wao wenyewe wanavyoona inafaa. Inaelezwa kuwa
Rais Abraham Lincoln alitumia sana madaraka kama hayo. Katika
kisa kimoja mwanajeshi mmoja (Barney) alitiwa hatiani kwa
makosa ya kijeshi na alitakiwa kupigwa risasi. Rais alibadili
mawazo dakika za mwisho. Akampa mtu mmoja aliyetakiwa
kukimbia kwa farasi na kuupeleka ujumbe uliondikwa kwenye
kijikaratasi kidogo kwenye sehemu ambayo adhabu ilipangwa
kutekelezwa. Alikuwa ameandika hivi: “Kanali Mulligan — kama
bado hujampiga Barney D. risasi, usimpige. A. Lincoln.”2 Suala
linalokuja hapa ni kuwa Rais alitumia vigezo gani kuibatilisha
adhabu hiyo dakika za mwisho? Jibu haliwezi kupatikana kwa
sababu Katiba yao haimlazimishi Rais kutoa sababu. Madaraka
yatatekelezwa kufuatana na busara na hisia za Rais mwenyewe.
Kwa sababu hizo hizo kuna matukio ambayo madaraka hayo ya
Rais yametumiwa vibaya. Harold J. Krent anaeleza kuwa Rais Bill
Clinton alizua utata na mjadala mkali alipoamua, katika dakika za
mwisho za awamu ya pili ya Urais wake, kutoa msamaha kwa kaka
yake, mtoto wa Waziri wake, Katibu wake wa zamani, rafiki yake wa
kisiasa, na mtu ambaye alitiwa hatiani kwa kukwepa kodi kwa
kiasi kikubwa cha fedha kuliko mtu mwingine katika historia ya
nchi hiyo.3

Udhibiti mkubwa wa madaraka ya kutoa msamaha katika nchi hiyo


ni uwazi (transparency) katika utendaji wa Serikali na uhuru wa
vyombo vya habari. Vyombo vya habari hujulishwa kuhusu

1 Katiba nyingi za majimbo ya Marekani zilikataa kufuata falsafa ya Hamilton


iliyoingizwa katika Katiba ya Shirikisho la Marekani. Katiba hizo zimedhibiti
mamlaka ya kutoa misamaha ya ma-Gavana wa Majimbo mbalimbali. [Angalia
John Dinan, “The Pardon Power and the American State Constitutional
Tradition”, in Polity, Vol. 35, No. 3 (Apr., 2003), pp. 389-418, p. 405].
2Kwa maneno yake Rais Lincoln aliandika hivi kwenye kijikaratasi: “Colonel

Mulligan – if you haven’t shot Barney D. – yet – don’t. A. Lincoln’ [angalia David
Tait, “Pardons in perspective: The role of forgiveness in criminal justice”, p.5, on
http://www.canberra.edu.au/ncf/events/pardonsperspective.pdf.]
3 Harold J. Krent, “Conditioning the President's Conditional Pardon Power”, in

California Law Review, Vol. 89, No. 6 (Dec., 2001), pp. 1665-1720, pp.1666-
1667. Angalia pia, Charles Shanor & Marc Miller “Pardon Us: Systematic
Presidential Pardons”, Federal Sentencing Reporter, Vol. 13, No. 3-4, Pardon
Power and Sentencing Policy(November/December 2000 - January/February
2001), pp. 139-146, p.140.
24
maamuzi ya Rais na kuwapa wananchi fursa ya kujadili busara ya
maamuzi ya Rais. Kama maamuzi ni mabaya basi Rais
atawajibishwa kisiasa uchaguzi ukifika. Katika nchi yetu hali ni
tofauti kwa sababu mambo mengi hufanyika bila wananchi
kufahamu kinachoendelea. Hali hii inatoa mwanya wa kuyatumia
madaraka hayo vibaya.

2.2.2 Kenya
Katiba mpya ya Kenya ya Mwaka 2010 imebakisha madaraka ya
Rais ya kutoa misamaha lakini imefanya mabadiliko makubwa
kuhusiana na madaraka ya aina hiyo.1 Kwanza, Katiba imeruhusu
mtu yeyote kuomba apewe msamaha. Pili, Katiba imeunda Kamati
ya Ushauri kuhusiana na misamaha.2 Tatu, Kamati ya Ushauri
inajumuisha watu wasio watumishi wa Serikali ambao watakuwa
huru na kwamba wajumbe wasio watumishi wa Serikali ni wengi
zaidi kuliko wale wa Serikali.3 Nne, Rais atalazimika kuamua
kufuatana na ushauri ailiopewa na Kamati ya Ushauri.4 Tano,
Katiba imeondokana na lugha ya kuyaita madaraka ya namna hii
kama “prerogative of mercy”, lugha ambayo kwa asili yake
inamaanisha “madaraka ya kipekee au maalum ya kifalme.” Badala
yake, madaraka haya yameitwa “power of mercy” (madaraka ya
kutoa msamaha wa huruma). Madaraka ya kifalme yatumikavyo
atakavyo Mfalme mwenyewe hayana nafasi katika nchi ya
kidemokrasia na inayofuata utawala wa sheria.

2.2.3 Afrika ya Kusini


Katiba ya Jamhuri ya Afrika ya Kusini ya Mwaka 1996 imempa
Rais wa nchi hiyo mamlaka ya kusamehe na kupunguza adhabu.5
Lakini kwa mujibu wa kifungu cha 1 cha Nyongeza B ya Katiba
hiyo ni sharti Rais ashauriane na Manaibu Rais watendaji kwanza
kabla ya kutoa msamaha. Hii yote ni kuhakikisha kuwa uamuzi
haufanywi na mtu mmoja ambaye anaweza kukosea au kutumia
madaraka vibaya.

2.3 TATHMINI NA MAPENDEKEZO


Tathmini

1 Ibara ya 133 ya Katiba ya Kenya ya Mwaka 2010.


2 Kama ilivyo juu, Ibara ya 133 (2).
3 Kama ilivyo juu, Ibara ya 133 (2) (c).
4 Kama ilivyo juu, Ibara ya 133 (1).
5 Ibara ya 84(2) (j) ya Katiba ya Jamhuri ya Afrika ya Kusini, 1996.
25
Ingawa kuna wananchi wanaotaka madaraka ya kutoa misamaha
ya adhabu yaondolewe kabisa, madaraka haya bado ni muhimu na
inafaa yaendelee kuwepo kwenye Katiba mpya. Madaraka ya
msamaha yanaweza kutumika kuokoa maisha hasa pale
inapotokea hali ya afya ya mtu anayetumikia adhabu ni mbaya.

Pia, amani na utengamano ni vitu muhimu katika Taifa lolote lile.


Madaraka haya yanaweza kutumika kuleta amani na maridhiano.
Mathalan, mtu mmoja au kikundi cha watu wanaweza kufungwa.
Wafuasi wao wanaweza kusababisha maandamano, ghasia na
machafuko. Ili kurudisha amani na utengamano kiongozi wa nchi
anaweza kutumia mamlaka ya msamaha kuwaachia. Hali
kadhalika, nchi inaweza kukumbwa na uasi wa ndani au balaa la
vita vya wenyewe kwa wenyewe. Katika kutafuta maridhiano waasi
wanaweza kutoa sharti la kuachiwa kwa mwenzao au wenzao walio
gerezani kwanza ndipo wasimamishe vita au kusaini mkataba wa
amani. Katika mazingira hayo kiongozi wa nchi anaweza kulazimika
kutumia mamlaka ya kutoa msamaha ili kurejesha amani na
utengamano.

Vile vile, madaraka hayo ni muhimu kurekebisha makosa


yaliyotokea katika mfumo wa utendaji haki. Mathalan, mtu mmoja
anaweza kukamatwa na kushtakiwa kwa mauaji ya mtu ambaye
amepotea. Ushahidi unaweza kuletwa Mahakamani kuonyesha
kuwa mtu aliyepotea ameuawa ingawa mwili wake haujapatikana.
Anayeshtakiwa anaweza kutiwa hatiani; pia aweza kukata rufaa na
rufaa hiyo kukataliwa pia. Vinginevyo anaweza kuwa mtu asiye na
uwezo wa kupata msaada wa kisheria. Inaweza kutokea wakati
anasubiri kunyongwa yule mtu aliyedaiwa kuuawa akatokea na
kudai kuwa alisafiri. Katika mazingira haya Rais atatoa msamaha
kumuokoa aliyetiwa hatiani. Pia, polisi wanaweza kukosea
kumkamata mtu ambaye hajaua, kumshtaki na hatimaye mtu
huyo kutiwa hatiani kwa mauaji ya mtu mmoja (tumuite “Funke”).
Wakati anasubiri adhabu ya kifo, muuaji halisi (akiwa amelewa)
anaweza kutamba, kwa mfano, kwa kusema: “bwana, mimi mtu
asinichezee kabisa. Mtu akitembea na mke wangu nitammaliza!
Funke nilimkomesha!” Habari kama hii ni sababu nzuri kwa Rais
kumwachilia huru kwa haraka mtu aliyetiwa hatiani kimakosa na
anayesubiri adhabu ya kifo. Kuna uwezekano pia kurudi
Mahakamani kuomba marejeo (review) lakini mara nyingi mtu
kama huyo hana uwezo wa kuajiri wakili; hatakuwa na uwezo wa

26
kutoka gerezani na kumtafuta shahidi aliyesikia ushahidi mpya au
kuwaomba Polisi wamtafute na hata wakiombwa inawezekana
wasitoe ushirikiano; kwa sababu miaka mingi itakuwa imeshapita
ndugu zake wanaweza kuwa wamemsahau au wameamini kuwa
atakuwa amekwisha kunyongwa. Kikwazo kingine ni kuwa watu
wanaosubiri adhabu ya kifo hawapewi fursa ya kuwasiliana na
ndugu zao. Hivyo, hatoweza hata kujua kuwa muuaji halisi
amejulikana. Katika mazingira ya namna hii, jirani mmoja mwenye
imani na ujasiri, na anayeelewa utaratibu, anaweza kwenda
kumwona au kumwandikia Rais na hatimaye kumuokoa. Utaratibu
huu ni rahisi kuliko ule wa Mahakamani ambao ni mrefu na wenye
gharama nyingi.

Aidha, madaraka ya kutoa msamaha yanaweza kutumiwa na


kiongozi wa nchi katika kudumisha uhusiano wa kidiplomasia kati
ya Tanzania na nchi nyingine. Kwa mfano, raia wa nchi nyingine
anaweza kutiwa hatiani na kufungwa katika magereza yetu.
Serikali ya nchi yake inaweza kutaka aachiwe. Kama Rais hana
mamlaka ya kumuachia hali hiyo inaweza kuharibu kabisa
mahusiano ya kidiplomasia na pengine hata kuzusha vita.
Haitokuwa busara kwa nchi kuingia vitani, kuharibu uchumi,
miundombinu, mali na kupoteza maisha ya watu wengi kwa
sababu ya kung’ang’ania kumshikilia mtu mmoja.

Zaidi ya hayo, madaraka ya kusamehe adhabu yanatoa fursa kwa


kiongozi wa nchi kuwasamehe watu waliotenda makosa katika
mazingira fulani ambayo huwafanya wahurumiwe na kuonekana
wanastahili kuhurumiwa. Kesi ya Jamhuri dhidi ya Juma
Kulambalimbali [1974] LRT n. 41 iliyotokea huko Chunya, Mkoa wa
Mbeya, inaweza kuwa mfano mzuri. Kesi hii ambayo ilikuwa ni
“kesi ya mwana kumuua baba yake” (patricide) inaweza pia
kuelezewa kama ni “kesi ya mwana kumuasi au kumkaidi baba
yake.” Maelezo yake kwa ufupi ni kuwa Mzee Kulambalimbali
Mhogomchungu aliamua kumfunza mwanae (Juma
Kulambalimbali) “ufundi” (yaani “uchawi”). Darasa, au sehemu ya
mafunzo, haikuwa sehemu ya kawaida bali vichakani. Na utaratibu
wa kutoa mafunzo haukuwa wa kawaida bali kabla ya mafunzo
kuanza mwanafunzi alitakiwa kutoa nguo zote na kubaki uchi wa
mnyama. Juma hakufuata maelekezo ya mwalimu, bali aliamua
kukimbia na kutoweka.

27
Kwa utamaduni wa kiafrika kumkaidi mzee siyo jambo la kawaida;
ni balaa kubwa. Hivyo, Juma aliamua kutoroka nyumbani na
kukimbilia kwa ndugu walio kijiji kingine. Huko nako mambo
hayakumwendea sawia, majoka yalimtokea na katika tukio moja
joka lilijiviringisha kwenye mguu wake. Alipoenda kwa “fundi”
(yaani “mganga”) aliambiwa baba yake ndiye alikuwa akimletea hizo
balaa zote. Baada ya hapo alikata shauri kurudi nyumbani ili
akamwombe baba yake msamaha. Alipofika tu baba yake
alimwambia, “huwezi kunikimbia wewe!” Alinena asamehewe lakini
msamaha haukupatikana. Baba yake alikuwa na hasira sana.
Mahusiano yao yaliharibika. Siku moja, watu hawa wawili
waligombana. Mara tu baada ya ugomvi ule tumbo la Juma
liliumuka/kuvimba na kuwa kubwa kwa ghafla. Mama yake
alikimbilia kwa mjumbe wa nyumba-kumi (balozi) na kumuomba
akamsihi Mzee Mhogomchungu amponye mwanae. Baada ya balozi
kuingilia kati, uvimbe wa tumbo ulitoweka.

Baada ya kisa hicho, Juma alianza kuona kuwa maisha yake yapo
hatarini. Aliwaza kuwa alikimbia nyumbani ili apate usalama lakini
haukupatikana; alirudi nyumbani kuomba msamaha lakini
msamaha nao haukupatikana. Hivyo, siku moja alichukua shoka,
akamvizia baba yake aliyekuwa amelala, na kumkatakata kichwani
hadi kufa. Alikamatwa na kushtakiwa kwa kosa la mauaji. Sheria
haitambui utetezi wa mtu kuua ili kujikinga na uchawi. Msimamo
wa sheria na Serikali ni kuwa uchawi haupo.1 Kutokana na
mazingira haya, Jaji (Kwikima, Ag J) aliyesikiliza kesi hii aliingiwa
na huruma sana lakini hata hivyo alisema hakuwa na namna ya
kumsaidia kwa sababu ilibidi afuate sheria. Alimtia hatiani kwa
kosa la mauaji na kumtangazia adhabu yake kuwa atanyongwa
hadi afe. Mwishowe, katika hukumu yake, Jaji alimwombea Juma
ili Mungu amsaidie katika safari yake ili Mtukufu Rais aweze
kumsaidia. Aidha, alipendekeza mabadiliko ya sheria.2

1 Katika shauri la Rex v Palamba s/o Fundikila, 14 EACA 96 Mahakama ya


Rufaa ya Afrika Mashariki ilieleza kuwa haiamini kuwa kuna uchawi (“This Court
cannot possibly proceed on any other basis than Wamlunda [one of the two
deceased women] was innocent of witchcraft, which so far as this court is
concerned does not exist”).
2 Kwa maneno yake Jaji alisema, “Our people, whether we like it or not, have

believed, believe and will continue to believe in witchcraft even if literacy were to
become universal tomorrow morning. Science and technology have yet to explain
the natural puzzles and phenomena which are peculiar to Africa. And judging
from very low and slow pace of our technological advancement, these beliefs shall
remain with us for quite sometime.” He then decided to grab the bull by its horns
28
Kesi hii ni kielelezo kuwa madaraka ya msamaha ni muhimu. Mtu
anaweza kuchukuliwa hatua za kisheria lakini jamii
inayomzunguka haitaki achukuliwe hatua. Kwa kiasi fulani,
utekelezaji wa sheria inabidi uzingatie maoni ya jamii vinginevyo
sheria haitoheshimika na vyombo vya utekelezaji wa sheria
havitaungwa mkono.

Shauri jingine ambalo Mahakama ilionekana kumhurumia


mtuhumiwa ni Jamhuri dhidi ya Agnes Doris Liundi [1980] TLR 38
(Rufaa yake imeripotiwa kama Agnes Doris Liundi dhidi ya Jamhuri
[1980] TLR 46). Kwa kifupi, mtuhumiwa katika shauri hili (Agnes
Doris Liundi) alimaliza elimu ya kidato cha nne mwaka 1966 na
kuolewa mwaka 1967. Katika miaka miwili ya mwanzo maisha ya
ndoa yalikuwa ni yenye furaha sana. Mambo yalianza kuharibika
alipoenda kusoma Chuo cha Ualimu Morogoro mwaka 1969. Alirudi
wakati mmoja Dar es Salaam na ndipo alipomwambukiza mumewe
ugonjwa wa kisonono. Alipoulizwa alieleza kuwa alibakwa na mtu
mmoja huko Morogoro lakini yeye hakutaka kumwambia mtu
yeyote kwa sababu alifikiri asingeweza kuaminiwa. Mume wake
alikataa kuiamini hadithi hii. Kuanzia hapo amani na furaha
vikatoweka; ndoa ilitawaliwa na migogoro na magomvi mengi kwa
miaka mingi.

Siku moja (tarehe 21 Februari 1978) mume wake alimwambia


mtuhumiwa kuwa yeye alikuwa anaenda kazini lakini akirudi
akute mtuhumiwa ameondoka la sivyo atamtoa nje akiwa uchi.
Alivyoambiwa hivyo alilia na kuhofu kuwa matatizo ya upweke
kutokana na uyatima aliyoyapata katika udogo wake yatawakumba
pia na watoto wake. Aliamua kuchukua uamuzi mgumu— alienda
kutafuta sumu na baadaye kununua maji ya matunda (Orange
squash); akawaita watoto wote wanne chumbani; akawaambia
kuwa walikuwa na safari; akambusu na kumuaga kila mtoto.
Hatimaye aliwapa orange squash iliyochanganywa na sumu na
kuwaambia wanywe, naye alikunywa. Mara tu baada ya kunywa,
watoto walianza kulia, kuharisha na kutapika. Msichana mmoja
alikimbia kuwaita majirani na hatimaye Polisi walifika na
kuwakimbiza hospitali (Muhimbili). Hata hivyo, watoto watatu
walikufa; mtuhumiwa na mtoto mkubwa walibahatika kuokolewa.

in the following words: “Should we not therefore face this fact and adjust the law
accordingly? It is time to re-examine the law on this point.”

29
Katika upelelezi wao Polisi walipekua nyumba yao na kukuta barua
nne ambazo ziliandikwa na mtuhumiwa kabla ya kunywa sumu.
Katika barua mojawapo alindika hivi: “KWA YEYOTE
ANAYEHUSIKA: Uamuzi niliochukua ni wa kudumu, mume wangu
George asisumbuliwe au kuteswa au kukabiliwa kwa namna yoyote
ile kwa sababu nilimpenda. Nimewachukua watoto kwa sababu
sikutaka wapate shida kama niliyopata mimi. Upweke unatisha.
Mume wangu George hukuelewa ni kiasi gani nilivyokupenda
nilipokuwa hai. Lakini sasa utaelewa. KWA OFISA WA POLISI:
Tafadhali usichukue hatua yoyote dhidi ya mume wangu kwa
sababu hana kosa.”

Mtuhumiwa alishashtakiwa kwa makosa ya mauaji ya watoto


watatu. Katika kujitetea, Mtuhumiwa alimwita Daktari wa Afya ya
Akili (psychiatrist) ambaye aliieleza Mahakama kuwa mtuhumiwa
alikuwa na matatizo au ugonjwa wa kisaikolojia na hivyo
hakuelewa alichotenda ni kinyume cha sheria. Mahakama (Jaji
Makame) alikataa utetezi huo na kusema Mtuhumiwa alifahamu
alichokitenda kuwa ni kinyume cha sheria. Jaji alieleza katika
hukumu yake kuwa kesi hii ilikuwa inasikitisha na kutia huruma
sana — jinsi watoto walivyoitwa, na walivyokuwa wakiuliza, “mama
tunaenda wapi?” Jinsi watoto walivyokuwa wakiagwa na kubusiwa!
Kwa upande mwingine, alimhurumia Mtuhumiwa kwa matatizo
yaliyompata. Hadithi yake ya kufiwa na wazazi na kubaki yatima,
na uchungu uliompata alipoambiwa aondoke nyumbani la sivyo
atatolewa nje akiwa uchi. Ingawa Jaji hakutaka kumlaumu
mumewe moja kwa moja lakini alihoji ni kwanini basi asingefungia
hata kesi ya talaka kwa sababu alikuwa ni mwanasheria.
Mwishowe, Jaji alisema hakuwa na budi kuamua kufuatana na
sheria na kumtia Mtuhumiwa hatiani ingawa dhamiri yake ilikuwa
ikimwelekeza vinginevyo. Alivyoeleza, kama mikono yake
isingefungwa na sheria angemwachia lakini sheria haikumpa nafasi
hiyo.

Shauri hili ni mfano mwingine mzuri wa shauri linalohitaji


mamlaka ya Rais ya kutoa msamaha wa huruma kutumika. Kama
watu wangeulizwa kama adhabu ya kifo itekelezwe au la,
inawezekana wengine wangesema itekelezwe lakini bila shaka
kuna wengine wangesema asamehewe. Hii ni kutokana na
mazingira ya kesi yenyewe. Sheria zinapotungwa haziwezi
kuzingatia kila kitu. Wanaotunga sheria hawawezi kujua kitu gani

30
kitatokea kesho, kesho kutwa na miaka ishirini ijayo. Mara nyingi
sheria haitofautishi kesi moja na nyingine zinazoweza kutokea
katika mazingira tofauti. Ni akili ya binadamu ndiyo inayoweza
kutofautisha na kusema, “kesi hii imetokea katika mazingira tofauti
na inafaa kushughulikiwa kwa namna tofauti.”

2.4 MAPENDEKEZO
Sababu zilizoainishwa hapo juu zinaonyesha mamlaka ya kutoa
msamaha ni muhimu na kiongozi wa nchi anastahili kuendelea
kuwa na mamlaka ya aina hii. Inaelekea malalamiko mengi
yanasababishwa na maoni kuwa madaraka ya aina hii yanaweza
kutumika kuwasamehe watu ambao jamii huona hawastahili
kusamehewa. Hivyo basi, Katiba mpya iweke udhibiti wa madaraka
ya msamaha ili yasiweze kutumika vibaya. Ili kufanikisha hili,
tunatoa mapendekezo haya:

 Katiba mpya ianzishe Kamati ya Kumshauri Rais kuhusiana


na misamaha;
 Kamati ya Ushauri ijumuishe wajumbe huru ambao siyo
watumishi wa Serikali. Kamati inaweza kujumuisha wadau
kama Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mwakilishi wa Jeshi la
Magereza, mwakilishi wa Jeshi la Polisi, mtaalamu wa tiba,
ofisa wa ustawi wa jamii, viongozi wa dini, wawakilishi wa
wahanga (victims of crime), wawakilishi wa taasisi zisizo za
kiserikali (NGOs), n.k.;
 Katiba mpya ieleze bayana mipaka ya Rais katika kutoa
misamaha. Isitoe tu mamlaka yasiyo na mipaka.

 Katiba iruhusu mwananchi yeyote kupinga msamaha


Mahakamani kupitia utaratibu wa mapitio (judicial review).
Siku za nyuma huko Uingereza msimamo wa sheria ulikuwa
mtu hawezi kuhoji matumizi ya kutoa msamaha
Mahakamani. Hata hapa Tanzania kwa sasa siyo rahisi kwa
Mahakama kuhoji mamlaka ya kutoa msamaha kwa kuwa
Katiba imempa Rais hiari ya moja kwa moja (absolute
discretion). Msimamo huu wa sheria umeanza kuhojiwa hata
huko Uingereza ulikoanzia: katika shauri la Council of Civil
Service Unions v Minister for Civil Service [1984] 3 All ER 935
at 951, Jaji Roskill wa Mahakama ya Kibwenyenye (House of
Lords) alisema wananchi wanayo haki ya kuhoji namna

31
mamlaka ya asili ya kifalme (prerogative powers)
yanavyotumika.1 Na katika shauri jingine, R. v Secretary of
State for the Home Department, ex parte Bentley, [1994] Q.B.
349, ilielezwa kuwa msamaha unaweza kuhojiwa
Mahakamani kwa utaratibu wa marejeo (judicial review).2

 Katiba iseme ni “lazima” Bunge litunge sheria ambayo


itaelekeza namna mamlaka ya kutoa msamaha
yatakavyotekelezwa (kwa mfano, sheria inaweza kuweka
utaratibu wa uwazi kama kutangaza majina ya wanaoomba
msamaha katika magazeti; jinsi ya kuishirikisha jamii ya
muomba msamaha na wahanga (victims); kueleza kuwa
wahalifu sugu hawawezi kupewa msamaha, au waliotenda
makosa ya aina fulani hawatapewa msamaha, kuianisha
utaratibu wa kulalamika kwa watu waliobaguliwa kupata
msamaha kwa sababu za rushwa, upendeleo, au sababu
zingine, na kadhalika). Katiba iweke kanuni za ujumla
(general principles). Masuala mengine yawe katika sheria kwa
sababu ni rahisi kwa Bunge kuibadilisha sheria kila
inapohitajika. Mathalan, ikifika wakati fulani jamii haitaki,
kwa mfano, wala rushwa wasamehewe, basi Bunge
litarekebisha sheria na kusema Rais hatowasamehe watu
waliotiwa hatiani kwa makosa ya rushwa.

 Ili Bunge liweze kutunga sheria inayosimamia misamaha,


Katiba isitoe mamlaka ya ujumla (absolute power) kwa Rais
kama ilivyo sasa ambapo Rais amepewa mamlaka ya
kumsamehe “mtu yeyote” anayetumikia “adhabu yeyote”
kuhusiana na “kosa lolote.”

1 Haya ndiyo maneno ya Jaji Roskill: “If the executive in pursuance of a statutory
power does an act affecting the rights of a citizen, it is beyond question that in
principle the manner of the exercise of that power may today be challenged. If the
executive acting under a statutory power acts under a prerogative power… so as
to affect the rights of a citizen, I am unable to see that there is any logical reason
why the fact that the source of the power is prerogative and not statutory should
today deprive the citizens of that right of challenge to the manner of its
exercise….To talk of the act as an act of the sovereign speaks of anarchism of the
past centuries.”
2 Shauri hili limenukuliwa katika B. V Harris, “Judicial Review, Justiciability and

the Prerogative of Mercy”, in The Cambridge Law Journal, Vol. 62, No. 3 (Nov,
2003), pp. 631-660, p. 650.
32
SEHEMU YA TATU

3.1 MAMLAKA YA KUTANGAZA HALI YA HATARI

3.1.1 Hoja
Kuna maoni kuwa mamlaka ambayo Rais amepewa na Katiba
yaondolewe. Na kuna watu wengine wanaosema kuwa madaraka
hayo yapunguzwe.

3.1.2 Maelezo ya Ujumla


Kila nchi inaweza ikajikuta katika haja ya kuipa Serikali yake
mamlaka makubwa hata kama italazimu kukiuka baadhi ya haki
za binadamu na baadhi ya sheria za nchi ili kuweza kukabiliana na
hatari ambayo inaikabili nchi au sehemu yake. Mfano nchi
inaweza ikajikuta katika hali ya uvunjifu mkubwa wa amani au
majanga makubwa kiasi kwamba katika kukabiliana na hali hiyo
Serikali itahitaji kutumia nguvu kubwa kukabiliana na hali hiyo
hata kama kwa kufanya hivyo itakuwa inakiuka haki za binadamu
au kuvunja baadhi ya sheria za nchi.

Mtaalamu mmoja wa masuala ya Katiba, Clinton Rossiter (1917-


1970), aliita madaraka ya kutangaza hali ya hatari ‘udikteta wa
kikatiba’1, kwa maana Katiba ya nchi inaruhusu Serikali kutawala
kidikteta katika kukabiliana na hatari kubwa inayoikabili nchi.
Hali hizo zinaweza kuwa vita, majanga makubwa ya kiasili, uasi
n.k.

Udikteta huo wa Serikali unakuwa ni muhimu kwa mustakabali wa


nchi na watu wake. Salus respublicae suprema lex esto, yaani
ulinzi na usalama wa watu ndio sheria kubwa kuliko zote. Kwa
sababu hiyo Katiba na sheria za nchi mbalimbali zinaruhusu
Serikali kukiuka haki za binadamu, kanuni na taratibu zingine
ikiwemo kusimamisha au kurekebisha baadhi ya sheria za nchi ili
kukabiliana na hali iliyopo katika kulinda mustakabali wa nchi.
Sheria ya Uingereza ijulikanayo kama The British Defence of the
Realm Act, 1914 iliweka Uingereza kwenye utawala sawa na wa

1Clinton, Rossiter (1948). Constitutional Dictatorship: Crisis Government in the


Modern Democracies. London, Oxford University Press
33
kijeshi wakati wa vita ya kwanza ya dunia1. Hali hiyo inatokana na
kuwa uzoefu wa nchi za Ulaya unaonyesha kuwa sheria za kiimla
ni lazima na muhimu ili kukabiliana na vita ama dharura kubwa2.

3.1.3 Viwango vya Kimataifa katika kutangaza hali ya hatari

Mikataba mbalimbali ya kimataifa zimeweka viwango vya kufuatwa


na nchi mbalimbali katika kushughulikia madaraka ya kutangaza
hali ya hatari ili kulinda haki za binadamu katika hali ya hatari.
Ibara ya 4(2) ya Mkataba wa Kimataifa Juu ya Haki za Kiraia na
Kisiasa [the International Covenant on Civil and Political Rights
(ICCPR)] inataja baadhi ya haki ambazo hazipaswi kukiukwa hata
kama nchi iko katika hali ya hatari. Haki hizo ni pamoja na haki ya
kuishi , haki ya kutokuwa mtumwa, haki ya kutambuliwa kuwa ni
mtu mbele ya sheria, haki ya mtu kuwa na imani anayotaka, haki
ya kutoteswa na kudhalilishwa ubinadamu. Haki hizo zimewekwa
kwenye sheria mbalimbali za kimataifa ikiwemo ibara ya 15 ya
Mkataba wa Ulaya wa Haki za Binadamu na Uhuru wa Msingi (the
European Convention for the Protection of Human Rights and
Fundamental Freedoms) na ibara ya 27 ya Mkataba wa Amerika
juu ya Haki za Binadamu (American Convention on Human Rights)3.

Tanzania ni mwanachama wa ICCPR, ambayo imeweka sifa za


msingi za kutangaza hali ya hatari4. Sifa hizi zinaendana na zile za
Shirika la Kimataifa la Wanasheria (International Law Association)
kupitia kile kinachoitwa Viwango vya Paris au ‘Paris Minimum
Standards’ ambayo ilipitishwa mwaka 1984. Sifa kubwa tano za
kutangaza hali ya hatari kulingana na vyombo hivi viwili . Kwanza,
Lazima hali ya hatari iwepo au inakaribia kutokea. Pili, hali ya
hatari iwe inagusa watu wote katika eneo ilipotangazwa hali ya
hatari. Tatu, hatari iwe inatishia uhai wa Taifa. Hii inaweza kuwa ni
hatari juu ya uwepo wa watu, usalama wa mipaka au utendaji wa
vyombo vya dola. Nne, tangazo la hali ya hatari liwe ni hatua ya
mwisho baada ya hatua zingine zozote kushindwa kukabiliana na
hali iliyopo. Tano, tangazo la hali ya hatari liwe ni hatua ya muda

1 Clark, R. (1990). Presidentail Emergency Powers : The Contribution of Lindsay


Rogers. Presidential Studies Quarterly, Vol.20.No.1 pp 13-30.
2 Kama hapo juu.
3 The European Convention on Human Rights and Fundamental Freedoms (ECHR)

was signed in 1950 and came into force in 1953, the International Covenant on
Civil and Political Rights (ICCPR) was signed in 1966 and came into force in in
1976 and the American Convention on Human Rights6 (ACHR) was signed in 1969
and came into force in 1978
4Tanzania ilisaini ICCPR tarehe 11 Juni 1976

34
mfupi. Hii ina maana kuwa tangazo la hali ya hatari liwe ni la muda
maalumu na linaweza kuongezwa tu kwa utaratibu uliowekwa na
sheria1.

Sheria na mikataba ya kimataifa inaorodhesha sababu kubwa nne


za kutangaza hali ya hatari nazo ni : Moja, wakati kuna vita, hasa
pale ambapo nchi imevamiwa. Katika hali hiyo kuna haja ya
kufanya uamuzi wa haraka na mgumu ambao unaweza
kusababisha baadhi ya haki ambazo zinatumika wakati wa amani
zisimamishwe. Mbili, pale ambapo pana uasi na vitendo vingine
ambavyo vinalenga kuiangusha Serikali iliyochaguliwa kihalali.
Tatu, pale ambapo kuna majanga makubwa ya kimataifa kama vile
matetemeko, mafuriko, milipuko ya volkano au majanga mengine.
Nne, Pale ambapo kuna matatizo makubwa ya kiuchumi kiasi cha
kuhatarisha uhai wa Taifa2.

Angalau kanuni sita zimebainishwa kuwa ni muhimu kufuata


katika kutangaza hali ya hatari. Hizi ni;

1. Kanuni ya Tishio la kipekee ;


2. Kanuni ya kutoa Tangazo la Hali ya Hatari ;
3. Kanuni ya kutoa Taarifa kwa Taifa ;
4. Hatua ya Kutokiukwa kwa haki za msingi;
5. Kanuni ya uwiano;
6. Kanuni ya kutokuwa na ubaguzi; na
7. Kanuni ya kufanana na sheria za kimataifa 3.

Pamoja na kanuni hizo ambazo zinaweza kutumika kutathmini


utaratibu wa kutangaza hali ya hatari kwenye nchi yeyote,
kunapaswa kuwepo njia za kudhibiti madaraka hayo yasitumike
vibaya au kutumiwa bila sababu ya msingi. Hii ni kwa sababu
kutangaza hali ya hatari kunaambatana na athari kubwa kwa Taifa
na haki za wananchi. Kama ilivyoonyeshwa hapo juu, utangazaji wa
hali ya hatari unaidhinisha dola kuchukua hatua zisizo za kawaida
ambazo zitaathiri haki za kawaida za kiraia na kibinadamu.Hivyo
basi, madaraka hayo yanapaswa kudhibitiwa.

1 Fombad , C.M.(2004). Cameroon’s Emergency Powers: A Recipe for (Un)


constitutional Dictatorship? In the Journal of African Law,School of Oriental and
African Studies. P.66
2 Kama hapo juu, p. 67. Rais Franklin Roosevelt wa Marekani alitumia madaraka

ya hali ya hatari kupambana na mbinyo wa kiuchumi(Great Depression) wa


miaka ya 1930
3 Oraa, J., (1992). Human Rights in States of Emergency in International Law,

Oxford, Clarendon Press


35
3.1.4 Ulinganifu wa Tanzania na viwango vya Kimataifa

Madaraka ya Rais kutangaza hali ya hatari yamewekwa na


kufafanuliwa na ibara ya 32 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania. Madaraka ya Rais na utekelezaji wa madaraka ya
kutangaza hali ya hatari yamefafanuliwa na Sheria ya Madaraka ya
Hali ya Hatari (The Emergency Powers Act1). Kwa mujibu wa
Kifungu cha 6-18 cha sheria hii, madaraka ya Rais yanajumuisha
kukamata na kuweka kizuizini watuhumiwa; kuthibiti taasisi na
asasi mbalimbali na kuzuia na kuthibiti machapisho mbalimbali.
Mengine ni kuzuia magazeti kuingia ndani ya nchi2, kuzuia
kuingiza, kupeleka nje ya nchi au kusambaza bidhaa fulani;
kuthibiti usafiri wa barabara, ndege, majini n.k; . Rais pia ana
madaraka ya kuzuia mikutano au maadamano; kutoa maagizo ya
kutelekeza amri; kutoa hati ya upekuzi; kusimamisha, kurekebisha
au kuzuia sheria zisitumike. Hata hivyo, ni muhimu kujua kuwa
inaonekana mpaka sasa madaraka haya hayajawahi kutumiwa3.

Kanuni sita ambazo zimetajwa hapo juu ni kipimo sawia kuona


kama mfumo wa utangazaji hali ya hatari ndani ya nchi unaendana
na misingi inayokubalika kimataifa. Tathmini hiyo infanyika hapa
chini;

Kanuni ya kwanza inataka tangazo la hali ya hatari litangazwe


rasmi na Serikali kufuatia tishio lisilo la kwaida kwa nchi. Lengo la
kanuni hii ni kuondoa uwezekano wa hali ya hatari kugeuzwa kuwa
ndio mfumo wa utawala. Ibara ya 32(1) ya Katiba ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania inampa Rais madaraka ya kutangaza hali
ya hatari katika Jamhuri ya Muungano au katika sehemu yake
yeyote. Rais aweza kutangaza hali ya hatari iwapo nchi iko katika
vita; au kuna hatari ya nchi kuvamiwa au kuingia katika hali ya
vita; au kuna hali ya kuvurugika kwa amani ndani ya nchi au
katika sehemu yeyote ya nchi kiasi kwamba ni lazima kuchukua

1 Cap 221 [RE 2002].


2 Kwa mujibu wa Sheria ya Magazeti [The Newspapers Act, Cap. 229], neno
magazeti linajumuisha machapisho yoyote yenye habari au taarifa yenye maslahi
kwa umma au sehemu yake.
3 Statement by Hon. Mathias Meinrad Chikawe (MP), Minister for Constitutional

Affairs and Justice of the United Republic of Tanzania during the consideration of
Tanzania`s Fourth Periodic Report on the International Covenant on Civil and
Political Rights (ICCPR) to the United Nations Human Rights Committee Geneva,
Switzerland, 13 - 14 July 2009, p.13.
36
hatua za kipekee ili kurejesha amani na usalama; au karibu
kutatokea tukio la hatari; au tukio la balaa; au la baa la
kimazingira ambalo linatishia jamii; au sehemu ya jamii katika
Jamhuri ya Muungano; au kuna aina yeyote ya hatari ambayo ni
dhahiri ni tishio kwa nchi[Ibara ya 32(2)]. Mfumo huu unatumiwa
pia na nchi kama Urusi na Marekani.

Pili, viwango vya kimataifa vinataka kutolewe taarifa kwa Taifa juu
ya tangazo la hali ya hatari. Hali ilivyo ni kwamba ; Rais lazima
apeleke nakala ya tangazo la hali ya hatari Bungeni ili lijadiliwe na
kuidhinishwa na Wabunge wasiopungua theluthi mbili ya wajumbe
wote[Ibara ya 32(3)]. Hapa, Bunge lina wajibu wa kudhibiti
madaraka ya Rais yasitumike vibaya au bila sababu ya msingi.

Pia, tangazo la hali ya hatari limewekewa muda maalumu. Ibara ya


32 (5) ya Katiba inaelekeza kuwa tangazo la hali ya hatari
lililotolewa na Rais litakoma iwapo litafutwa na Rais; au zitapita
siku kumi na nne tangu tangazo lilipotolewa kabla ya kupitishwa
na azimio la Bunge au baada ya kupita muda wa miezi sita tangu
tangazo hilo lilipotolewa. Kikao cha Bunge chaweza , kabla ya muda
huo kuisha kuongeza mara kwa mara muda wa tangazo hilo
kutumika kwa vipindi vya miezi mingine sita kwa azimio
litakaloungwa mkono na wajumbe wasiopungua theluthi mbili ya
kikao hicho; au wakati wowote ambapo mkutano wa Bunge
utalitengua tangazo hilo kwa azimio litakaloungwa mkono na
wajumbe wasiopungua theluthi mbili ya wajumbe wote [Ibara ya
32(5)]. Uwezo wa Bunge kutengua tangazo la hali ya hatari wakati
wowote ni njia ya kudhibiti madaraka ya Rais yasitumike vibaya.
Utaratibu huu wa kulipa Bunge kura ya veto dhidi ya uamuzi wa
Rais kutangaza hali ya hatari unatumika pia katika nchi zingine
kama vile Namibia na Marekani.

Zaidi ya hapo, hali ya hatari iliyotangazwa itatumika tu katika


eneo la Jamhuri ya Muungano ambapo hali ya hatari imetangazwa
[Ibara ya 32(6)]. Pia, hatua zinazochokuliwa wakati wa kutekeleza
hali ya hatari lazima ziwe kwa kiasi ambacho ni lazima na halali
kwa ajili ya kushughulikia hali iliyopo.

Mwisho, Katiba inabainisha kuwa kutangazwa hali ya hatari


hakuidhinishi mtu kunyang’anywa haki yake ya kuwa hai
isipokuwa tu kwa kifo kama matokeo ya matendo ya kivita.

37
Kama inavyoonekana hapo juu, madaraka ya kutangaza hali ya
hatari unazingatia vigezo na misingi ya sheria za kimataifa. Na kwa
kweli mfumo uliopo Tanzania unatumika na nchi zingine nyingi
duniani ikiwemo Marekani, Uingereza, Uganda, Namibia na Urusi.

3.1.5 Mamlaka ya kutangaza Vita

Sambamba na madaraka ya kutangaza hali ya hatari, Rais ana


madaraka ya kutangaza vita kati ya Jamhuri ya Muungano na nchi
yoyote.1 Baada ya kutoa tangazo la vita, Rais atapeleka nakala ya
tangazo hilo Bungeni ambapo Bunge litaamua kupitisha au
kutopitisha tangazo la vita lililotolewa na Rais.2 Swala hapa ni
kuwa kulingana na sheria za kivita, kwa kutoa tangazo la vita, Rais
atakuwa ameingiza nchi vitani na uamuzi wowote wa Bunge
unaweza usiwe na maana kwani nchi itakuwa tayari iko vitani. Kwa
sheria za kimataifa, tangazo la vita linaruhusu nchi nyingine
kuanza kushambulia na hivyo nchi itakuwa imeshaingia vitani bila
kujali Bunge litapitisha azimio la kutounga mkono vita au la.

Uzoefu tofauti na mfumo wa Tanzania ni wa Marekani ambapo


Bunge ndio lenye mamlaka ya kutangaza vita na sio Rais3. Ingawa
hiyo haimzuii Rais kuchukua hatua za kivita kwa jambo linalohitaji
uamuzi wa haraka katika kujilinda. Bunge la Marekani lilipitisha
sheria mwaka 1973 ijulikanayo kama The War Powers Act of 1973
ambayo iliweka wazi kuwa Rais atapeleka nchi vitani tu kutokana
na azimio la Bunge au kwa kujilinda na kujibu mashambulizi dhidi
ya nchi.4 Kifungu cha 4 cha sheria hii kinasema kuwa lengo kuu la
sheria hii ni kuhakikisha kuwa kuna uamuzi wa pamoja kati ya
Bunge na Rais katika kutangaza vita au kuendelea kupigana vita.5
Sheria hiyo imeweka utaratibu wa aina tatu;

 Rais kushauriana na Bunge kila inapowezekana kabla ya


kutangaza vita na mashauriano lazima yaendelee wakati wote
wa vita.

1 Ibara ya 44(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977.


2 Kama ilivyo juu, Ibara ya 44(2).
3 Ibara ya 1 kifungu cha 8(11) ya Katiba ya Marekani.
4 Currie, D.(2000).Rumors of Wars: Presidential and Congressional War Powers,

1809-1829: The University of Chicago Law Review, Vol. 67, No. 1 (Winter, 2000),
pp. 1-40.
5 Burgin, E.,(1992). Congress, the War Powers Resolution, &the Invasion of
Panama. Polity, Vol. 25, No. 2 (Winter, 1992), pp. 217-242
38
 Sheria inamtaka Rais apeleke Taarifa Bungeni ndani ya
masaa 48 pale ambapo hakuna vita lakini kuna uwezekano
wa kupeleka majeshi kwenye maeneo yenye uwezekano wa
kutokea vita, akieleza mazingira, mamlaka na wigo wa
matendo anayokusudia kufanya1.

 Rais atalazimika kusimamisha vita au mgogoro isipokuwa


pale ambapo amepata kibali rasmi cha Bunge. Ni jukumu la
Bunge kuongeza muda wa vita au muda wa kujitoa vitani;

 Ndani ya siku 60 mpaka 90 Bunge linaweza kuamuru jeshi


litoke vitani kwa azimio la Bunge ambapo Rais hawezi
kulipinga kwa veto.

Sheria hiyo ilipitishwa baada ya uzoefu uliotokana na vita ya


Vietnam kukabiliana na tabia ya Marais kuingiza nchi vitani wakati
ambapo vita ingeweza kuepukwa2.

Nchini Uganda Rais analazimika kutoa tangazo la vita baada ya


kupata kibali cha Bunge na kama hali imelazimisha Rais kutangaza
vita kabla ya Bunge kutoa kibali, Rais ataomba kibali baada ya
hapo3

3.2 MWISHO
Rais ana madaraka makubwa ya kutangaza hali ya hatari. Hata
hivyo, madaraka hayo ni muhimu ili kumuwezesha kukabiliana na
hatari kubwa inayolikabili Taifa. Kama alivyowahi kusema
Mwanafalsafa wa zamani wa Kiitaliano, Machiavelli, nchi ambazo
wakati wa hatari zitaacha kutumia njia za kiimla kukabiliana na
hatari hizo zitaweza kusambaratika.4

Katika hali ya vita, Rais kama Amiri-Jeshi-Mkuu anahitaji


madaraka ya kutosha kuweza kuchukua hatua zozote anazoona
zinafaa kumshinda adui ili kulinda usalama wa Raia na mali zao.

1 Kama hapo juu


2 Klieman, A.S.(1979). Preparing for the Hour of Need: Emergency Powers in the
United States in the Review of Politics, Vol. 41, No. 2 (Apr., 1979), pp. 235-255.
3 Ibara ya 124 ya Katiba ya Uganda, 2005.
4 Fombad , C.M.(2004). Cameroon’s Emergency Powers: A Recipe for
(Un)constitutional Dictatorship? In the Journal of African Law,School of Oriental
and African Studies, p.66.
39
Kwa vyoyote vile, kwa mfumo uliopo, madaraka ya ulinzi wa Taifa
hayawezi kuwekwa kwa mtu mwingine isipokuwa Rais.

Hata hivyo, madaraka ya Rais katika kutangaza hali ya hatari na


kutangaza vita hayo ni lazima yadhibitiwe kikatiba ili yasitumiwe
vibaya. Uzoefu wa zaidi ya miaka 200 ya Marekani unaonyesha
kuwa kuweka madaraka mengi kwa chombo kimoja inaweza kuleta
hatari kwa nchi. Hivyo, ni muhimu kuweka mfumo wa kudhibiti
utumiaji wa madaraka hayo ili kukabiliana na uwezekano wa
kutumia madaraka hayo vibaya. Kwa sababu hiyo inapendekezwa
hapa kuwa;

 Madaraka ya Rais kutangaza hali ya hatari yadhibitiwe na


Bunge yasije yakatumiwa vibaya. Rais aombe kibali cha
kutangaza hali ya hatari Bungeni kadiri inavyowezekana.
Bunge liwe na mamlaka ya kuidhinisha au kuzuia Rais
kutangaza hali ya hatari au kuliondoa tangazo la hali ya
hatari wakati wowote litakapoona kuna haja ya kufanya
hivyo;

 Jukumu la Mahakama la kulinda haki za watu na kudhibiti


matumizi mabaya ya madaraka ni muhimu yakatumika pia
kudhibiti matumizi mabaya ya madaraka ya kutangaza hali
ya hatari;

 Rais alazimike kushauriana na Bunge kabla ya kutangaza


vita. Kama alivyowahi kuonya Mwanafalsafa na Rais wa
zamani wa Marekani, James Madison kuwa kumpa Rais
madaraka ya kutangaza vita inaweza kuwa ni “ushawishi
mkubwa sana kwa mtu mmoja.”1 Rais asiruhusiwe
kutangaza vita bila ruhusa ya Bunge isipokuwa katika hali
ambayo nchi inaelekea kuvamiwa au tayari imeshavamiwa na
adui. Katika kushauriana na Bunge, Rais alazimike kutoa
taarifa muhimu ikiwemo kuhusu maslahi ya nchi yaliyo
katika hatari na sababu za kutumia njia ya vita kama njia
pekee ya kulinda maslahi hayo;

 Wakati wa vita Rais alazimike kutoa taarifa za mara kwa


mara kuhusu maendeleo ya vita.

1Nukuu kutoka barua ya Walter Jones, Mbunge wa Bunge la Marekani kwenda


kwa Rais wa nchi hiyo, Barack Obama ya tarehe 29 Agosti, 2012
40
SEHEMU YA NNE

4.1 NAFASI YA RAIS WAKATI WA UCHAGUZI

4.1.1 Hoja
Kuna maoni ya watu wengi kuwa wakati wa uchaguzi Rais asishike
madaraka. Wengi wanaotoa maoni ya aina hiyo wanapendekeza
kuwa Jaji Mkuu ashike madaraka wakati wa uchaguzi. Sababu za
mapendekezo ya namna hii ni tatu. Kwanza, ni vigumu kwa vyama
vya upinzani kushindana na Rais au chama chake kwa sababu
Rais anakuwa na mamlaka ya kidola na anaweza hata kuamuru
wakamatwe au kuzuiwa kufanya kampeni. Pili, Rais anapokuwa
madarakani wakati wa uchaguzi hutumia rasilimali za Kiserikali
kuendesha uchaguzi. Kuwepo kwake madarakani kunampa nafasi
kuwaamuru watumishi wengine kutoa vifaa kama magari na vitu
vingine vitumiwe na chama tawala wakati wa uchaguzi. Kwa
ujumla hoja ni kuwa hakuna usawa wa ushindani (level playing
ground) inapotokea kuwa mgombea mmojawapo anakuwa na
mamlaka ya Serikali au chama kimoja kuwa na mwanachama au
kiongozi ambaye ameshika mamlaka ya dola wakati wa uchaguzi.

4.1.2 Muda wa Rais Kushika Madaraka


Kwa mujibu wa ibara ya 42 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya
Muungano, 1977 Rais aliyechaguliwa anatakiwa kushika madaraka
ndani ya siku saba mara baada ya kutangazwa kuwa ameshinda
uchaguzi na Tume ya Uchaguzi. Na kwamba Rais atashika
madaraka kwa miaka mitano tangu alipochaguliwa isipokuwa tu
kama akifariki, akijiuzulu au akiondolewa kwa namna nyingine.
Hata kama Rais akifariki, akijiuzulu au kuondolewa, hakuna
utaratibu ambao kiti cha Urais kitakuwa wazi. Mojawapo ya
matukio hayo likitokea, Makamu wa Rais ataapishwa mara moja na
kushika madaraka na kuwa Rais mpya.

4.1.3 Changamoto za Uchaguzi


Hoja ya kutaka Katiba mpya izuie Rais kuwa madarakani wakati
wa uchaguzi inatokana na changamoto zinazotokea wakati wa
uchaguzi. Taarifa ya Waangalizi wa Uchaguzi wa Jumuiya ya
Madola katika Uchaguzi wa Tanzania wa mwaka 2010 inaeleza
kupokea malalamiko kuwa chama tawala kilikuwa kikitumia
41
rasilimali za Serikali yakiwemo magari kinyume na Kanuni za
Uchaguzi.1 Taarifa hiyo inasisitiza na kupendekeza utamaduni wa
kufuata kanuni kwa kuzingatia vyombo vya dola kama Polisi
wanakuwa upande wa chama tawala.2 Nayo TEMCO katika Taarifa
yake inaeleza kuwa jinsi Mawaziri walivyokuwa wakitumia
rasilimali za Serikali, na kupewa ulinzi na vyombo vya dola.3
Taarifa ya TEMCO inaeleza pia kuwa Wakuu wa wilaya na mikoa
wakati wote wa kampeni walikuwa wakitumia magari ya Serikali
katika misafara ya kampeni ya chama tawala.4 Vile vile, Taarifa
hiyo inasema kuwa mgombea Urais wa chama tawala ambaye pia
alikuwa kiongozi wa nchi aliamua kufanya kampeni katika muda
ambao haukuruhusiwa na taratibu za uchaguzi kitendo ambacho
kiliigwa na vyama vya upinzani.5

Pillipo Damas anaeleza kwa jinsi ambavyo Sheria ya Gharama za


Uchanguzi (The Election Expenses Act, 2010) haikufuatwa wakati
wa Uchaguzi Mkuu wa 2010 huko Bukoba. Anaeleza kulikuwa na
vitendo vya rushwa na changamoto nyingine nyingi lakini Tume ya
Uchaguzi, Msajili wa Vyama vya Siasa na TAKUKURU hawakufanya
chochote hata pamoja na kupewa taarifa mara kwa mara.6 Kama
alivyosema, vyombo vyote hivyo vimeundwa na Rais ambaye naye ni
mgombea na hivyo havikuwa na uhuru.7

Tatizo la malalamiko ya kukosekana kwa uwanja sawa na


mashindano ya kisiasa (level playing field) ni la siku nyingi. Shauri
la Attorney-General and two others v Aman Walid Kabourou [1996]
TLR 156 lilihusu moja ya chaguzi za mwanzo kabisa katika mfumo
wa siasa ya vyama vingi. Lilihusu uchaguzi mdogo wa jimbo la ujiji
uliofanyaika tarehe 13 Februari 1994. Mahakama ya Rufani ilieleza
kuwa Serikali iliamua kukarabati barabara ya Kigoma-Ujiji wakati
kampeni ya uchaguzi kitendo ambacho kilikuwa ni rushwa. Hii

1 Anagalia Ripoti ya Kundi la Waangalizi wa Uchaguzi la Jumuiya ya Madola


katika Uchaguzi wa Tanzania, 2010, uk. 21.
2 Ripoti ya Kundi la Waangalizi wa Uchaguzi la Jumuiya ya Madola katika

Uchaguzi wa Tanzania, 2010, uk.24.


3 TEMCO, The 2010 Tanzania General Elections, p.207.
4 TEMCO, The 2010 Tanzania General Elections, p.207.
5 Kama iliyo hapo juu, uk. 208.
6 Damas, Phillipo, (2012), The Challenges of Enforcing the Election Expenses Act,

2010: A Case Study of Bukoba District, LL.B. Dissertation submitted to the


University of Dar es Salaam, p.43.
7 Damas, Phillipo, (2012), The Challenges of Enforcing the Election Expenses Act,

2010: A Case Study of Bukoba District, LL.B. Dissertation submitted to the


University of Dar es Salaam, p.43.
42
ilionyesha kuwa kulikuwa na tatizo la kutotenganisha shughuli za
Serikali na chama. Aidha, Mahakama ilisema kuwa Radio
Tanzania, Dar es Salaam, ilikipendelea chama tawala. Vilevile,
Mahakama ilisema Mawaziri walishiriki kufanya kampeni kwa
namna ambayo ilikuwa kinyume cha sheria na taratibu za uongozi.

Katika shauri la Joseph Mwandu Kashindye v Dalaly Peter Kafumu


and two others1 , ambalo lilihusu uchaguzi mdogo wa Igunga
uliofanyika tarehe 2 Oktoba 2011. Mahakama ilielezwa na kukubali
kuwa Serikali iligawa chakula wakati wa uchaguzi; na kwamba
Waziri alitoa vitisho kuwa endapo mgombea wa chama tawala
hatochaguliwa basi daraja lisingejengwa. Ikumbukwe kuwa
uchaguzi huo mdogo ulitawaliwa na fujo ambazo hazijawahi
kuonekana katika nchi yetu katika mazingira ya uchaguzi. Vyama
vya siasa viliendesha kampeni kana kwamba hapakuwa na sheria
kabisa.

Shauri hili lilionyesha kuwa changamoto zilizokuwepo mwaka 1994


wakati mfumo wa vyama vingi ulikuwa na miaka miwili tu bado
zipo hata baada ya mfumo huo kuwepo kwa miaka 20. Kujihusisha
kwa Mawaziri katika kampeni ilionyesha tatizo bado ni lile lile —
hakuna utenganisho wa Serikali na chama tawala wakati wa
uchaguzi. Inaelekea Taifa letu halijapiga hatua katika kutengeneza
mfumo wa uchaguzi ambao unakubalika kwa wadau wote. Hivyo,
inaonekana kuwa ni changamoto hizi ndizo zinawafanya watu
kufikiria ni vizuri Rais asiwe madarakani wakati wa uchaguzi.

4.1.4 Tathmini ya Hoja


Utafiti ulijaribu kuangalia kama kuna nchi nyingine ambayo kuna
utaratibu wa Rais wa nchi kutokuwa madarakani wakati wa
uchaguzi lakini haukufanikiwa kuona mfano hata mmoja. Katiba
ya Nchi ya Ufilipino inamzuia Rais wa nchi hiyo kufanya uteuzi
miezi miwili kabla ya uchaguzi, wakati wa uchaguzi, na mara ya
uchaguzi kabla ya Rais mteule kuanza kazi.2 Hali kadhalika, Katiba

1 High Court (Tabora Registry) (sitting at Nzega) Miscellaneous Civil Cause NO. 10
of 2011(unreported).

2Ibara ya VII Kifungu cha 15 cha Katiba ya Jamhuri ya Ufilipino ya Mwaka 1987
kinasema, “Two months immediately before the next presidential elections and
up to the end of his term, a President or Acting President shall not make
appointments, except temporary appointments to executive positions when
43
ya Kenya imemzuia mtu anayekaimu madaraka ya Rais kufanya
uteuzi wa maofisa fulani au kutekeleza madaraka fulani ya Rais
wakati wa uchaguzi.1 Inaelekea Katiba hizi mbili zinazuia matumizi
mabaya ya madaraka wakati uchaguzi lakini hazisemi kuwa Rais
hatakuwa madarakani wakati wa uchaguzi.

Ingawa utafiti haukuona nchi ambayo ina utaratibu wa Rais


kuondoka madarakani haina maana kuwa Watanzania hawawezi
kuweka utaratibu ambao unajaribu kutatua changamoto zilizopo
katika nchi yao, la hasha. Isipokuwa katika kuangalia mazingira
yetu utaratibu wa Rais kuondoka madarakani wakati wa uchaguzi
unaweza kuleta matatizo makubwa zaidi. Kwanza, Rais ni kiongozi
wa Serikali, Mkuu wa Nchi na Amiri-Jeshi-Mkuu. Hivyo, kuondoka
madarakani au kukasimu madaraka yake kwa mtu mwingine
ambaye hakuchaguliwa na wananchi inaweza kuleta hatari ya
kiusalama katika nchi. Pili, hali hiyo inaweza kusababisha ombwe
(vacuum) la uongozi. Hii inatokana na ukweli kuwa watumishi wa
Serikali na vyombo vya ulinzi na usalama vyaweza kutomtii mtu
anayeshikilia ofisi ya Rais kwa muda. Suala la nidhamu na utii kwa
watumishi wa Serikali ni muhimu wakati wote. Watumishi
wanaweza kukataa kutekeleza maagizo yake kwa kuwa wanajua
atakaa madarakani kwa muda mfupi. Hali kama hii inaweza kuleta
fujo (anarchy) katika nchi wakati wa uchaguzi. Tatu, mtu
anayeshikilia madaraka kwa muda anaweza kubadilika na kukataa
kukabidhi madaraka kwa kisingizio kuwa taratibu za uchaguzi
zilikiukwa na kwamba ameamua kuufuta uchaguzi mpaka hapo
baadaye ili aendelee kuwa madarakani. Kutokana na sababu hizi,
utaratibu wa Rais kuondoka madarakani wakati wa uchaguzi siyo
utaratibu mzuri. Labda ni kutokana na sababu kama hizi Katiba ya
Iran inatamka kwa namna ya msisitizo kuwa Rais atakuwa
madarakani hata katika kipindi cha uchaguzi.2

4.2 MAPENDEKEZO
Kutokana na sababu zilizoainishwa hapo juu inapendekezwa kuwa
Katiba itamke kuwa Rais aendelee kuwa madarakani kama ilivyo
katika Katiba ya sasa. Lakini Katiba inatakiwa kufanya yafuatayo

continued vacancies therein will prejudice public service or endanger public


safety.”
1 Ibara ya 34 ya Katiba ya Kenya, 2010.
2 Ibara ya 119 ya Katiba ya Jamhuri ya Kiislam ya Iran, 1979.

44
ili kushughulikia matatizo yaliyosababisha watu kusema asiwe
madarakani wakati wa uchaguzi;
 Sheria ya Uchaguzi, Kanuni za Uchaguzi (The Election Code of
Conduct) na Sheria ya Gharama za Uchaguzi zinazuia
matumizi ya rasilimali za Serikali katika uchaguzi. Rais ndiye
kiongozi nambari moja anayetakiwa kusimamia utekelezaji
wa sheria za nchi. Anapochaguliwa kuwa kiongozi wa nchi
ina maana anaaminiwa na wananchi kuifanya kazi hiyo kwa
uaminifu, na anaapa kuilinda Katiba na kufuata sheria.
Anatakiwa kuwahimiza viongozi wa juu, Mawaziri na
watumishi wegine wa Serikali kufuata sheria. Hivyo, akikiuka
kiapo chake Mahakama iwe na uwezo wa kuufuta uchaguzi.
Uchaguzi ukifutwa, Tume ya Uchaguzi iitishe uchaguzi
mwingine ambao hautamjumuisha Rais. Bila shaka, kurudia
uchaguzi ni gharama kubwa kwa nchi ambayo watu wake ni
maskini kama Tanzania. Hata hivyo, kupotea kwa haki ni
gharama kubwa zaidi kwa sababu watu wanaweza
kuchinjana na nchi kuingia kwenye machafuko makubwa.

 Endapo Mahakama itaona kwamba ukiukwaji uliofanywa


haukuwa mkubwa kiasi cha kuathiri matokeo ya uchaguzi
lakini kuna ushahidi kuwa Rais alielekeza au akifahamu
ukiukwaji husika basi Mahakama iliarifu Bunge kumfungulia
mashtaka (impeachment) ili aondolewe madarakani. Na kama
ikitokea hivyo Makamu wa Rais ashike madaraka. Hii
itaepusha gharama kubwa ya kurudia uchaguzi;

 Kuwe na Tume huru ya Uchaguzi ambayo itashughulikia


matatizo yanayotokea wakati wa uchaguzi bila kuegemea
upande wowote; na

 Vyombo vya uwajibikaji kama TAKUKURU na Polisi


vinatakiwa kuwa huru ili kusimamia uchaguzi kwa mujibu
wa sheria.

45
SEHEMU YA TANO

5.1 UDHIBITI WA MADARAKA YA RAIS NA


UWAJIBIKAJI
5.1.1 Hoja

Dhana ya udhibiti wa madaraka na uwajibikaji imejengeka katika


msingi kwamba madaraka makubwa kwa mtu mmoja au chombo
kimoja yanafanya udhibiti wake kuwa mgumu na hivyo uwezekano
mkubwa wa kuleta utawala wa kidikteta, ukiukwaji haki za watu
na matumizi mabaya ya madaraka, ugawaji wa rasilimali za nchi
kwa upendeleo na aina nyingine za matumizi mabaya ya madaraka
bila kizuizi chochote. Pia, madaraka makubwa yanafanya hatima ya
nchi itegemee utashi na uwezo binafsi wa Rais, kwa kuwa inakuwa
vigumu kwa jambo lolote kufanyika juu ya nchi bila ridhaa na
hisani ya Rais. Kwa mantiki hiyo, madaraka makubwa kwa mtu au
chombo kimoja ni hatari kwa mustakabali wa nchi.

Zaidi, madaraka makubwa kwa mtu mmoja au taasisi moja bila


udhibiti mahususi wa jinsi ya kutumia madaraka hayo, nchi
inaweza ikajikuta iko kwenye utawala wa mtu mmoja (Personal
rule). Mwanahistoria wa zamani wa Uingereza, Lord Acton aliwahi
kusema kuwa "Power tends to corrupt, and absolute power corrupts
absolutely. Great men are almost always bad men." Yaani,
madaraka makubwa yana tabia ya kuwaharibu waliyo nayo, na
wenye madaraka makubwa zaidi huharibika zaidi, kwa kuwa hata
watu wema hugeuka kuwa wabaya wakishakuwa na madaraka.

Ni kwa sababu hiyo, Mwanafalsafa wa zamani wa kifaransa,


Montesquieu (1689-1755) alibainisha kuwa kuna hatari kwa nchi
ikiwa mamlaka ya dola yatalundikwa kwa mtu au chombo kimoja,
hivyo basi ni vema yagawanywe kati ya Bunge, Serikali na
Mahakama1. Mawazo ya Montesquieu, yameleta ushawishi mkubwa
katika utengenezaji wa Katiba za nchi za Ulaya na Marekani. Hii
ina maana kuwa swala la udhibiti wa madaraka ya Rais ni
muhimu kwa mustakabali wa nchi yeyote. Kama Rais atakosa
madaraka ya kutosha kutekeleza majukumu yake au kama ana

1Montesquieu, 1748. L’Esprit des Lois, Book XI. The quotation is from Finer,
Herman, 1965. Theory and Practice of Modern Government. London: Methuen &
Co Ltd, pp 94-95
46
madaraka makubwa sana kuliko anayohitaji kutekeleza majukumu
yake itaathiri umadhubuti wa mfumo mzima wa kisiasa wa nchi.

Katiba ya sasa ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imegawa


mamlaka ya nchi baina ya mamlaka ya utendaji yaani Serikali
inayofanya kazi chini ya Rais, mamlaka ya kutekeleza utoaji haki
yaani Mahakama na mamlaka ya kutunga sheria na kusimamia
utekelezaji wa shughuli za umma, yaani Bunge1. Hata hivyo,
kumekuwa na maoni kuwa madaraka ya Rais ni makubwa sana na
hivyo yanapaswa kupunguzwa kwenye Katiba mpya.

5.1.2 Hali Halisi juu ya Madaraka ya Rais

1. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Mkuu wa Nchi,


Kiongozi wa Serikali na Amiri-Jeshi-Mkuu2. Kwa utamaduni wa
kisiasa uliopo, Rais pia huwa kiongozi wa chama chake cha
siasa. Kwa sababu hiyo Rais amepewa mamlaka mapana katika
kutekeleza Mamlaka yote ya Serikali ya Muungano na mambo
yote yahusuyo Tanzania Bara. Madaraka hayo yanawezwa
kutekelezwa na Rais mwenyewe moja kwa moja ama kwa
kukasimu madaraka hayo kwa watu wengine wenye madaraka
katika utumishi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano.3

2. Rais ana mamlaka ya kuanzisha na kufuta madaraka ya namna


mbalimbali katika utumishi wa Serikali ya Jamhuri ya
Muungano,kuteua watu wa kushika madaraka ya viongozi na
watendaji wakuu wa idara na taasisi za Serikali, kuwateua watu
wengine wote wasiokuwa viongozi wala watendaji wakuu,
kushika nafasi za madaraka,kuwapandisha vyeo na kuwaondoa
madarakani watu hao na kudhibiti nidhamu zao moja kwa moja
au kwa kushirikiana na Tume za Utumishi4;
(a) Katika Mhimili wa utendaji, Rais anafanya uteuzi wa
Makamu wa Rais(nafasi inapokuwa wazi)5, Waziri Mkuu6,
Mawaziri na Manaibu Waziri kadiri anavyoona yeye na

1 Ibara ya 4 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977


2 Kama ilivyo juu, Ibara ya 33(2).
3 Kama ilivyo juu, Ibara ya 34.
4 Kama ilivyo juu, Ibara ya 36.
5 Ibara ya 50 (4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka

1977
6 Kama ilivyo juu, Ibara ya 51(1).

47
kwa idadi anayotaka1, Mwanasheria Mkuu wa Serikali2,
Mkurugenzi wa mashtaka3, Katibu Mkuu Kiongozi,
Wakuu wa Mikoa4, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa
Halmashauri zote nchini5, Mkurugenzi wa Taasisi ya
Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU)6, Wakuu
wa Majeshi7, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania na Tume
ya Uchaguzi8; Kamishna wa Tume ya Maadili9, wakuu wa
idara na taasisi za Serikali zisizo chini ya wizara;10

(b) Katika mhimili wa Mahakama, Rais anateua Jaji Mkuu


na Majaji wa Mahakama ya Rufani11. Rais pia anamteua
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu na Majaji wa Mahakama
Kuu12. Msajili wa Mahakama ya Rufaa na Naibu wake,
Msajili wa Mahakama Kuu na Naibu wake, Mtawala Mkuu
wa Mahakama(Chief Court Administrator) pamoja na
Msajili Mkuu wa Mahakama13.

(c) Katika Mhimili wa Bunge, Rais anateua Katibu wa


Bunge14 na Wabunge wasiozidi 1015.Rais anateua
Mawaziri miongoni mwa Wabunge. Kiambatanisho 1
kinaorodha pana ya wateule wa Rais ingawa sio wote.

3. Kukubali au kukataa muswaada wowote uliopitishwa na Bunge


kuwa sheria;

1 Kama ilivyo juu, Ibara 55(1) and 55(2).


2 Kama ilivyo juu, Ibara ya 59 (1).
3 Kama ilivyo juu, Ibara ya 59B (1).
4 Kama ilivyo juu, Ibara ya 61(1).
5 The Public Service Act, 2002, kifungu cha 5(1)(a) ya Katiba ya Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977.


6 The Prevention and Combating of Corruption Act, Cap 329, Section 6(1) ya

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977.


7 Kama ilivyo juu, Ibara ya 148(2) (a).
8 Kama ilivyo juu, Ibara ya 74 (1).
9 The Public Code of Ethics Act, Cap 398 [RE 2002]m Kifungu 19(3).
10 The Public Service Act, 2002m Kifungu cha 5(1)(a).
11 Ibara ya 118 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977.
12 Kama ilivyo juu, Ibara ya 109.
13 The Judiciary Administration Act, 2011 kufungu cha 7(1) na 27(1).
14 Ibar aya 87 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977.
15 Kama ilivyo juu, Ibara ya 66(e).

48
4. Rais anaweza kutangaza vita kati ya Jamhuri ya Muungano na
nchi yoyote1

5. Rais anaweza kutoa msamaha kwa mtu yeyote aliyepatikana na


hatia mbele ya Mahakama kwa kosa lolote, na naweza kutoa
msamaha huo bila ya masharti au kwa masharti2

6. Rais anaweza kutangaza hali ya hatari kwa Jamhuri ya


Muungano yote au kwa sehemu yake3;

7. Rais anaweza kumuweka mtu yeyote kizuzini au kumhamisha


mtu kwenda sehemu yeyote ndani ya Jamhuri ya Muungano;
na4

8. Rais ni mdhamini wa ardhi na anaweza kuamua mabadiliko ya


matumizi ya ardhi kadiri atakavyoona inafaa5

Na Katika kutekeleza majukumu yake, Rais halazimiki kufuata


ushauri wa mtu yeyote au chombo chochote isipokuwa pale
anapotakiwa na Katiba kufanya hivyo6. Madaraka haya ya Rais
yasipowekewa udhibiti madhubuti yanaweza kumfanya Rais atumie
madaraka yake kwa ajili ya maslahi yake binafsi na si kwa mslahi
ya umma ikiwa ni pamoja na kugawa fadhila kinyume na
matakwa ya Katiba.

5.1.3 Chanzo cha Madaraka ya Rais

Madaraka ya Rais Tanzania kama ilivyo kwa nchi zingine zote, kwa
kiwango kikubwa ni matokeo ya historia ya nchi. Tanzania
ilitawaliwa na Wingereza tangu baada ya vita kuu ya kwanza ya
dunia mpaka ilipopata uhuru. Wakati wote, mwakilishi wa Mfalme
wa Uingereza, Gavana alikuwa na mamlaka yote ya Mkuu wa Nchi,
Mkuu wa Serikali na Amiri-Jeshi-Mkuu. Gavana alitawala kama

1 Ibara ya 44(1), ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka


1977.
2 Kama ilivyo juu, Ibara ya 45.
3 Kama ilivyo juu, Ibara ya 32.
4 The Preventive Detention Act 1962, Cap 361, [RE 2002] ya Katiba ya Jamhuri

ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977


5Kifungu cha 2(1)(a) cha Sheria ya Ardhi,[The Land Act, Cap 113 R.E 2002].
6 Ibara ya 37(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka
1977.
49
alivyopenda ili kufikia malengo ya ukoloni. Gavana alikuwa ni
mwajiri mkuu mwenye uwezo wa kuunda na kufuta ofisi kadiri
anyoona inafaa, alikuwa na uwezo wa kuajiri na kufukuza
watendaji wa Serikali. Gavana aliteua Mawaziri Majaji na watendaji
wa Mahakama. Ardhi yote ilitangazwa kuwa ni mali ya umma chini
ya udhamini wa Gavana kwa niaba ya Mfalme wa Uingereza.
Madaraka mengine ilikuwa ni kusamehe wafungwa, kuhamisha
watu kutoka sehemu moja ya nchi kwenda sehemu nyingine.
Gavana alikuwa na uwezo wa kutoa amri ya watu kuhamishwa
kutoka nchini kwenda nje ya nchi1.

Tanganyika ilipata uhuru mwaka 1961. Baada ya Uhuru,


madaraka ya Mkuu wa Nchi na Mkuu wa Serikali yalitenganishwa.
Gavana aliiendelea kuwa Mkuu wa Nchi na Amiri-Jeshi-Mkuu kwa
niaba ya Malkia wa Kiingereza. Kiongozi wa Serikali alikuwa ni
Waziri Mkuu, ambaye alikuwa ni kiongozi wa chama kilichopata
Wabunge wengi kwenye Uchaguzi Mkuu2. Gavana alikuwa na
madaraka ya kuteua Wabunge na pia wajumbe wa Tume ya
uchaguzi. Bunge lilizuiliwa kutengeneza muswada juu ya utozaji wa
kodi kwa namna yeyote isipokuwa kupunguza; kuagiza malipo au
matumizi ya fedha yafanywe kutokana na mfuko mkuu wa Hazina
ya Serikali au mfuko mwingine wowote ikifahamika kwamba fedha
iliyomo katika mifuko hiyo haikupangiwa ipangiwe kufanyika kwa
ajili ya matumizi hayo; kufuta au kusamehe deni lolote linalotakiwa
lilipwe na Serikali au kutoa hoja ya kushughulikia mambo
yaliyotajwa hapo juu .
3

Gavana alikuwa pia na uwezo wa kuvunja Bunge; kuanzisha na


kufuta ofisi za umma; kuteua Mawaziri na Manaibu wake kutoka
miongoni mwa Wabunge; kuteua na kufukuza maofisa wa umma4;
kusamehe wafungwa au kuwabadilishia adhabu kwa kadiri
anavyoona inafaa5; kuteua Majaji ikiwemo Jaji Mkuu na Tume ya
Utumishi wa Mahakama6 .

Mwaka 1962, kulikuwa na mabadiliko ya Katiba yaliyoifanya


Tanganyika kuwa Jamhuri chini ya Rais. Madaraka ya Mkuu wa

1 The Tanganyika Order in Council, 1920; Tanganyika (Legislative Council) Order


in Council, 1926.
2 Kifungu cha 41 cha The Tanganyika (Constitution) Order in Council, 1961.
3 Kifungu cha 37 (a) na (b) cha The Tanganyika (Constitution) Order in Council,

1961.
4 Kifungu cha 54
5 Kifungu cha 55, Kama ilivyo juu.
6 Kifungu cha 59, Kama ilivyo juu.

50
Nchi na Mkuu wa Serikali yaliunganishwa na kuwekwa kwa Rais.
Hivyo, Rais akawa Mkuu wa Nchi, Kiongozi wa Serikali na Amiri-
Jeshi-Mkuu. Madaraka ya Rais yaliongezwa kwa mabadiliko
yaliyofuata ya Katiba na kuundwa ama kurekebishwa kwa sheria
mbalimbali. Madaraka hayo yaliimarika zaidi baada ya kuundwa
kwa Jamhuri ya Muungano baada ya iliyokuwa Jamhuri ya
Tanganyika na Jamhuri ya Zanzibar kuungana na baada ya
kuundwa kwa Katiba ya kudumu ya Jamhuri ya Muungano ya
Mwaka 1977.

Rais wa Kwanza wa Tanzania, Julius Nyerere akizungumzia


madaraka ya Rais alishawahi kunukuliwa akisema madaraka ya
Rais ni makubwa kiasi cha kuweza kumfanya dikteta kama
akitaka1. Lakini madaraka hayo yalikuwa muhimu kwa kuwa
Tanzania ilihitaji Serikali yenye nguvu ili iweze kufanya kazi kwa
ufanisi na kuzuia upinzani na vikwazo mbalimbali katika ujenzi wa
Taifa2. Tanzania ilihitaji kukimbia wakati wengine wanatembea
katika kukabiliana na changamoto za ujenzi wa Taifa ili kujiletea
maendeleo.3

5.1.4 Uwajibikaji wa Rais

Madaraka makubwa ya Rais katika nchi za Afrika yamesababisha


udikteta na utawala mbovu kwa sababu ya kutokuwa na njia imara
za uwajibikaji katika matumizi ya madaraka hayo4. Katiba iliyopo
imetoa njia kuu tatu za kudhibiti na kumwajibisha Rais kwa
namna anavyotumia madaraka yake. Njia kuu hizo ni Uchaguzi,
Bunge na Mahakama;

Ibara ya 38 inawapa wananchi mamlaka ya kumchagua Rais


kupitia kura zao. Hii ina maana wananchi wanaweza kumwadhibu
Rais au kumzawadia Rais aliye madarakani kwa kumpigia au

1 Peter, C. M. (2000). Constitution Making in Tanzania: The Role of the People in


the Process. Dar es Salaam: University of Dar es Salaam.
2 Prempeh, K. (2008). Presidential Power in Comparative Perspective: The

Puzzling Persistence of Imperial Prseidency in Post-Authoritarian Africa. 35


Hastings Constitutional Law Quarterly 761, 784-795.
3 Nukuu ya Rais wa kwanza wa Tanzania “We must run while others walk”

kutoka kwa Mkandawire, T.(2011). Running While Others Walk: Knowledge and
the Challenge of Africa’s Development in Africa Development, Vol. XXXVI, No. 2,
2011, pp. 1– 36.
4 Nwabueze, B.O. (1974). Presidentialism in Commonwealth Africa, Hurst, London,

p. 1.
51
kumnyima kura yeye au wagombea anao waunga mkono au chama
chake kulingana na jinsi wanavyoridhika au kutoridhika na namna
anavyotumia madaraka yake. Hata hivyo, kuna mapungufu
ambayo yanaweza kuifanya njia ya uchaguzi ikashindwa kuwa
madhubuti katika kumfanya Rais awajibike ipasavyo.

Kwanza, kutokana na mabadiliko ya 13 ya Katiba yaliyofanyika


mwaka 2000, mgombea atatangazwa kuwa amechaguliwa kuwa
Rais iwapo tu amepata kura nyingi kuliko mgombea mwingine
yeyote.1 Ibara hii inatoa mwanya kwa Rais kuchaguliwa na watu
wachache na hivyo kubaki madarakani hata kama wananchi wengi
hawamtaki. Mfano mwaka 2001 mshindi wa Urais nchini Zambia
alipatikana kwa asilimia 29 ya kura zote. Hivyo hivyo, katika
uchaguzi wa Kenya wa mwaka 1992, Rais alipatikana kwa asilimia
36.3 ya kura zote. Ili kudhibiti hali hii, Katiba ya Tanganyika na
baadaye Tanzania kabla ya mabadiliko ya 13 ya Katiba ya mwaka
2000, mshindi wa Urais alilazimika kupata kura zaidi ya nusu ya
kura zote. Utaratibu huu unamfanya Rais aweze kuwajibika kwa
wananchi walio wengi tofauti na mfumo uliopo ambao unaweza
kumfanya mgombea kupata ushindi kutoka kwa kundi dogo la
wananchi, na hivyo kukosa uhalali wa kuongoza. Hali hii ni tofauti
katika Katiba ya Kenya ya mwaka 2010 inatamka kuwa mshindi wa
Urais atakuwa ni yule aliyepata zaidi ya kura zote2. Pia, Uganda
Katiba inataka Rais apatikane kwa zaidi ya nusu ya kura zote.3

Pili, ibara ya 41(7) imezuia Mahakama kuchunguza kuchaguliwa


kwa Rais. Hali hii inaweza kuwa kichocheo kwa Rais kutumia
mbinu chafu kushinda akijua kuwa baada ya kushinda hakuna
chombo cha kuchunguza ushindi wake. Rais anaweza kutumia
madaraka yake vibaya kufanikisha ushindi wake au wa chama
chake. Zaidi ya hayo, mfumo huu unatoa mwanya wa nchi
kuongozwa na mgombea aliyeshinda kwa njia haramu ikiwemo
ufadhili usio na maslahi kwa nchi. Ibara hii imeongezewa nguvu na
Ibara ya 74(12) ambayo imetamka kuwa “Hakuna Mahakama
yoyote itakayokuwa na mamlaka ya kuchunguza jambo lolote
lililotendwa na Tume ya Uchaguzi katika kutekeleza madaraka yake
kwa mujibu wa masharti ya ibara hii.” Tume ya Uchaguzi ina

1 Ibara ya 41(6).
2 Ibara ya 138(4)(a) ya Katiba ya Kenya.
3 Ibara ya 102 ya Katiba ya Uganda.
52
jukumu la kuratibu na kuendesha uchaguzi ikiwemo uchaguzi wa
Rais. Ili kuzuia uwezekano wa nchi kuongozwa na Rais ambaye
hajapatikana kihalali, Katiba ya Uganda ya Mwaka 1995 katika
ibara ya 104 inatoa mamlaka kwa Mahakama kuchunguza uhalali
wa matokeo ya Urais. Hivyo hivyo, Katiba ya Kenya ya Mwaka
2010, ibara ya 140 inatoa mamlaka kwa Mahakama kuchunguza
uhalali wa matokeo ya Urais.

Njia nyigine inayohusiana na uchaguzi katika kumdhibiti Rais na


kumfanya awajibike ni kuweka ukomo wa mtu kuendelea
kuchaguliwa kuwa Rais. Ibara ya 40 (2) ya Katiba imeweka ukomo
wa muda wa mtu kushika madaraka ya Rais kuwa vipindi viwili. Ni
muhimu tukaendelea kuwa na ukomo wa Urais kwa kuwa uzoefu
unaonyesha kuwa kukaa madarakani kwa muda mrefu kwenye
nafasi ya Urais kunafanya Marais wang’ang’anie madaraka na
kusababisha matatizo mengi kwa nchi ikiwemo vita za kugombea
madaraka. Na kwa kweli ung’ang’aniaji madaraka ni chanzo
kikubwa cha kudidimia kwa maendeleo ya nchi na kukua kwa
udikteta. Imebainika wazi kuwa, ofisi ya Rais ni muhimu sana
kwa nchi kushikiliwa na mtu mmoja kwa muda mrefu1. Kama
alivyopendekeza Mubako, ukomo wa madaraka unaifanya nchi
ijifunze kutegemea uwepo wa taasisi imara na sio bahati ya kuwa
na kiongozi mzuri2.

Bunge la Jamhuri ya Muungano limepewa mamlaka ya kudhibiti


madaraka ya Rais kwa njia za moja kwa moja na njia zisizo za moja
kwa moja (direct and indirect ways).

Kwanza, Bunge linaweza kumshtaki Rais na kupitisha hoja ya


kumuondoa Rais madarakani (impeachment). Hoja ya kumshtaki
Rais itatolewa ikiwa inadaiwa Rais ametenda vitendo ambavyo
vinavunja Katiba au sheria ya maadili ya viongozi wa umma,
ametenda vitendo vinavyohusu ukiukwaji wa maadili ya
uandikishwaji wa vyama vya siasa, amekua na mwenendo
unaodhalilisha kiti cha Rais3. Hata hivyo, kigezo hiki kinaonekana
kuwa na utata (ambinguous) kwa maana kinaweza kutumika
kukwepa baadhi ya makosa makubwa kama vile uhujumu uchumi

1 Hatchard, J., Ndulo, M., Slinn, P.(2010). Comparative Constitutionalism and


Good Governance in the
Commonwealth. Cambridge: Cambridge University Press.
2 S.VMubako, ‘The Constitution of the Republic of Zambia’, unpublished paper,

1972, p. 16.
3 Ibara ya 46A ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977

53
na rushwa ambayo yangepaswa yatajwe moja kwa moja1. Katiba
haijafafanua hatima ya Rais baada ya kuondoka madarakani
kutokana na mashtaka dhidi yake kuthibitika zaidi ya kukosa
malipo ya pensheni na haki za Rais mstaafu. Pia, ingefaa Katiba
itamke bayana makosa yanayoweza kumuondoa Rais madarakani.
Katika kushughulikia changamoto hiyo, Katiba ya Marekani
inatamka kuwa Rais, Makamu wa Rais, na “Maafisa wote wa umma
wa Marekani” wanaweza kuondolewa madarakani na Bunge
wakitiwa hatiani kwa makosa ya rushwa, uhaini au uhalifu
mwingine mkubwa2. Bunge limepewa mamlaka ya kumshtaki na
kumuondoa Rais madarakani3. Mtu aliyeondolewa kwenye nafasi
ya Urais kwa njia hiyo, anakosa sifa ya kushika nafasi zingine za
heshima,kuaminiwa au faida ndani ya nchi. Pamoja na hivyo, mtu
huyo anaweza kushtakiwa na kuadhibiwa kwa mujibu wa sheria.4
Pili, Katiba imeorodhesha njia mbalimbali ambazo Bunge linaweza
kudhibiti madaraka ya Rais5. Hii ni pamoja na;

(a) Kuuliza maswali kwa kwa Mawaziri Bungeni kuhusu


utendaji wa Serikali;
(b) Kujadili, kupitisha bajeti ya Serikali na mpango
wowote wa Serikali na kutunga sheria za kusimamia
utekelezaji wake;
(c) Kutunga sheria za kusimamia Serikali;
(d) Kuidhinisha mikataba mbalimbali ya kimataifa
ambayo Tanzania imeingia na ambayo inahitaji
kuidhinishwa;
(e) Kuithibitisha uteuzi wa Waziri Mkuu6;
(f) Kupitia kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu7;
(g) Kuidhinisha kutangaza hali ya hatari katika Jamhuri
ya Muungano au katika sehemu yake yoyote.8

1 Wambali, Michael, (2012). Paramount Issues for Consideration in the


Constitutional Review Process in Tanzania. The paper presented to the
Tanganyika Law Society(TLS) Annual Conference on “The Lawyers’Contribution to
the Process of Constitutional Review” held on 31st August, 2012 at the Arusha
International Conference Centre, Arusha, Tanzania.
2 Ibara ya II kifungu cha 4 cha Katiba ya Marekani.
3 Ibara ya I, kifungu cha 2(5), kifungu cha 3(6)].
4 Ibara ya 1, kifungu cha 3(7) cha Katiba ya Marekani.
5 Ibara ya 63(3) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977.
6 Kama ilivyo juu, Ibara ya 51 (2).
7 Ibara 53A(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977
8Kama ilivyo juu, Ibara ya 32(3).

54
Hata hivyo, uwezo wa Bunge kudhibiti madaraka ya Rais na kuleta
uwajibikaji unaweza kuathiriwa na mambo mbalimbali ikiwemo
yafuatayo;

Moja, mfumo wa kuteua Mawaziri na Manaibu wao kutoka


miongoni mwa Wabunge na uwepo wa Wabunge mpaka 10
wanaoteuliwa na Rais kunaongeza ushawishi wa Rais katika
utendaji wa Bunge na hivyo kuathiri uwezo wake wa kuisimamia na
kuiwajibisha serikali pale inapobidi. Rais pia anaweza kuteua
wakuu wa mikoa na wilaya kutoka miongoni mwa wabunge. Bunge
linaweza kushindwa kumdhibiti Rais na Serikali yake kwa kuwa
Serikali yake ni Wabunge wenzao. Pia, Wabunge wanaweza
kushindwa kufanya kazi ya kuisimamia Serikali kwa matazamio ya
kuteuliwa kuwa Mawaziri. Wabunge ambao ni Mawaziri, ambao
wanaweza kuwa wengi kwa kuwa Katiba haijaweka ukomo wa
idadi, wanamaslahi kuhakikisha kumlinda Rais na Serikali ambao
wao ni sehemu. Zaidi ya hayo, uteuzi wa Mawaziri miongoni mwa
Wabunge unafanya Bunge kuwa sehemu ya Serikali na hivyo
kushindwa kufanya kazi ya kuisimamia Serikali ipasavyo.

Ili kuleta uwajibikaji kati ya Bunge na Rais, Katiba ya Marekani


inazuia Mawaziri kuwa Wabunge na hivyo kuwa na utofauti kati ya
Bunge na Serikali. Hakuna Mbunge yeyote anaruhusiwa kuteuliwa
Serikalini ila mpaka ajiuzulu nafasi yake. Rais wa Marekani hana
mamlaka ya kulivunja Bunge. Mfumo huu, unasaidia kila upande
kuweza kufanya kazi zake kwa madhubuti katika kusimamiana na
kuwajibishana. Kenya pia imeamua kufuata mfumo huu ambapo
Mawaziri wamezuiliwa na Katiba kuwa Wabunge1

Pili, Rais ana madaraka ya kupanga na kuamua mishahara na


posho za Wabunge, hivyo kuwa na uwezo wa kutumia fursa hiyo
kama njia ya kushawishi utendaji wa Bunge2
Tatu, Rais anaweza kulivunja Bunge kama ilivoainishwa kwenye
ibara ya 90(2)(a);
(a) Bunge likikataa kupitisha Bajeti iliyopendekezwa na
Serikali;
(b) Likikataa kupitisha Muswada wa sheria ambao Rais
anautaka au Bunge likisisitiza kupitisha muswada
ambao Rais hautaki1

1Ibara ya 152(3) ya Katiba ya Kenya


2 Kifungu cha 19(1) na (2) cha Sheria ya Utawala wa Bunge [The National
Assembly(Administration) Act , CAP 115 [RE 2002].
55
(c) Bunge likikataa kupitisha muswada wa sheria
ambao Rais anaona ni wa muhimu
(d) Kama Bunge limekataa kupitisha hoja ambayo Rais
anaona ni ya msingi na kwamba njia ya kuendelea
kutoka hapo si kuteua Waziri Mkuu mwingine bali ni
kuitisha Uchaguzi Mkuu
(e) Endapo, kutokana na uwiano wa uwakilishi wa
vyama vya siasa katika Bunge, Rais anaona kwamba
hakuna uhalali kwa Serikali iliyopo kuendelea
kuiwapo na wala haiwezekani kuunda Serikali mpya
(f) Kupitia chama chake, kuwafukuza Wabunge
wanaokosoa utendaji wake na hivyo kuhatarisha
nafasi ya chama kuendelea kutawala.

Badala ya Rais kuvunja Bunge na nchi kuingia kwenye gharama za


uchaguzi mwingine, Nchini Namibia, iwapo Rais atakataa kusaini
muswaada wowote uliopitishwa na Bunge kuwa sheria. Jambo hilo
litapelekwa kwa Mahakama ambayo itaamua uhalali wa jambo hilo.
Ikiwa Mahakama itaamua kuwa muswaada uliopitishwa na Bunge
ni halali Rais ataweka saini lakini ikiwa ulipitishwa na robo tatu ya
Wabunge wote. Kama Bunge halikupitishwa na uwingi huo wa
Wabunge, Rais anaweza kuendelea kutokutia saini muswada huo.
Ikiwa hivyo, muswaada huo utahitaji kuthibitishwa na baraza la
Taifa. Ikiwa Mahakama itaona kuwa muswada huo sio halali, Rais
hatalazimika kutia saini2. Nchini Ufaransa, ikiwa Bunge litakataa
kupitisha muswada au kushughulikia jambo ambalo Rais anaona
ni muhimu, jambo hilo litapelekwa kwa wananchi kwa njia ya kura
ya maoni(referedum) na kama ukipita, basi muswada huu unakuwa
sheria3

Nne, Bunge limezuiliwa kushughulikia jambo lolote isipokuwa


kama Rais atapendekeza kupitia kwa Waziri kati ya haya yafuatayo:
Kutoza kodi au kubadilisha kodi kwa namna yeyote isipokuwa
kupunguza; kuagiza kwamba malipo au matumizi ya fedha
yafanywe kupitia Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali au Mfuko
mwingine wa Serikali au kubadili kiwango hicho kwa namna
nyingine isipokuwa kupunguza. Nyingine, ni kuagiza kwamba
malipo au matumizi ya fedha yafanywe kutokana na Mfuko wa

1 Ibara ya 97 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977


2 Ibara ya 64 ya Katiba ya Namibia.
3 Palmer, M.(1997,p. 159), Comparative Politics, F.E. Peacock Publishers, Florida.
56
Hazina ya Serikali au Mfuko mwingine wa Serikali wakati
ikifahamika kwamba fedha iliyomo katika mifuko hiyo
haikupangiwa itolewe kwa ajili ya malipo au matumizi hayo, au
kuagiza kwamba malipo au matumizi yanayofanywa kutokana na
mifuko hiyo yaongezwe. Pia, kufuta au kusamehe deni lolote
linalotakiwa lilipwe kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano. Tofauti
na ilivyo Tanzania, Katiba ya Marekani inatoa madaraka ya
kupanga na kushughulikia masuala ya fedha ikiwemo kutoza kodi
na kushughulikia deni la Taifa kwa Bunge.

Tano, nidhamu ya chama. Tanzania imeiga mfumo wa Kiingereza


wa utendaji wa Bunge (Westminster system) ambapo Wabunge
hutakiwa kupiga kura kulingana na maelekezo ya chama. Kwa njia
hiyo, utendaji wa Wabunge unaegemea zaidi maelekezo ya
mnadhimu wa chama kuliko Spika. Kwa kuwa wote Spika na
Wabunge wanatakiwa kutii maelekezo ya chama wanapopitisha
miswaada na maamuzi mengine ya Bunge. Kwa hiyo ingawa, ibara
ya 100 ya Katiba inasema kuwa Wabunge watakuwa na uhuru wa
maoni na watakuwa na kinga ya kutoadhibiwa kwa wanayoyasema
wakiwa Bungeni, ukweli ni kwamba nidhamu ya chama imekuwa
ikipewa kipaumbele zaidi ya Katiba katika utendaji wa Wabunge1.
Hii inawezekana kuwa ni kwa sababu vyama vimeruhusiwa na
Katiba kuwanyang’anya Wabunge nafasi zao2. Kwa hiyo, vyama
vinakuwa vikwazo kwa Bunge kuweza kuisimamia Serikali na
kumwajibisha Rais kwa sababu kila chama kina tabia ya kulinda
maslahi yake kwa nguvu zao zote.3

Nchini Uingereza ambapo ndio chimbuko la mfumo huu, Uingereza,


Wabunge wanaweza kupingana na msimamo wa chama katika
kupiga kura na kuhamia upande mwingine kati ya chama Tawala
na upande wa upinzani. Utaratibu huo unaitwa crossing the floor,
ambapo Mbunge huhamia upande wa pili kama akitofautiana na
msimamo wa chama chake. Mfano, mwaka 1904 Winston Churchil
alihama kutoka chama chake cha Conservative na kuhamia chama
cha Liberal kabla ya kurudi tena Conservative mwaka 1920. Mwaka

1 Angalia Sitta, S., Slaa, W., &Cheyo, J.M, (2008). Bunge Lenye Meno: A
Parliament with Teeth, for Tanzania. London. African Research Institute
2 Kwa mujibu wa ibara ya 67(2)(e) mtu hatakuwa na sifa ya kuwa Mbunge ikiwa

si mwanachama wa chama cha siasa. Hivyo, mtu akifukuzwa uanachama wa


chama cha siasa anakuwa amekosa sifa ya ama kuchaguliwa kuwa Mbunge au
kundelea kuwa Mbunge
3 Angalia Sitta, S., Slaa, W., & Cheyo, J.M,(2008). Bunge Lenye Meno: A

Parliament with Teeth, for Tanzania. London. African Research Institute pp 27-38
57
2007, Quentin Davies alihama chama cha Conservative na
kuhamia chama chama Labour kwa kutoridhishwa na mwenendo
wa chama chake. Marekani pia, vyama havina mamlaka ya
kumnyang’ang’anya mtu Ubunge kwa kumfukuza uanachama na
hivyo kuwafanya Wabunge kuwajibika zaidi kwa wapiga kura wao
kuliko kwa vyama vyao.

Sita, Rais kuwa na mamlaka ya kufanya uteuzi wa nafasi


mbalimbali kadiri anavyoona yeye. Katika hali hiyo ni rahisi kwa
Rais kutumia mamlaka yake vibaya na itakuwa vigumu kwa Bunge
kumwajibisha. Ili kukabiliana na hali hiyo, Katiba ya Marekani,
kupitia kifungu kinachojulikana kama “kifungu cha Uteuzi”
kinampa mamlaka Rais wa Marekani kuteua viongozi wakuu wa
umma ikiwemo Majaji wa Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufaa,
Mabalozi na viongozi wengine wakuu ambao wametajwa na sheria
mbalimbali za nchi, lakini uteuzi huo lazima uchunguzwe na
kuthibitishwa na Bunge kwa niaba ya wananchi1. Kenya ni
miongoni mwa nchi ambazo Katiba inahitaji uteuzi wa Rais
uthibitishwe na Bunge. Zaidi ya hayo, baadhi ya Katiba za nchi
zinaelekeza kuwa Rais atafanya uteuzi wa nafasi za watendaji
wakuu wa umma kwa kufuata mapendekezo ya Tume za Utumishi.
Nchi zinazofuata mfumo huo ni pamoja na Ghana, Zambia, Uganda
na Ufilipino. Pia, katika baadhi ya nchi Rais amewekewa mipaka
katika kufanya uteuzi. Kwa mfano, katika Katiba ya Kenya, Rais
atateua Mawaziri wasiopungua kumi na nne na wasiozidi 222.
India, Mawaziri wanatakiwa wasizidi asilimia 15 ya Wabunge wote3.
Katiba ya Ghana inataka Rais ateue Mawaziri kati ya 10 na 194.
Katiba ya Ufilipino imemzuia Rais kushika wadhifa mwingine
wowote wa umma utakaosababisha mgongano wa maslahi katika
kutekeleza majukumu yake ya Kirais wakati wote wa utawala wake.
Rais amekatazwa na Katiba kuteua ndugu na jamaa zake kuteuliwa
kushika madaraka katika nafasi za umma ikiwemo mashirika ya
Kiserikali5.

Mahakama ina mamlaka ya kudhibiti madaraka ya Rais akienda


kinyume na misingi ya Katiba na sheria za nchi. Msingi wa
mamlaka ya Mahakama ulielezwa vizuri na Jaji Mkuu wa Zamani

1 Ibara ya II, kifungu cha 2(2) ya Marekani.


2 Ibara ya 152(1)(d) cha Katiba ya Kenya.
3 Ibara ya 75 ya Katiba ya India.
4 Ibar aya 54 Katiba ya Ghana ya Mwaka 1992.
5 Kifungu cha 13 cha Katiba ya Ufilipino.
58
wa Marekani, John Marshall, katika kesi ya Marbury v Madison,
(1803), kuwa Kanuni ya Msingi ni kwa Serikali kuwajibika kwa
Mahakama kwa tuhuma za kushindwa kutii sheria ya Bunge na
msingi ya sheria mama kiasi cha kusababisha hasara ya haki za
watu. Na kwamba, ni jukumu la Mahakama kutamka kama
maamuzi ya afisa wa Serikali au Bunge au taasisi nyingine
yamefanyika kulingana na matakwa ya Katiba, kama siyo, ni
jukumu la Mahakama kutangaza uamuzi huo kuwa ni batili1.
Mahakama zinahitaji uhuru wa kutosha ili ziweze kutimiza wajibu
wao wa kuleta uwajibikaji wa kikatiba na utawala unaozingatia
sheria. Uhuru kutoka kwa mamlaka ya Rais ni muhimu ili
Mahakama ifanye kazi bila woga au upendeleo katika kusimamia
haki.

5.1.5 Hali halisi ilivyo

Ibara ya 107A (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,


1977, inasema kuwa Mamlaka yenye kauli ya mwisho ya utoaji
haki katika Jamhuri ya Muungano itakuwa ni ya Mahakama.”
Ibara ya 107A ya Katiba inatoa mamlaka kwa Mahakama kutoa
uamuzi wa mashauri dhidi ya Serikali kwa Kutumia sheria zilizopo
ikiwa pamoja na Marejeo ya Maamuzi (Judicial Review) maamuzi ya
Serikali ili kubatilisha uamuzi wa Serikali, au kuizuia Serikali
isifanye uamuzi fulani au kuilazimisha Serikali kutekeleza
majukumu yake kama inakuwa inasita.

Ibara ya 108 imetamka kuwa Mahakama Kuu itakuwa na uwezo wa


kutekeleza shughuli yoyote ambayo kwa mujibu wa mila za kisheria
zinazotumika Tanzania shughuli ya aina hiyo kwa kawaida
hutekelezwa na Mahakama Kuu. Mojawapo wa mila hizo ni
mamlaka ya kiasili kwa Mahakama kuhakikisha taasisi za utendaji
zinafanya kazi ndani ya mipaka waliyowekewa kikatiba. Tanzania
imerithi kanuni hii kutoka jumuiya ya Madola na ni sehemu
sehemu ya sheria za nchi .2 Ibara ya 108 inatoa mamlaka mapana
ya Mahakama Kuu kusikiliza shauri lolote ambalo halijatajwa kuwa
mahususi kwa Mahakama ya ngazi fulani.

1 Soma Thomas E. Patterson, (2004), We the People: A Concise Introduction to


American Politics, 5th edition, McGraw Hill, New York, p. 56.
2 kifungu cha 2(3) cha Judicature and Application of Laws Act, Cap 358 [RE
2002].
59
Mamlaka ya Mahakama kumwajibisha Rais yanaweza kuathiriwa
na mamlaka ya Rais kuteua Majaji na watendaji wakuu wa
Mahakama. Katiba ya sasa inatoa mamlaka ya kuteua watendaji
wote wakuu wa Mahakama kama ilivyotangulia kuonyeshwa na
kuonekana zaidi katika nyongeza namba 1. Rais anaweza pia
kuwaondoa watendaji wa Mahakama. Kwa mfano, Rais anaweza
kumuondoa Jaji Mkuu na Jaji Kiongozi kadiri anavyotaka kwa
kuteua watu wengine kushika nafasi zao. Ukosefu wa uhakika wa
usalama kwenye nafasi zao kunaweza kuwafanya viongozi hao
kuepuka kufanya chochote ambacho hakimfurahishi Rais, na hivyo
kuathiri uhuru wa Mahakama katika kusimamia madaraka ya Rais
na Serikali yake. Rais pia ana madaraka ya kuwaondoa Majaji
madarakani kwa mchakato ambao yeye mwenyewe anausimamia.
Rais ndio huunda Tume ya kuchunguza tuhuma dhidi ya Jaji na
Tume hiyo ndio hupendekeza uamuzi wa kuchukuliwa na Rais. Ili
kuhakikisha kuwa Mahakama ina watendaji wenye sifa stahili,
kama ilivyoonyeshwa juu, baadhi ya nchi zimeweka utaratibu
kuwa uteuzi wa watendaji na nidhamu ya Majaji na watendaji wa
Mahakama usimamiwe na Tume ya Utumishi wa Mahakama na
uthibitishwe na Bunge. Katiba ya Uganda ya Mwaka 1995
inatamka kuwa Jaji Mkuu, Naibu Jaji Mkuu, Jaji Kiongozi, Majaji
wa Makama ya juu (Supreme Court), Majaji wa Mahakama ya Rufaa
(The Court of Appeal) na Majaji wa Mahakama Kuu watateuliwa na
Rais kwa ushauri wa Tume ya Utumishi wa Mahakama na
kuthibitishwa na Bunge.1

Tume ya Utumishi wa Mahakama Tanzania imeundwa na wateule


wa Rais kwa nafasi zao mbalimbali. Kupitia nafasi zao zinazowapa
sifa ya kuwa wajumbe wa Tume, Rais anaweza kuwandoa
madarakani. Hali hii inaweza kuathiri uhuru wa Mahakama katika
kuisimamia Serikali na kudhibiti madaraka ya Rais. Katiba ya
Uganda inatoa mamlaka kuteua wajumbe wa Tume ya Utumishi wa
Mahakama kwa Rais lakini lazima wathibitishwe na Bunge.
Wajumbe wa Tume hiyo ni pamoja na; mwenyekiti na makamu
wake ambao ni watu wenye sifa ya kuwa Jaji wa Mahakama ya
Juu, lakini asiwe Jaji Mkuu au Naibu wake au Jaji Kiongozi; mtu
mmoja atakayependekezwa na Tume ya Utumishi wa Umma;
Mawakili wawili watakaoteuliwa na Uganda Law Society; Jaji
mmoja wa Mahakama ya Juu atakayeteuliwa na Rais kwa
kushauriana na Majaji wa Mahakama ya Juu, Majaji wa

1 Ibara ya 142 ya Katiba ya Uganda ya Mwaka 1995.


60
Mahakama ya Rufaa na Majaji wa Mahakama Kuu; wajumbe wawili
ambao sio wanasheria ambao watateuliwa na Rais kutoka kwa
umma; na Mwanasheria Mkuu wa Serikali atakayeingia kwa nafasi
yake1.

Pia, baadhi ya nchi zimetamka bayana kuwa mamlaka ya


Mahakama kufanya marejeo (Judicial Review) ya maamuzi ya
Serikali na Bunge. Katiba ya India imeweka wazi kuwa jukumu
kubwa la Mahakama ya Juu (Supreme Court) ni kuhakikisha kuwa
sheria za nchi na utekelezaji wake viko ndani ya mipaka ya Katiba
ya nchi. Mahakama ya Juu hufanya kazi kama mlinzi wa haki za
raia dhidi ya kuingiliwa na Serikali2. Pia, Katiba ya Kenya imeweka
bayana mamlaka ya Mahakama kufanya marejeo ya sheria au
utekelezaji wake kama vinaendana na Katiba ya nchi3

5.2 MAPENDEKEZO
Ili kuongeza uwajibikaji na kuongeza uthibiti wa madaraka ya Rais
mapendekezo inapendekezwa;

 Idadi ya wateule wa Rais ipunguzwe ili ibakie orodha fupi ya


viongozi na maofisa wa umma wakiwemo Mawaziri, Mabalozi,
wasaidizi wake, na watendaji wengine watakao wajibika
kwake moja kwa moja. Watendaji na viongozi wengine
wapatikane kwa utaratibu wa kuajiriwa, kupandishwa vyeo
au kuteuliwa na mamlaka na vyombo vingine kadiri
itakavyofaa;

 Kuwe na utaratibu wa Bunge kuidhinisha wateule wa Rais


kwa nafasi mbalimbali;

 kuwe na utaratibu wa Rais kufanya uteuzi wa maofisa


waandamizi wa umma kulingana na mapendekezo ya vyombo
mbalimbali vilivyoanishwa kikatiba kama vile Tume za
Utumishi unafaa kuigwa. Utaratibu huo zaidi ya kupunguza
mianya ya kufanyika uteuzi usiozingatia sifa stahili, pia
unaongeza uwezekano mkubwa wa kupata watendaji walio
bora;

1 Ibara ya 146 ya Katiba ya Uganda.


2Angalia Kriger, Joel & Joseph, William ed.(2007, pp.277-278),Introduction to
Comparative Politics, Houghton Mifflin Company, Boston.
3 Ibara ya 165 ya Katiba ya Kenya.

61
 Mawaziri wasitokane na Wabunge ili kuongeza urari; ili
Bunge liweze kufanya kazi ya kumsimamia Rais ipasavyo.
Mawaziri wasipokuwa Wabunge kutaondoa mgongano wa
maslahi unaowakumba Mawaziri na Wabunge kati ya wajibu
wakiBunge na wajibu wa kiuWaziri. Mawaziri pia wataweza
kutumia muda wao na nguvu zao kwenye wizara zao
wakiondolewa mzigo wakushughulikia majimbo yao. Pia,
Mawaziri wasipokuwa Wabunge itampa Rais wigo mpana wa
kuteua Mawaziri wenye sifa zinazotakiwa. Mawaziri
watakuwa wanakutana na Wabunge kwenye kamati zao na
mbele ya Bunge kueleza sera zao na kujibu maswali ya
Wabunge;

 Sambamba na hilo hapo juu, wabunge wasiruhusiwe


kuteuliwa kushika nafasi za mkuu a mkoa na mkuu wa
wilaya;

 Rais asiwe na uwezo wa kuvunja Bunge pale Bunge


linaposhindwa kupitisha muswada ambao Rais
anaupendelea. Badala yake, swala husika lipelekwe
Mahakamani au kwenye kura za maoni(referendum) kadiri
itakavyofaa;

 Kusiwe na Wabunge wa kuteuliwa na Rais maana uwepo wao


unaongeza ushawishi wa Rais katika utendaji wa Bunge na
hivyo kushindwa kuathiri uwezo wa Bunge kumwajibisha
Rais. Hoja hii itakuwa na nguvu zaidi kama Mawaziri
watakuwa hawatokani na Wabunge maana moja ya malengo
ya kuwa na nafasi hii ni kumwezesha Rais kuwapata
wananchi wenye uwezo na sifa za kuwa Mawaziri lakini
hakuingia Bungeni kwa njia ya kuchaguliwa;

 Utamaduni wa nidhamu ya chama usiruhusiwe kuzuia


uhuru wa Wabunge kufanya kazi za kiBunge kama
ilivyowekwa kikatiba. Utaratibu unaojulikana kama crossing
the floor, yaani kupiga kura kulingana na upande anaona
unafaa bila kupoteza nafasi yake ya Ubunge;

62
 Mahakama ziwe na uwezo wa kusikiliza malalamiko dhidi ya
uchaguzi wa Rais. Hata hivyo, ni muhimu kuwe na ukomo wa
kusikiliza shauri la namna hiyo;

 Wabunge wasizuiliwe kuanzisha muswada inayohusiana na


masuala ya fedha na kodi au jambo lolote isipokuwa yale
yanayogusa maslahi yao binafsi.

63
SEHEMU YA SITA

6.1 KINGA YA RAIS KUSHTAKIWA


6.1.1 Hoja

Kuna maoni kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania


aondolewe kinga ya kushtakiwa. Wanaotoa hoja hii wanatoa
sababu kadha wa kadha. Baadhi ya sababu hizo ni kama ifuatavyo.
Kwanza, Rais anaweza kufuja mali ya umma na ni vigumu
kumwajibisha kwa sababu ana kinga. Pili, kuna watu wanaotoa
hoja kuwa binadamu wote ni sawa, hivyo Rais anastahili
kushtakiwa kama wananchi wengine. Tatu, katika nchi ya
kidemokrasia na inayoongozwa na utawala wa sheria kama
Tanzania haifai kuwa na utaratibu wa mtu au watu fulani kupewa
kinga ya kuwajibishwa pindi wanapokosea.

6.1.2 Kinga ya kushtakiwa

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imempa Rais kinga


ya kushtakiwa. Ibara ya 46 inaeleza;

(1) Wakati wote Rais atakapokuwa bado ameshika


madaraka yake kwa mujibu wa Katiba hii,
itakuwa ni marufuku kumshtaki au kuendesha
mashtaka ya aina yoyote juu yake Mahakamani
kwa ajili ya kosa lolote la jinai.

(2) Wakati wote Rais atakapokuwa bado ameshika


madaraka yake kwa mujibu wa Katiba hii,
haitaruhusiwa kufungua Mahakamani shauri
kuhusu jambo lolote alilolitenda au alilokosa
kulitenda yeye binafsi kama raia wa kawaida
ama kabla au baada ya kushika madaraka ya
Rais, ila tu kama angalau siku thelathini kabla
ya shauri kufunguliwa Mahakamani, Rais
atapewa au kutumiwa taarifa ya madai kwa
64
maandishi ili kufuata utaratibu uliowekwa kwa
mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge, na
taarifa hiyo ikiwa inatoa maelezo kuhusu
chanzo cha shauri hilo, kiini cha madai
yenyewe, jina lake na anwani ya mahali
anapoishi huyo mdai na jambo hasa analodai.

(3) Isipokuwa kama ataacha kushika madaraka ya


Rais kutokana na masharti ya ibara ya 46A(10),
itakuwa ni marufuku kumshtaki au kufungua
Mahakamani shauri lolote la jinai au la kumdai
mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais
baada ya kuacha madaraka hayo kutokana na
jambo lolote alilofanya yeye kama Rais wakati
alipokuwa bado anashika madaraka ya Rais
kwa mujibu wa Katiba hii.

Ibara ya 46 (1) inatoa kinga kwa Rais kutoshtakiwa kwa kosa la


jinai wakati akiwa madarakani. Hivyo, wakati wote ule ambao Rais
atakuwa ameshika madaraka itakuwa ni marufuku kumfungulia
kesi ya jinai.

Ibara ya 46 (2) inatoa kinga ya ujumla ya Rais kutofunguliwa


shauri la madai wakati akiwa madarakani. Hata hivyo, mtu yeyote
amepewa mamlaka na ibara hii haki ya kufungua shauri la madai
dhidi ya Rais endapo atatoa taarifa (notisi) siku thelathini kabla ya
kufungua shauri la madai dhidi ya Rais. Hivyo, mtu akitekeleza
masharti husika anaweza kufungua shauri la madai dhidi ya Rais
Mahakama Kuu.1 Mtu anayetaka kufungua shauri kama hilo
inabidi aambatanishe notisi na hati ya madai (plaint)2 na aipeleke
kwa rejesta kwa Katibu Mkuu kiongozi au Katibu wa Rais.3 Hata
hivyo, haki ya kumfungulia Rais shauri la madai imezungumziwa
pia na Sheria ya Masuala ya Urais (The Presidential Affairs Act4).
Sheria hii inasema endapo Mahakama itamwona Rais anawajibika
katika kesi iliyofunguliwa dhidi yake itatoa “hukumu tamko”
(declaratory judgment) tu.5 Hii ina maana Mahakama haiwezi

1 Kifungu cha 5 cha Sheria ya Masuala ya Urais, Sura ya 9.


2 Kama ilivyo juu, Kifungu cha 6 (1) (a).
3 Kama ilivyo juu, Kifungu cha 6 (1) (b).
4 Cap 9 [RE 2002].
5 Kifungu cha 6 (3) cha Sheria ya Masuala ya Urais, Sura ya 9.
65
kumwamuru Rais kutenda kitu fulani, mfano kulipa. Ni hiyari ya
Rais mwenyewe.

Ibara ya 46(3) inamlinda Rais mstaafu. Kwa mujibu wa ibara hii,


Rais mstaafu hatofunguliwa mashtaka ya jinai au shauri la madai
kuhusiana na jambo lolote alilolifanya alipokuwa madarakani.
Ibara hii haiko wazi kama inamlinda Rais mstaafu hata kwa
mambo ya kibinafsi aliyoyafanya wakati akiwa madarakani.

6.1.3 Sheria ya Masuala ya Kirais (The Presidential Affairs Act,


Cap 9 [RE 2002])

Sheria ya Masuala ya Kirais (The Presidential Affairs Act1) imepanua


wingo wa kinga anayopewa Rais. Kifungu cha 8 cha sheria hii
kinatoa kinga nyingi kwa Rais. Kwanza, Rais hawezi kukamatwa.2
Pili, Mahakama haina ruhusa kutoa hati (kama hati ya kukamatwa,
hati ya wito, n.k.) yoyote inayoelekezwa kwa Rais.3 Tatu, Mahakama
haina ruhusa ya kumuita au kumtaka Rais yeye mwenyewe afike
Mahakamani au amlete mtu fulani au awasilishe kitu fulani.4 Nne,
endapo kuna mtu ameiomba Mahakama kumuita Rais au
kumwamuru amlete mtu fulani au awasilishe kitu fulani,
Mahakama haitakiwi kutoa amri yoyote kwa Rais kuhusiana na
maombi hayo isipokuwa itamjulisha Rais kuwa kuna maombi ya
namna hiyo.5

1 Cap 9 [RE 2002].


2 Kama ilivyo juu, Kifungu cha 8 (1).
3 Kama ilivyo juu, Kifungu cha 8 (2) (a).
4 Kama ilivyo juu, Kifungu cha 8 (2) (b).
5 Kama ilivyo juu, Kifungu cha 8 (3).
66
6.1.4 Wigo wa Kinga

Ni vizuri kufafanua wigo (scope) wa kinga ya kushtakiwa. Kinga


iliyowekwa kwenye Katiba inamhusu Rais yeye mwenyewe. Katiba
inazuia kumshtaki Rais yeye mwenyewe na siyo kwamba Serikali
haiwezi kufunguliwa madai kuhusiana na maamuzi ya Rais kama
kiongozi wa Serikali. Shauri la Tumukunde dhidi ya Mwanasheria
Mkuu na Mwingine [2005] 2 EA 291 lililoamuliwa na Mahakama ya
Kikatiba ya Uganda linatoa ufafanuzi mzuri. Tumukunde, akiwa
mwanajeshi katika Jeshi la Uganda, alikuwa Mbunge
anayewakilisha Jeshi la Uganda (UPDF). Aliongea maneno ambayo
hayakumfurahisha Rais ambaye pia ni Amiri-Jeshi-Mkuu. Aliitwa
na kuamriwa amwandikie spika barua ya kujiuzulu Ubunge.
Alitekeleza amri hiyo. Baadaye alikamatwa na kufunguliwa
mashtaka ya kijeshi. Tumukunde alifungua kesi dhidi ya
Mwanasheria Mkuu wa Uganda akiitaka Mahakama itoe tamko
kuwa vitendo vya Amiri-Jeshi-Mkuu kumlazimisha Mbunge
kujiuzulu, kumkamata na kumfungulia mashtaka kuhusiana na
alichoongea Bungeni vilikuwa ni kinyume cha Katiba ya nchi hiyo.
Wakili wa Serikali (Bw Tibaruha) alitoa hoja kuwa Katiba inazuia
Rais kushtakiwa. Wakili wa Tumukunde (Bw Oscar Kambona)
alipinga hoja hiyo na kusema Rais hayupo juu ya Katiba na
kwamba kinga ya Rais inamlinda yeye mwenyewe (his person).
Aidha, alisema Rais hayuko katika upande mmojawapo wa shauri
hilo na kwamba hakuitwa Mahakamani kutoa ushahidi.

Mahakama ilikubaliana na Bw Kambona kuwa Katiba inazuia tu


“kumburuza Rais mwenyewe” na kumpeleka Mahakamani na
kwamba maamuzi yake yanaweza kuhojiwa Mahakamani. Kwa
namna ya obita dictum, Mahakama ilisema endapo Katiba
ingekuwa imezuia maamuzi ya Rais kuhojiwa Mahakamani basi
hakutakuwa na haja ya kuwa na Mahakama ya Kikatiba kwa
sababu Mawaziri na maofisa wengine wa Serikali wanafanya kazi
kwa niaba ya Rais. Hivyo, kinga ya Rais inamlinda Rais
asikamatwe au asifunguliwe kesi ambayo atatakiwa kulipa fidia
yeye mwenyewe. Mathalan, Rais akiamua mtu awekwe kizuizini bila
kufuata sheria Katiba haimzuii muathirika kwenda Mahakamani
na kuiomba Mahakama kutamka kuwa kitendo hicho ni kinyume
cha sheria na kutoa amri aachiwe. Kuna mashauri mengi ambayo
67
Mahakama Kuu iliamua kuwa uamuzi wa Rais ni kinyume cha
sheria: Patman Garments Industries Ltd v Tanzania Manufacturers
Ltd. [1981] TLR 303; James Funke Gwagilo v Attorney General
[1994] TLR 73; Permanent Secretary (Establishments) and another v
Hilal Hamed Rashid and four others [2005] TLR 121; na Said Juma
Muslim Shekimweri v Attorney-General [1997] TLR 3.

6.1.5 Mantiki ya Kinga

Sheria za kimataifa (international law) na sheria za nchi (domestic


law) zinatambua kuwa viongozi wa nchi wana kinga ya kushtakiwa
kama ilivyo wanadiplomasia. Katika sheria za Mataifa, kila nchi
inachukuliwa kuwa ni huru (sovereign) hivyo kiongozi wake naye ni
huru (sovereign) au mwanadiplomasia kutoka nchi hiyo kwa
kawaida hawezi kukamatwa au kushtakiwa na Serikali ya nchi
nyingine.1 Hata hivyo, tutaangalia zaidi kinga anayopewa kiongozi
wa nchi katika Katiba ya nchi au sheria za ndani na siyo ile
inayotambuliwa katika sheria za kimataifa.

Ni kwa nini kiongozi wa nchi anapewa kinga ya Kikatiba ya


kutoshtakiwa? Hazel Fox na wenzake2, wanamnukuu Watts3
aliyesema chanzo hasa cha kinga kwa kiongozi wa nchi katika nchi
za Ulaya ni mfumo wa kifalme (monarchy). Katika mfumo huo nchi
ilichukuliwa kuwa ni mali ya Mfalme. Serikali na vyombo vyote vya
Kiserikali vilichukuliwa kuwa ni vyake na hivyo hakukuwa na mtu
au chombo kilichokuwa na mamlaka ya kumhoji “mwenye nchi.”
Watawala wetu wa zamani, Waingereza, husema kuwa “Mfalme
hawezi kutenda kosa” (the king can do no wrong)4 msemo ambao

1 Peter Evans Bass, “Ex-Head of State Immunity: A Proposed Statutory Tool of


Foreign Policy”, The Yale Law Journal, Vol.97, No 2 (Dec., 1987), pp.299-319,
p.300.
2 Hazel Fox, Colin Warbrick and Dominic McGoldrick, “The Future of Former

Head of State Immunity after ex parte Pinochet”, in The International and


Comparative Law Quarterly, Vol. 48, No. 4 (Oct., 1999), pp. 937-949 p.939.
3 Sir Arthur Watts, "The Legal Position in International Law of Heads of States,

Heads of Governments and Foreign Ministers" (1994) 247 Hague Recueil 9, at


p.52.
4 Herbert Barry anamnukuu mwandishi wa Kiingereza, Blackstone, aliyeandika,

"Besides the attribute of sovereignty, the law also ascribes to the King in his
political capacity absolute perfection. The King can do no wrong. "The King,
moreover, is not only incapable of doing wrong, but even of thinking wrong; he
can never mean to do an improper thing. In him is no folly or weakness."[Herbert
Barry, “The King Can Do No Wrong”, in Virginia Law Review, Vol. 11, No. 5 (Mar.,
1925), pp. 349-371, p.353]. Angalia pia Erwin Chemerinsky, “Against Sovereign
68
msingi wake, kama anavyosema Herbert Barry, ni kuwa Mfalme
siyo binadamu wa kawaida—hakuwa na udhaifu wowote wa
kibinadamu.1 Hali kadhalika, ilisemwa kuwa “Mfalme hawezi
kushtakiwa au kulazimishwa kujibu swali katika Mahakama zake
mwenyewe.”2 Hivyo, Mfalme alikuwa juu ya Mahakama na sheria.3
Kwa ufupi, kinga ya kushtakiwa kwa kiongozi wa nchi yenye
mfumo huo ilitokana na misingi hii ya utawala wa kifalme na nafasi
ya kipekee ambayo mfalme alipewa katika jamii ile.

Kutokana na historia na msingi huu wa kinga kwa kiongozi wa


nchi sheria zenye asili ya kiingereza (common law) hazitoi
mwongozo mzuri kuhusiana na dhana ya kinga ya Rais.4 Taasisi ya
Urais (presidency) ni kitu kigeni katika utamaduni wao. Taasisi ya
Urais ilianzishwa na nchi zingine kama Ufaransa na Marekani
kama mbadala wa mfumo wa kifalme. Katika mfumo wa Urais
kiongozi wa nchi siyo huru (sovereign) kama ilivyo kwa Mfalme;
wananchi ndiyo huru na Rais ni mtumishi wao. Kwa maneno
mengine, katika mfumo wa utawala wa kijamhuri (Republican
System of Government) wananchi ndiyo Wafalme. Kwa msingi huo
Rais hapewi kinga kwa sababu nchi ni mali yake au kwa kuwa yeye
ni tofauti na binadamu wengine, la hasha. Bali anapewa kinga kwa
sababu asili ya kazi yake inahitaji kinga kama itakavyoelezwa hapa
chini.

Katika shauri la Ferri v Ackerman, 444 U.S. 193 (1979) Mahakama


ya Juu ya Marekani (The Supreme Court) ilisema kuwa matakwa ya
jamii katika kuwapa kinga watumishi wa umma katika utendaji

Immunity”, in Stanford Law Review, Vol. 53, No. 5, Symposium: Shifting the
Balance of Power? The Supreme Court, Federalism, and State Sovereign
Immunity (May, 2001), pp. 1201-1224, pp.1201-1202.
1 Herbert Barry, “The King Can Do No Wrong”, in Virginia Law Review, Vol. 11,

No. 5 (Mar., 1925), pp. 349-371, p.354.


2 F. Pollock & F. Maitland, (1909), History of English Law , 2nd edtn, Liberty Fund,

Indianapolis, p. 518.
3 Mwanasheria maarufu wa Kiingereza katika karne ya 16, Sir Edward Coke,

akiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, anakumbukwa kwa ujasiri wake siku


moja alipokuwa akiongea na Mfalme James I na kumwambia Mfalme huyo
alikuwa chini ya sheria. Mfalme alikasirika sana kuambiwa yupo chini ya sheria
na kusema maneno hayo yalikuwa ni maneno ya kihaini. [Angalia Roland G.
Usher, “James I and Sir Edward Coke”, in The English Historical Review”, Vol.
18, No. 72 (Oct., 1903), pp. 664-675, p.664].
4 Katika Shauri la Nixon v Fitzgerald, 457 U.S. 731 (1982) Mahakama ya Juu ya

Marekani (Supreme Court) ilisema kuwa wakati sheria za Kiingereza (common


law) zikikua hakukuwa na taasisi ya Urais. Hivyo sheria hizo hazisaidii sana
Mahakama kuhusiana na taasisi ya Urais.
69
wao wa kazi ni kutaka watumishi hao waweze kutekeleza
majukumu yao bila upendeleo na woga. Ni kwamba kinga ina lengo
la kuzuia vitisho vya kushtakiwa ambavyo wanaweza kukumbana
navyo na ambayo vitakinzana na utendaji wao wa kazi kwa
utaratibu unaofaa.1

Mahakama hiyo ilibidi iamue mgogoro mwingine uliohusu kinga ya


Rais katika shauri la Nixon v Fitzgerald, 457 U.S. 731 (1982).
Fitzgerald, alikuwa mfanyakazi katika Jeshi la Anga la Marekani.
Alifukuzwa kazi na kuamua kufungua shauri la madai dhidi ya
Rais mstaafu, Richard Nixon. Kabla ya hapo Fitzgerald aliieleza
kamati ya Bunge matatizo ya sehemu yake ya kazi, kitu ambacho
hakikuwafurahisha wakuu wake wa kazi. Baadaye kitengo
alichokuwa akikiongoza Fitzgerald kilifutwa na yeye kuachwa bila
kazi. Tukio hilo lilizua mjadala mkubwa kwenye vyombo vya habari.
Nixon alipoingia madarakani aliahidi kulishughulikia suala la ofisa
huyo. Hata hivyo, baadhi ya maofisa ndani ya Ikulu hawakutaka
Fitzgerald arudishwe kazini haraka. Katika dokezo moja lililovuja,
mshauri wa Rais alimshauri Nixon kuwa Fitzgerald ni mtaalamu
mzuri lakini ana tatizo la utii na kwamba ni vizuri aachwe ili “damu
imtoke kwa muda” (“We should let him bleed, for a while at least”).
Alimaanisha aachwe “ataabike” kwanza kabla ya kurudishwa
kazini. Baada ya hapo hakurudishwa na akaamua kulalamika
hadharani.

Suala ambalo Mahakama ilijielekeza ni kama Rais mstaafu


anaweza kushtakiwa kwa maamuzi aliyoyafanya akiwa madarakani
na wigo wa kinga yenyewe. Iliamua kuwa Rais mstaafu alistahili
“kinga kamilifu” (absolute immunity). Hii maana yake ni kuwa
alikuwa na kinga hata kwa maamuzi aliyoyafanya kwa “nia mbaya.”
Ikasema pia kinga inatolewa kwa sababu ya ofisi ya kipekee ya ofisi
ya Rais katika utamaduni wa Kikatiba wa mgawanyo wa madaraka
na kuungwa mkono na historia yao.2 Ilieleza kuwa “kinga kamilifu”

1 Tafsiri kutoka kwenye maneno haya: “The societal interest in providing such
public officials with the maximum ability to deal fearlessly and impartially with
the public at large has long been recognized as an acceptable justification for
official immunity. The point of immunity for such officials is to forestall an
atmosphere of intimidation that would conflict with their resolve to perform their
designated functions in a principled fashion.”
2 Hii ni tafsiri toka maneno haya: “we hold that petitioner, as a former President

of the United States, is entitled to absolute immunity from damages liability


predicated on his official acts. We consider this immunity a functionally
70
haitoliacha Taifa bila kinga yoyote dhidi ya vitendo visivyo vya
kimaadili vya Rais kwa sababu kuna utaratibu wa Rais kuondolewa
na Bunge (impeachment), kuna vyombo vya habari na Bunge
(Congress) ambayo humwangalia Rais kwa ukaribu sana. Pia
ilisemwa kuwa kuna vichocheo vya Rais kutovunja maadili kama
vile kutaka kuchaguliwa tena, kulinda heshima yake na kuwa na
nafasi fulani katika historia ya nchi.

Vile vile, Mahakama ilieleza sababu zingine kwanini Rais anahitaji


kinga. Kwanza, kutokana na umuhimu wa ofisi yake Rais akianza
kufunguliwa mashtaka ya madai mengi na kutumia muda wake
kujitetea kuna hatari ya kazi za Serikali kukwama au kushindwa
kutekeleza majukumu yake ipasavyo. Pili, kuna matakwa ya umma
kuwapa watumishi wa umma uwezo kamili wa kufanya kazi zao
bila woga na upendeleo. Tatu, kutokana na asili ya kazi zake,
kuruhusu Rais kufunguliwa madai kunaweza kuwafanya watu
wengi kufungua mashauri dhidi yake. Nne, wakati mwingine
matakwa ya umma ya kutaka kuboresha utendaji wa Serikali
inabidi yapewe kipaumbele kuliko haki ya mtu mmoja mmoja
kupata fidia.

Katika shauri lingine, Clinton v Jones (95-1853), 520 U.S. 681


(1997), Rais Bill Clinton alitaka Mahakama imzuie mwanamke,
Paula Corbin Jones, kufungua kesi ya madai dhidi yake. Paula
Jones alidai kudhalilishwa na Rais Clinton ambaye “alimtongoza
kwa namna ya kuchukiza” ("abhorrent sexual advances”) ndani ya
chumba kimojawapo katika hoteli moja lakini yeye (Paula) alikataa.
Na kwamba baadaye alinyanyaswa na kubadilishiwa kazi na
uongozi wa hoteli hiyo kwa sababu ya kumkataa Mheshmiwa
Gavana. Wakati huo Rais Clinton alikuwa Gavana wa Jimbo la
Arkansas, yaani kabla hajawa Rais. Mahakama ilitakiwa kuamua
kama Rais aliye madarakani anaweza kufunguliwa shauri la madai.
Iliamua kuwa kinga anayopewa mtumishi wa umma inahusu kazi
zake za kiofisi na wala siyo matendo yake binafsi.1 Vilevile,

mandated incident of the President's unique office, rooted in the constitutional


tradition of the separation of powers and supported by our history.”
1 Haya ndiyo maneno halisi ya Mahakama: “The principal rationale for affording

certain public servants immunity from suits for money damages arising out of
their official acts is inapplicable to unofficial conduct. In cases involving
prosecutors, legislators, and judges we have repeatedly explained that the
immunity serves the public interest in enabling such officials to perform their
designated functions effectively without fear that a particular decision may give
rise to personal liability.”
71
Mahakama iliamua kuwa Rais kushtakiwa Mahakamani au kupewa
amri na Mahakama haina maana ya kuingilia “msingi wa
mgawanyo wa mamlaka” (the doctrine of separation of powers)
ambao ni moja ya misingi muhimu katika Katiba ya Marekani.

Katika shauri la Tumukunde dhidi ya Mwanasheria Mkuu na


Mwingine [2005] 2 EA 291, Mahakama ya Kikatiba ya Uganda
ilisema kuwa Rais ana madaraka muhimu na majukumu mengi.
Kwa hiyo ni matakwa ya umma (public interest) Rais apewe kinga
ya kushtakiwa ili aweze kutumia muda wake katika kutekeleza
majukumu yake mengi aliyopewa na Katiba. Vile vile Mahakama
iliamua kuwa Katiba ya Uganda imempa Rais wa nchi hiyo kinga
kamilifu (absolute immunity) kuhusiana na mambo yote
yanayohusiana na kazi yake.

6.1.6 Kinga Kamilifu (absolute immunity) na Kinga yenye


Ukomo (Restrictive Immunity)

Kama ilivyoelezwa hapo juu kwa kawaida viongozi wa nchi


wanapewa kinga kamilifu (absolute immunity). Pia kama
ilivyokwisha kuelezwa, kinga hii ina maana kiongozi wa nchi
anapewa kinga kuhusiana na maamuzi yake yote, akiwa kiongozi,
hata kama ni mengine yalikuwa yanavunja sheria au maamuzi
anayoyafanya kwa nia mbaya (malicious decisions). Huko Marekani
kinga ya namna hii inahalalishwa kwa misingi ifuatayo. Kwanza,
kinga kamilifu inamwondolea Rais woga wa kushtakiwa au
kuwajibishwa kutokana na maamuzi yake mengi na hivyo
kushindwa kufanya kazi yake sawasawa. Pili, Bunge (Congress)
linao uwezo wa kumwondoa kwa utaratibu wa kumshtaki Bungeni
(impeachment). Tatu, wanasema kuwa Rais wao anamulikwa sana
na vyombo vya habari. Na mwisho, wanasema kuwa Marais wao
wanaogopa kukosea au kuvunja sheria kutokana na woga wa
kushusha hadhi zao na vilevile wanapenda kupata nafasi nzuri
katika historia ya nchi yao. Lakini uzoefu umeonyesha kuwa
Marais wengi wa Marekani wamevunja sheria na kutumia
madaraka yao vibaya.1

1 Katika kashfa ya watergate watu waliohusishwa na Rais Richard Nixon,


walienda kuvunja ofisi ya chama cha kidemokrasia (the Democratic Party) usiku
wa tarehe 17 Juni 1972 na kuchukua nyaraka. Rais alijaribu kukataa kutoa
vielelezo na ilielekea kuwe angeondolewa madarakani na Bunge na hivyo
alijiuzulu tarehe 9 Agosti 1974. [Anaglia Donald A. Ritchie, “Investigating the
Watergate Scandal” in OAH Magazine of History, Vol. 12, No. 4, Congressional
72
Hata hivyo, maoni ya sasa yana mwelekeo wa kutaka kuachana na
kinga ya namna hii, yaani “kinga kamilifu” (absolute immunity).
Baadala yake “kinga yenye ukomo” (restrictive immunity)
inapendekezwa. Suala hili lilijadiliwa katika mashauri mawili dhidi
ya Pinotchet {Reg. v Bow Street Magistrate, ex parte Pinochet [1998]3
W.L.R.1 456 (itaitwa Pinochet Na. 1) na Reg. v Bow Street
Magistrate, exparte Pinochet (No. 3) [1999] 2 W.L.R. 827 (itaitwa
Pinochet Na. 3)}. kulikuwa pia na shauri la Pinochet Na. 2 ambalo
liliongelea suala tofauti la Jaji mwenye maslahi fulani kushiriki
katika maamuzi. Kwa ufupi, Jenerali Agusto Pinochet alikuwa
Mkuu wa Jeshi la Chile. Mwaka 1973 alimpindua Rais Salvador
Allende na kushika madaraka hadi mwaka 1990. Inasemekana
kuwa katika uongozi wake Jenerali Pinochet aliua watu wengi sana.
Wapinzani wake wa kisiasa, wanafunzi na wengineo walikuwa
wakitekwa nyara na vyombo vya usalama usiku, kuteswa na
wengine kutoweka kabisa. Mwaka 1998, akiwa Rais mstaafu, alifika
Uingereza kutibiwa. Akiwa huko Jaji mmoja wa Hispania (Jaji
Baltasar Garzon) alitoa hati ya kukamatwa kwa Pinochet na
kuamuru apelekwe Hispania kushtakiwa kwa makosa yake ya
uvunjaji wa haki za binadamu. Alikamatwa lakini utaratibu wa
urejeshwaji (extradition) ilibidi ufanyike. Mawakili wake walitoa hoja
kuwa Rais mstaafu hawezi kushtakiwa kwa mambo aliyoyafanya
akiwa kiongozi wa nchi na hivyo hawezi kupelekwa Hispania. Kesi
hii ilifika kwenye Mahakama ya Mamwinyi (House of Lords).

Mahakama (House of Lords) ilisema kuwa kiongozi wa nchi na


balozi wana kinga mbili: wana kinga ya kiofisi (rationae materiae1)

History (Summer, 1998), pp.49-53, p.49 & 50]. Naye Rais Bill Clinton alizua
utata na mjadala mkali alipoamua, katika dakika za mwisho za awamu ya pili ya
Urais wake, kutoa msamaha kwa kaka yake, mtoto wa Waziri wake, Katibu wake
wa zamani, rafiki yake wa kisiasa, na mtu ambaye alitiwa hatiani kwa kukwepa
kodi kwa kiasi kikubwa cha fedha kuliko mtu mwingine katika historia ya nchi
hiyo.[Angalia Harold J. Krent, “Conditioning the President's Conditional Pardon
Power”, in California Law Review, Vol. 89, No. 6 (Dec., 2001), pp. 1665-1720,
pp.1666-1667. na, Charles Shanor & Marc Miller “Pardon Us: Systematic
Presidential Pardons”, Federal Sentencing Reporter, Vol. 13, No. 3-4, Pardon
Power and Sentencing Policy(November/December 2000 - January/February
2001), pp. 139-146, p.140]
1 Kamusi ya Sheria ya Black inaeleza kuwa maana “rationae materiae” ni kuwa

“kitokanacho na suala fulani” (By reason of the matter involved) [Angalia Bryan
A. Garner (ed.), (2009), Black's Law Dictionary, 9th edn, Thomson Reuters, St
Paul, Minnesota].
73
na kinga ya kibinafsi (rationae personae1). Maana yake ni kuwa
kiongozi wa nchi hawezi kushtakiwa kwa maamuzi aliyoyafanya
kama kiongozi wa Serikali (rationae materiae) na pia akiwa
madarakani hawezi kukamatwa kwa sababu mwili wake una kinga
(rationae personae). Kinga hizi, kama anayoeleza Dinstein, zinaenda
pamoja.2 Mahakama iliendelea kusema kuwa kiongozi akiondoka
madarakani anapoteza kinga ya kibinafsi (rationae personae) lakini
anabaki na kinga ya kiofisi (rationae materiae). Maana yake ni kuwa
hatoweza kushtakiwa kwa mambo yote aliyoyafanya katika
“kutimiza kazi za Kiserikali.” Mahakama ilienda mbele na kujiuliza:
“je, kutesa na kuua watu ni kazi za Serikali?”

Katika Pinochet Na 3, Lodi Browne-Wilkinson alijiuliza swali kama


hilo na kujibu kama ifuatavyo;
Can it be said that the commission of a crime which is
an international crime against humanity and jus
cogens is an act done in an official capacity on behalf
of the state? I believe there to be strong ground for
saying that the implementation of torture as defined in
the Torture Convention cannot be a State function.

Naye Lodi Hutton alieleza;


My conclusion that Senator Pinochet is not entitled to
immunity is based on the view that the commission of
acts of torture is not a function of a head of state, and
therefore in this case the immunity to which Senator
Pinochet is entitled as a former head of state does not
arise in relation to, and does not attach to, acts of
torture.

Na katika Pinochet Na 1, Lodi Nicholls alinena:


International law recognises, of course, that the
functions of a head of state may include activities
which are wrongful, even illegal, by the law of his own

1 Kamusi ya Sheria ya Black inaeleza kuwa maana “rationae materiae” ni kuwa


“kitokanacho na suala fulani” (By reason of the person concerned) [Angalia Bryan
A. Garner (ed.), (2009), Black's Law Dictionary, 9th edn, Thomson Reuters, St
Paul, Minnesota].
2 Dinstein, "DiplomaticI mmunity from Jurisdiction Rationae Materiae"( 1966) 15

I.C.L.Q. 76, at p.79. kama alivyonukuliwa na J. Craig Barker, Colin Warbrick and
Dominic McGoldrick, “The Future of Former Head of State Immunity after ex
parte Pinochet”, in The International and Comparative Law Quarterly, Vol. 48, No.
4 (Oct., 1999), pp. 937-949, p.940.
74
state or by the laws of other states. But international
law has made plain that certain types of conduct,
including torture and hostage-taking, are not
acceptable conduct on the part of anyone. This applies
as much to heads of state, or even more so, as it does
to everyone else; the contrary conclusion would make
a mockery of international law.

Nukuu hizi zote zinaweza kutafsiriwa kwa ujumla wake kama


ifuatavyo: ingawa zamani msimamo wa sheria ulikuwa kuwa,
kiongozi wa nchi alikuwa na kinga kwa mambo yote aliyoyafanya
kwa niaba ya Serikali hata kama mambo hayo yalikuwa ni kinyume
cha sheria, katika mazingira ya sasa msimamo huo haukubaliki.
Sheria za kimataifa zinazuia vitendo vya kutesa au kuteka watu
nyara. Hivyo, vitendo vya kutesa, kuteka au kuua watu
havitakubalika kama ni kazi za Serikali. Kwa kuwa kinga
inahusishwa na kazi za Kiserikali, anayefanya uhalifu wa kutesa au
kuteka nyara watu hawezi kupewa kinga kwa sababu hizo siyo kazi
za Kiserikali. Serikali inatakiwa kuwalinda watu, siyo kuwateka,
kuwatesa ama kuwaua.

Yaliyoelezwa hapo juu yanawakilisha mtizamo wa kisasa kuwa


“kinga kamilifu” (absolute immunity) inaruhusu viongozi wa nchi
kufanya uhalifu na hivyo inakinzana na utawala wa sheria na
hifadhi ya haki za binadamu ambao ni utamaduni mpya wa jamii
ya dunia ya sasa. Hivyo, kinga yenye ukomo (restrictive immunity)
ndiyo inayoonekana kuwa inafaa katika mazingira ya sasa.

6.1.7 Muhtasari

Kutokana na marejeo yaliyofanywa hapo juu masuala haya


yamejitokeza;

Msingi wa kinga ya kushtakiwa kwa kiongozi wa nchi huko


Uingereza na nchi zingine za Ulaya ni mfumo wa ufalme
(monarchy). Mfalme hakutakiwa kushtakiwa kwa sababu nchi
(realm au kingdom) ilichukuliwa kuwa ni mali yake. Vyombo vyote
vya Kiserikali pamoja na Mahakama vilikuwa vyake; watu (subjects
of the king) walikuwa chini yake na hakuna aliyekuwa na haki ya
kumhoji Mfalme kuhusu lolote lile; na Mfalme hakuwa binadamu
wa kawaida — asingeweza kufanya makosa kama binadamu

75
wengine (the king can do no wrong). Mwandishi wa Kiingereza, Sir
Arthur Watts, anasema hivi;

A Head of State's immunity is enjoyed in recognition of


his very special status as holder of his State's highest
office ... his position as Head of State is one which he
has erga omnes, at all times and wherever he is.1

Tafsiri ya ujumla ya nukuu hii ni kwamba kiongozi wa nchi


anapewa kinga kwa “kutambua hadhi yake” kama mtu
anayeshikilia ofisi ya juu kabisa na ana haki ya kuheshimiwa na
kutambuliwa hivyo na mataifa mengine. Erga omnes ni kanuni
(principles) za sheria za kimataifa ambazo zinastahili kutambuliwa
na kuheshimiwa na mataifa yote.2 Mwandishi huyu anachosema ni
kuwa kiongozi wa nchi anapewa kinga kutokana na “hadhi yake ya
kipekee kabisa.” Mfalme ana hadhi ya kipekee katika utamaduni
wa nchi hiyo.

Katika nchi ambazo zina mfumo wa Urais kama Ufaransa na


Marekani kiongozi wa nchi hapewi kinga kwa sababu ya hadhi
yake. Anapewa kinga kufuatana na misingi ya utendaji (functional
necessity or convenience) kama inavyoainishwa hapa chini;

 Kinga kwa watumishi wa umma katika utendanji wao wa kazi


ni kutaka watumishi hao waweze kutekeleza majukumu yao
bila upendeleo na woga. Kinga ina lengo la kuwakinga
watumishi wa umma dhidi ya vitisho vya kushtakiwa
ambavyo wanaweza kukumbana navyo na ambayo
vitakinzana na utendaji wao wa kazi kwa utaratibu unaofaa.

 Msimamo wa sheria wa nchi ya Marekani ni kuwa “kinga


kamilifu” (absolute immunity) kuhusiana na “mambo yote
anayoyafanya kuhusiana na kazi yake.” Hii ina maana kuwa
anapewa kinga hata kuhusiana na maamuzi anayoyafanya

1 Sir Arthur Watts, "The Legal Position in International Law of Heads of States,
Heads of Governments and Foreign Ministers" (1994) 247 Hague Recueil 9, at
p.53. kama alivyonukuliwa na J. Craig Barker, Colin Warbrick and Dominic
McGoldrick, “The Future of Former Head of State Immunity after ex parte
Pinochet”, in The International and Comparative Law Quarterly, Vol. 48, No. 4
(Oct., 1999), pp. 937-949, p.940.
2 Angalia Jean-Marie Henckaerts and Louise Doswald-Beck, (2009), Customary

International Humanitarian Law, Vol 1, Cambridge University Press, Cambridge,


p.512.
76
kwa nia mbaya (malice) au yanayovunja sheria. Mahakama ya
Juu ya Marekani ilisema kinga ya namna hii siyo hatari kwao
kwa sababu kuna utaratibu wa Rais kuondolewa na Bunge
(impeachment), kuna vyombo vya habari vinayomwangalia
Rais kwa ukaribu mkubwa. Pia ilisemwa kuwa kuna
vichocheo vya Rais kutovunja maadili kama vile kutaka
kuchaguliwa tena, kulinda heshima yake na kuwa na nafasi
fulani katika historia ya nchi.

 Kutokana na umuhimu wa ofisi yake Rais akianza


kufunguliwa mashtaka ya madai kuhusiana na maamuzi
yake mengi na kutumia muda wake kujitetea kuna hatari ya
kazi za Serikali kukwama.

 Kutokana na asili ya kazi zake, kuruhusu Rais kufunguliwa


mashauri ya madai kuhusiana na maamuzi yake kunaweza
kuwafanya watu wengi kufungua mashauri dhidi yake.

 Wakati mwingine matakwa ya umma ya kutaka kuboresha


utendaji wa Serikali inabidi yapewe kipaumbele kuliko haki
ya mtu mmoja mmoja kupata fidia.

 Huko Marekani Rais hana kinga kuhusiana na matendo yake


binafsi yasiyohusiana na kazi yake ya Urais.

 Mwelekeo wa sasa unapendelea kinga yenye ukomo


(restrictive immunity) kuliko kinga kamilifu (absolute immunity).
Tofauti na kinga kamilifu, kinga yenye ukomo haimpi kiongozi wa
nchi kinga kuhusiana na vitendo vyake vya kihalifu.

6.1.8 Tathmini ya Kinga ya Rais kwa Sasa

Ni vizuri kutathmini kwa kifupi msingi wa kinga ya Rais katika


Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977. Bila shaka
kinga hiyo haitokani na msingi wa ufalme. Mwaka 1962, viongozi
wetu waliamua kuanzisha ofisi ya Rais na kuachana na Katiba ya
Uhuru ambayo ilimtaja Gavana (mwakilishi wa Malkia wa
Uingereza) kuwa ni Mkuu wa Nchi.1 Hali kadhalika, Wazanzibari
waliamua kumwaga damu katika Mapinduzi ya tarehe 12 Januari

1 Kifungu cha 11 cha Katiba ya Uhuru ya Mwaka 1961.


77
1964 ili kuuondoa utawala wa KiSultani, ambao ni utawala wa
kifalme, na kuanzisha ofisi ya Rais. Na hatimaye Muungano
ulipoundwa tarehe 26 Aprili 1964 ulijengwa katika msingi wa Rais
kama Mkuu wa Nchi. Hii ina maana kuwa waasisi wa Taifa letu
walidhamiria kuchukua mwelekeo tofauti — mwelekeo wa kuunda
Taifa la kidemokrasia lenye viongozi wanaochaguliwa na
wanaofuata sheria. Waliamua kuachana na utaratibu wa mtu
kupewa uongozi kutokana na hadhi au nasaba yake. Walitaka
kuwe na utawala wa sheria. Kuhusiana na hili, katika shauri la
Mwalimu Paul John Mhozya v Attorney General (No. 1) [1996] TLR
130, Samatta, JK, alisema;

The notion, apparently harboured by some people in


this country, that the President of the United Republic
is above the law is subversive of the Constitution and
the laws. All Government leaders, including the
President, are, like the humblest citizen, bound to
comply with the laws of this country. The maxim `The
King can do no wrong' has no place in our law even if
the word `President' is substituted for the word `King'.
Everyone and every institution or organisation in this
country is enjoined to pay respect to the principle of
supremacy of the law, see s 26(1) of the Constitution.

Katika nukuu hii Samatta, JK (kama alivyokuwa), alisisitiza kuwa


viongozi wote akiwemo Rais wanatakiwa kufuata sheria lakini la
muhimu zaidi ni kuwa mfumo wa Kiingereza ambao Mfalme
anapewa upendeleo maalum hauna nafasi katika nchi yetu.

Kwa hivyo, mambo yafuatayo yanaweza kuelezwa. Kwanza, sheria


inayosema kuwa Mahakama haiwezi kutoa amri kwa Rais hata
kama kuna mwananchi ameshinda kesi ya madai dhidi yake
inahitaji kuangaliwa upya ili kuimarisha misingi ya utawala wa
sheria. Mathalan, Rais anagombania kiwanja (plot of land) na
mwananchi mmoja. Mwananchi akafungua kesi na Mahakama
ikasema kiwanja hicho siyo cha Rais bali ni cha mwananchi lakini
mwishowe Mahakama ikamwambia mwananchi, “hatuwezi
kumwamuru Rais kuondoka kwenye kiwanja chako; itakuwa hiari
yake!” Hii inaweza kumfanya Rais aonekane kuwa yuko juu ya
sheria. Hali hiyo pia inaweza ikaathiri misingi ya utawala wa
sheria.

78
Pili, sheria inasema kuwa Mahakama haiwezi kumwamuru Rais
kufika Mahakamani; haiwezi kumwamuru Rais kumleta mtu fulani
au kuleta kitu fulani. Vile vile kama kuna mwananchi ameiomba
Mahakama kumuita Rais, Mahakama haitakiwi kutoa amri ya
kumuita bali itamjulisha kuwa kuna maombi kama hayo ili iwe
hiari yake kuja au la. Sheria hii pia inaweza ikafanyiwa
marekebisho ili kumruhusu Rais kuwakilisha ushahidi wake
mahakamani pale inapohitajika. Ikiwa hivyo, Rais kama Mkuu wa
Nchi na raia nambari moja atakuwa anawaongoza wananchi
wengine katika kuimarisha mfumo wa utendaji haki. Utii wa amri
ya mahakama kwa Rais siyo kitu kigeni kama tunavyoweza kuona
kutoka huko ambako taasisi ya Urais imetokea. Katika shauri la
Clinton v Jones (95-1853), 520 U.S. 681 (1997) Mahakama ya Juu
ya Marekani ilisema hivi;

Sitting Presidents have responded to court orders to


provide testimony and other information with sufficient
frequency that such interactions between the Judicial
and Executive Branches can scarcely be thought a
novelty. President Monroe responded to written
interrogatories, see Rotunda, Presidents and Ex
Presidents as Witnesses: A Brief Historical Footnote,
1975 U. Ill. L. F. 1, 5-6, President Nixon--as noted above-
-produced tapes in response to a subpoena duces tecum,
see United States v Nixon, President Ford complied with
an order to give a deposition in a criminal trial, United
States v Fromme, 405 F. Supp. 578 (ED Cal. 1975), and
President Clinton has twice given videotaped testimony
in criminal proceedings, see United States v McDougal,
934 F. Supp. 296 (ED Ark. 1996); United States v
Branscum, No., LRP-CR-96-49 (ED Ark., June 7, 1996).
Moreover, sitting Presidents have also voluntarily
complied with judicial requests for testimony. President
Grant gave a lengthy deposition in a criminal case under
such circumstances, R. Rotunda & J. Nowak, Treatise on
Constitutional Law §7.1 (2d ed. 1992), and President
Carter similarly gave videotaped testimony for use at a
criminal trial, ibid.”

Katika nukuu hii inaonyeshwa namna Marais mbalimbali wa


Marekani walivyoheshimu maagizo ya Mahakama. Wameshiriki
kutoa ushahidi; wameshirikiana na Mahakama kuwasilisha

79
nyaraka au vitu vingine vinavyohitajika ili haki itendeke.
Wamekuwa ni watu watiifu wa sheria na mfano mzuri kwa raia
wengine.

6.2 MAPENDEKEZO
6.2.1 Uwepo wa Kinga
Kama ilivyoelezwa mwanzoni, kuna maoni kuwa kinga ya Rais
iondolewe. Mojawapo ya sababu zinazotolewa ni kuwa Rais
anaweza kufuja mali ya umma, hivyo inafaa awajibishwe; nchi
inaongozwa na utawala wa sheria; na kwamba binadamu wote ni
sawa. Baada ya kufanya marejeo mbalimbali, tunaona kuwa ni
muhimu Rais kama kiongozi wa nchi awe na kinga. Ofisi ya Rais
ina nafasi ya kipekee katika mfumo wetu wa Kikatiba: Rais
amepewa majukumu mengi. Anatakiwa kuhakikisha kuwa nchi ina
amani na utengamano. Analo jukumu la kuhakikisha kuwa nchi
inasonga mbele kiuchumi, kijamii na kisiasa. Anao wajibu wa
kusimamia nidhamu ya viongozi na watumishi wengine wa Serikali.
Anayo majukumu mengine kadha wa kadha.

Yumkini katika utekelezaji wa majukumu haya Rais atakosana na


watu wengi. Mathalan, wale watu ambao Rais ataamuru ardhi yao
ichukuliwe ili barabara au hospitali ijengwe wangependa
wamshtaki Rais; vile vile Waziri anayefukuzwa kazi kwa vile ni mla-
rushwa (ingawa hajakamatwa) atapenda kumfungulia Rais
mashtaka; hali kadhalika maadui wake wa kisiasa wangependa
wamfungulie kesi nyingi Mahakamani, waharibu sifa yake ili
wamshinde katika uchaguzi unaokuja. Haya ni machache katika
yumkini nyingi za aina hii. Katika mazingira ya namna hii itakuwa
ni vigumu kwa Rais kufanya kazi kwa kujiamini na kutekeleza
majukumu yake ipasavyo kama hana kinga. Kwa hiyo kinga ni
muhimu. Ni kweli Watanzania wote ni sawa lakini siyo Watanzania
wote wenye majukumu kama ya Rais.
Hata hivyo tunapendekeza mabadiliko kuhusu kinga ya Rais kama
ilivyo hapa chini.

6.2.2 Misingi ya Kinga

Kutokana na yaliyosemwa hapo juu inapendekezwa kuwa kinga ya


Rais kutoshtakiwa ijengwe katika misingi mikuu mitatu. Msingi wa

80
kwanza ni “utendaji” (functional necessity or theory). Rais apewe
kinga ambayo itamuwezesha kufanya kazi yake bila hofu ya
kushtakiwa mara kwa mara na aweze kutumia muda na nguvu
zake katika kuiongoza Serikali katika kutekeleza sera, mipango na
matakwa ya wananchi.

Msingi wa pili uwe ni “uwajibikaji” (accountability). Msingi huu


unatokana na ukweli kwamba nafasi ya Urais inakaliwa na
binadamu ambao wanaweza kushawishika kutumia nafasi zao
kujinufaisha wao binafsi. Pia, nafasi ya Urais inaambatana na
madaraka makubwa ambayo yanaweza kutumika kuonea watu
wengine na kuhujumu nchi kwa ajili ya faida binafsi ya Rais au ya
kikundi fulani cha watu. Hivyo, kutokana na changamoto hii
dhana ya “kinga kamilifu” (absolute immunity) inafaa kuepukwa na
badala yake Rais apewe “kinga yenye ukomo” (restrictive or limited
immunity). Maana yake ni kuwa Rais akitenda uhalifu au
kuuhujumu uchumi akiwa madarakani asiruhusiwe kujificha
nyuma ya kivuli cha kinga, awajibishwe. Katiba ya Kenya
imeondokana na kinga kamilifu. Ibara ya 143 (4) ya Katiba hiyo
inasema, “The immunity of the President under this Article shall not
extend to a crime for which the President may be prosecuted”. Ibara
ya hii inasema kuwa Rais hatokuwa na kinga kuhusiana na kosa la
jinai ambalo anaweza kushtakiwa nalo. Hata hivyo, wakati wa
kuandika Katiba inafaa kuzingatia kuwa Rais ana kazi nyingi,
anaongea na watu wengi, na anapata changamoto nyingi.
Inawezekana akafanya kitendo fulani bila kujua kuwa kitendo
hicho ni kinyume cha sheria. Hivyo, ni vizuri Katiba ieleze bayana
kuwa Rais atawajibishwa kwa kufanya vitendo vile ambavyo
“kiuwazi ni kinyume cha sheria” (manifestly unlawful) tu. Mathalan,
haitokuwa utetezi kusema Rais hakujua kama kuua au kutesa
watu, au kuchukua fedha za umma kunazuiwa na sheria.

Msingi wa tatu wa kinga uwe ni “utawala wa sheria” (Rule of Law).


Dhana ya utawala wa sheria ina maana nyingi lakini mojawapo ni
kuwa watu au wananchi wote pamoja na viongozi wote wapo chini
ya sheria. Ni wajibu wa kila Mtanzania, awe mwananchi wa
kawaida au kiongozi, kufuata sheria. Hivyo, sheria inayosema kuwa
Mahakama haina uwezo wa kumuita Rais Mahakamani kutoa
ushahidi, au kumwamuru kuleta nyaraka fulani Mahakamani, au
kusema Rais hata kama katika maisha yake binafsi akimwonea
mwananchi wa kawaida Mahakama haina uwezo wa kutoa amri
dhidi yake, inaweza kufanyiwa marekebisho ili kuimarisha utawala
81
wa sheria. Ikiwa hivyo, Rais, kama kiongozi mkuu, atakuwa ni
mfano kwa wananchi wengine katika kufuata na kutii sheria. Hii ni
kutokana na kuwa Ofisi ya Rais inajengwa katika msingi wa
demokrasia na utawala wa sheria.

6.2.3 Kinga Inayopendekezwa


Inapendekezwa Rais awe na kinga kama ifuatavyo;
 Rais hatoshtakiwa kwa kosa la jinai kwa jambo alilolifanya
akiwa madarakani isipokuwa akitenda kosa la “kiuwazi” la
kihaini, kijinai, au uhujumu uchumi;

 Rais hatoweza kushtakiwa kwa kosa la “kiuwazi” la uhaini,


jinai au uhujumu uchumi hadi kwanza aondolewe
madarakani na Bunge au baada ya kumaliza muhula wake
wa uongozi;

 Rais atakuwa na kinga ya kutofunguliwa shauri la madai


kuhusiana na jambo alilolifanya kuhusiana na kazi yake na
kinga hii atakuwa nayo akiwa madarakani na itaendelea
katika maisha yake yote akiwa nje ya madaraka;

 Rais anaweza kufunguliwa shauri la madai kwa vitendo vyake


binafsi ambavyo havihusiani na majukumu yake ya umma
ama akiwa madarakani au baada ya kumaliza muhula wake
wa uongozi.

82
SEHEMU YA SABA

7.1 MAMLAKA YA UTEUZI


7.1.1 Hoja
Kuna hoja kuwa madaraka ya Rais ya kuwateua watumishi
mbalimbali wa Wizara, mashirika ya umma, idara na taasisi
mbalimabali za dola ni makubwa sana. Vile vile Rais amepewa
mamlaka ya kuanzisha na kufuta ofisi mbalimbali za Serikali,
kuajiri, kuwachukulia watumishi hatua za kinidhamu, na hata
kuwafukuza. Hoja ni kwamba madaraka haya yapunguzwe.

7.1.2 Hali Halisi


Madaraka ya Rais kuhusu uteuzi ni makubwa. Madaraka hayo
yamekuwa yakiongezeka kupitia mabadiliko mbalimbali ya katiba
na sheria mbalimbali za nchi.1 Rais ana mamlaka ya kumteua
Makamu wa Rais nafasi hiyo ikiwa wazi, Waziri Mkuu na Mawaziri
na Manaibu Waziri, Mwanasheria Mkuu, Mabalozi wote
wanaoiwakilisha Tanzania nchi za nje, Katibu Mkuu Kiongozi,
Makatibu Wakuu, Gavana wa Benki Kuu na Manaibu wake,
Mkurugenzi wa Mashtaka, Wakuu wa Mikoa yote na wilaya zote,
wakuu na watendaji wa vyombo vya uwajibikaji kama TAKUKURU,
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Sekretariati ya
Maadili ya Viongozi wa Umma, Wakurugenzi wa Halmashauri zote.
Vile vile, Rais anawateua wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama.
Aidha, Rais anawateua Wenyeviti wa Bodi mbalimbali na
Wakurugenzi Wakuu wa Mashirika na Taasisi zingine za umma.
Vile vile, Rais anateua wakuu wa vyuo vikuu (chancellors) na
wenyeviti wa Mabaraza ya Vyuo Vikuu vyote vya umma; anawateua
Wenyeviti wa Bodi mbalimbali na Wakurugenzi Wakuu wa
mamlaka mbalimbali za udhibiti (regulatory authorities), idara na
taasisi zingine mbalimbali za Serikali.

Katika mhimili wa Mahakama, Rais anateua Jaji Mkuu na Majaji


wengine wote wa Mahakama ya Rufani; anamteua Jaji Kiongozi na
Majaji wote wa Mahakama Kuu. Hali kadhalika, Rais anamteua
Mtawala Mkuu wa Mahakama (Chief Court Administrator), Msajili

1Chama cha Mapinduzi, Mapendekezo ya Halmashauri Kuu ya Taifa Juu ya


Marekebisho ya Katiba ya Serikali, Waraka wa 1983.
83
wa Mahakama ya Rufani na makamu wake, Msajili wa Mahakama
Kuu na Naibu wake. Vilevile, wajumbe wote wa Tume ya Utumishi
wa Mahakama ni wateule wa Rais. Mamlaka ya uteuzi ya Rais yapo
pia katika mhimili wa Bunge. Rais anamteua katibu wa Bunge na
amepewa mamlaka ya kuwateua Wabunge kumi (10).

Hata hivyo, hii siyo orodha kamili ya wateule wa Rais. Uwingi wa


wateule ulishawahi kuzungumziwa na Tume ya Rais kuhusu
rushwa maarufu kama Tume ya Warioba. Taarifa ya Tume ilisema:
“The President appoints too many people beyond his ability to put
them in his memory.” 1 Maana yake ni kuwa Rais anateua watu
wengi sana kiasi kwamba ni vigumu kuwakumbuka wote. Pia,
Tume ya Rais ya Mfumo wa Chama Kimoja au vyama vya siasa
Tanzania, maarufu kama Tume ya Nyalali iliona kuwa madaraka ya
Rais “ni makubwa mno”. 2 Halikadhalika, Kamati ya Kuratibu
Maoni Kuhusu Katiba (Kamati ya Kisanga) ilibaini kuwa madaraka
ya Rais ni makubwa kiasi cha kutoa mwanya wa kutumika vibaya.3
Mwishoni mwa taarifa hii kuna Jedwali lenye orodha pana ya
wateule wa Rais. Jedwali linaonyesha wateule, sheria inayompa
Rais mamlaka ya kuteua, ibara ya Katiba au kifungu cha sheria
husika kinachotoa mamlaka, na kama Rais anafanya uteuzi huo
kwa kushauriwa au kwa anavyoona yeye mwenyewe.

7.1.3 Faida na Changamoto


Utaratibu ambao Rais ana mamlaka mapana ya uteuzi una faida na
changamoto zake. Faida za utaratibu huu ni kama ifuatavyo:
 Ni rahisi kwa kiongozi kufanya mabadiliko na maamuzi kwa
haraka zaidi. Utaratibu wa kuwatafuta kutangaza nafasi,
kuwasaili, na kuwachuja viongozi na watendaji unachukua
muda mrefu zaidi;

 Unawafanya wateule na wale wenye mategemeo ya kuteuliwa


kuwa watiifu kwa Rais na hivyo kumsaidia Rais kutekeleza
sera, mipango na majukumu aliyopewa wananchi kwa
urahisi zaidi;

1 The Report on the Commission on Corruption, Volume 1 (Chapter 1-5), pg. 76.
2 Tume ya Rais ya Mfumo wa Chama Kimoja au vyama vya siasa Tanzania,
Kitabu cha Kwanza, Uk.133
3 Kamati ya Kuratibu Maoni Kuhusu Katiba, Kitabu cha Kwanza, 1999, uk.77.

84
 Utaratibu huu unamsaidia Rais kuwapata watu anaowataka
ambao yeye anaona wanafaa kufanya nao kazi; na

 Utaratibu huu unampa Rais mamlaka ya kuteua watu


wanaowakilisha makundi mbalimbali katika nchi na kuifanya
Serikali kuwa na sura ya kitaifa kuliko makundi fulani.
Utaratibu mwingine unaangalia sifa zaidi kuliko kigezo hiki
muhimu;

Hata hivyo, utaratibu huu una changamoto nyingi kama


ifuatavyo:
 Unatoa nafasi ya uteuzi kufanyika kwa upendeleo na rushwa
bila kuzingatia uwezo na sifa stahili. Kwa mfano, kwa sababu
ya mfumo huu, Rais wa zamani wa Marekani, James A.
Garfield, aliuawa mwaka 1881 na mtu ambaye alitegemea
kuteuliwa lakini akanyimwa nafasi kinyume cha matarajio
yake kutokana na upendeleo na rushwa. Baada ya tukio hilo
sheria1 ilitungwa ili kumpunguzia Rais madaraka ya uteuzi
na kumbakishia nafasi chache kwa ajili viongozi wa ngazi juu
tu;

 Kukiwa na idadi kubwa ya wateule wengi kama ilivyo sasa


hali hiyo inatoa mwanya kwa Rais kufanya uteuzi kwa
kupotoshwa na washauri wake;

 Kwa kuwa kuna orodha ya viongozi na watendaji wanaohitaji


kuteuliwa, Rais anatumia muda mwingi ambao angeutumia
kufanya kazi zingine za kuleta maendeleo;

 Katika mazingira fulani kunakuwa na matatizo ya


uwajibikaji. Mfano katika wizara, Waziri, Katibu Mkuu, na
Kamishna wote ni wateule wa Rais. Inakuwa siyo rahisi kwa
watu hawa kuwajibishana kwa sababu wote ni wateule wa
Rais. Kila mmoja anaona kuwa ana hadhi sawa na
mwenzake.

 Rais hayupo karibu na wateule wake wengi na hivyo siyo


rahisi kuwasimamia kinidhamu na kuwawajibisha. Hali hii
inaweza kushusha ufanisi katika utendaji wa kazi.

1 The Pendleton Act, 1883.


85
7.2 UZOEFU WA NCHI NYINGINE

Inaonekana kuwa utaratibu unaofaa wa kupunguza madaraka ya


Rais ya uteuzi ni ya kuwa na utaratibu wa kugawa madaraka
baina yake na Waziri Mkuu. Utaratibu huu umepewa jina la
mgawanyo mpya wa madaraka(the newest separation of powers).1
Ingawa inaonekana kuwa mfumo huu unafanana na wa Tanzania,
Waziri Mkuu wa Tanzania sio kiongozi wa Serikali ila ni msimamizi
wa shughuli za kila siku za Serikali. Katika mfumo uliotajwa hapo
juu, Rais anakuwa ni Mkuu wa Nchi, Amiri-Jeshi-Mkuu na
anabakiza madaraka ya Kiserikali kidogo hasa kutoa mwongozo wa
kisera wa nchi. Waziri Mkuu anakuwa ni kiongozi wa Serikali.
Nchi zinazofuata mfumo huo ni pamoja na Ufaransa, Austria,
Finland, Iceland, Lithuania, Moldova, Poland, Ureno, Romania, na
Slovenia2. Tutaangalia mifano ya Ufaransa na Finland.

7.2.1 Ufaransa
Nchini Ufaransa, Rais ni Mkuu wa Nchi na Amiri-Jeshi-Mkuu na
jukumu lake kubwa ni kuhakikisha kuwa Katiba ya nchi inalindwa
na taasisi za umma zinafanya kazi vyema, ni mlinzi wa uhuru na
mipaka ya nchi.3 Kwa kuwa Mkuu wa Nchi, Rais amepewa
madaraka ya kumteua Waziri Mkuu, na kuwateua Mawaziri kwa
kushauriana na Waziri Mkuu.4 Rais amepewa mamlaka ya kufanya
uteuzi wa baadhi ya viongozi na watendaji wa kiraia na kijeshi
ambao nafasi zao zinahitaji Uteuzi wa Mkuu wa Nchi na Amiri-
Jeshi-Mkuu. Rais amepewa madaraka ya uteuzi wa Mabalozi,

1 Angalia Cindy, Skach.(2007). The “Newest” Separation of Powers:


Semipresidentialism . Oxford University Press and New York University School of
Law.
2 Steven, Roper.(2002). Are All Semipresidential Regimes the Same? A
Comparison of Premier-Presidential Regimes. Comparative Politics, Vol. 34, No. 3
(Apr., 2002), pp. 253-272
3 Angalia ibara ya 5 ya Katiba ya Ufaransa. Inasema kuwa « The President of the

Republic shall ensure due respect for the Constitution. He shall ensure, by his
arbitration, the proper functioning of the public authorities and the continuity of the
State.”
He shall be the guarantor of national independence, territorial integrity and due
respect for Treaties.
4 Ibara ya 8 ya Katiba ya Ufaransa ya Mwaka 1958. Ibara hiyo inasema

kuwa « the President of the Republic shall appoint the Prime Minister. He shall
terminate the appointment of the Prime Minister when the latter tenders the
resignation of the Government. On the recommendation of the Prime Minister, he
shall appoint the other members of the Government and terminate their
appointments.”
86
viongozi wa juu wa majeshi, wakurugenzi mbalimbali wa idara za
Serikali, wakuu wa taasisi za elimu, wakaguzi wa mahesabu ya
Serikali na Wakuu wa Mikoa. Sheria zinaweza kuainisha nafasi
zingine zaidi ya hizo hapo juu ambazo uteuzi wake utafanywa na
Rais. Uteuzi huo unafanyika kwenye mikutano ya Baraza la
Mawaziri lakini lazima uteuzi uthibitishwe na Bunge. Mamlaka ya
uteuzi ya Rais yatafanyika kwa kushauriana na kamati husika za
Bunge. Rais hatafanya uteuzi ikiwa theluthi mbili ya kura za
kamati za Bunge zinazohusika zitakataa.1

Waziri Mkuu ni kiongozi wa Serikali na ana mamlaka ya kuteua


viongozi mbalimbali wa kiraia na kijeshi2

7.2.2 Finland
Rais ni Mkuu wa Nchi na Amiri-Jeshi-Mkuu. Rais anachangia
madaraka na Waziri Mkuu ambaye ndiye kiongozi wa Serikali. Rais
anamteua Waziri Mkuu na huthibitishwa na Bunge. Rais pia
anateua Mawaziri wengine kwa ushauri wa Waziri Mkuu.3 Rais
anateua Makatibu Wakuu wa wizara, Mabalozi na viongozi wengine
ambao Katiba na sheria zinaona kuwa zinahitaji kuteuliwa na
mamlaka ya kipekee ya Rais kama Mkuu wa Nchi na Amiri Jeshi.
Rais pia anateua Maofisa wa vyombo vya ulinzi na usalama.4
Viongozi na watendaji wa dola wengine wanateuliwa na Serikali
kupitia mamlaka mbalimbali za nchi.5

7.3 MAPENDEKEZO
Kuna haja ya kutenganisha shughuli za Mkuu wa Nchi na kiongozi
wa Serikali ili Rais abaki zaidi na majukumu ya Mkuu wa Nchi na
Amiri-Jeshi-Mkuu na shughuli za Serikali ziwe kwa kiwango

1 Ibaraya 13 Katiba ya Ufaransa ya Mwaka 1958. Ibara hiyo inasomeka kama


ifuatavyo « He shall make appointments to the civil and military posts of the
State. Conseillers d’État, the Grand Chancelier de la Légion d’Honneur,
Ambassadors and Envoys Extraordinary, Conseillers Maîtres of the Cour des
Comptes, Prefects, State representatives in the overseas communities to which
article 74 applies and in New Caledonia, highest-ranking Military Officers,
Recteurs des Académies and Directors of Central Government Departments shall
be appointed in the Council of Ministers…. The President of the Republic shall not
make an appointment when the sum of the negative votes in each committee
represents at least three fifths of the votes cast by the two committees.”
2 Ibara ya 21 , kama hapo juu.
3 Ibara ya 61 ya Katiba ya Finland, 1999
4 Ibar aya 128 kama hapo juu
5 Ibara ya 126 kama hapo juu

87
kikubwa chini ya Waziri Mkuu. Ikiwa hivyo, Rais atabaki na
madaraka ya kumteua Waziri Mkuu, Mawaziri, wakuu wa vyombo
vya ulinzi na usalama, Mabalozi, watendaji na viongozi wengine
ambao uteuzi wao unahitaji mamlaka ya kipekee ya Mkuu wa Nchi
na Amiri-Jeshi-Mkuu.

Uteuzi mwingine wowote ufanywe na Serikali katika mamlaka


zake mbalimbali kama vile Tume za Utumishi kwa kuzingatia sifa,
uwezo na vigezo. Utaratibu huu ulipendekezwa pia na Tume ya
Warioba.

88
ORODHA YA WATEULE WA RAIS
IKULU NA WIZARA

Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa


/kushauriana
1. Makamu wa Rais (nafasi Katiba Ibara ya 50 (4) Bunge
ikiwa wazi)

2. Waziri Mkuu Katiba Ibara ya 51(1) Bunge

3. Mawaziri na Manaibu Katiba 55(1) and 55(2) Waziri Mkuu


Mawaziri wote

4. Katibu Mkuu Kiongozi The Public Service Act, 2002 4(1)

5. Makatibu Wakuu wa wizara The Public Service Act, 2002 5(1) (a)
zote

6. Manaibu Makatibu Wakuu The Public Service Act, 2002 5(1)(c)


wa wizara zote

7. Mabalozi wanaowakilisha The Public Service Act, 2002 5(1)(c)


nchi kwa mataifa mengine

8. Makamishana na Katiba 129(3)


Makamishana wasaidizi wa
Tume ya Haki za Binadamu
na Utawala Bora

89
Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa
/kushauriana
9. Mwanasheria Mkuu wa Katiba 59 (1)
Serikali

10. Naibu Mwanasheria Mkuu Katiba 59A (1)

11. Mkurugenzi wa Mashtaka Katiba 59B (1)

12. Jaji Mkuu Katiba 118(2) Tume ya


Utumishi wa
Mahakama

13. Jaji Kiongozi Katiba 109(1) Tume ya


Utumishi wa
Mahakama

14. Majaji wa Rufaa Katiba 118(3) Jaji Mkuu

15. Majaji wa Mahakama Kuu Katiba 109 (1) Tume ya


Utumishi wa
Mahakama

16. Wajumbe wa Baraza la Katiba 110A(3)(b)


Kushughulikia nidhamu ya
Majaji

90
Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa
/kushauriana
17. Wajumbe wa Tume ya Katiba 112(2); 112 (2) Jaji Mkuu
Utumishi wa Mahakama (c); kuhusiana na
uteuzi wa Jaji
wa Rufaa
kama mjumbe

18. Mtawala Mkuu wa The Judiciary Administration 7(1) Tume ya


Mahakama Act, 2011 Utumishi wa
Mahakama

19. Msajili Mkuu wa Mahakama The Judiciary Administration 27(1) Tume ya


Act, 2011 Utumishi wa
Mahakama

20. Mwenyekiti, Katibu na The Law Reform Commission 5(1)


makamishna wote wa Tume Act, Cap.171 [R.E. 2002]
ya Kurekebisha sheria

21. Mwenyekiti, Shirika la The Tanzania Legal 5(2)(a)


Huduma za Kisheria Corporation (Establishment)
Tanzania(The Tanzania Legal Order. (Sections 3, 5 and 10),
Corporation) [RE 2002]

22. Wabunge 10 wa Kuteuliwa Katiba 66(e)

23. Katibu wa Bunge Katiba 87

91
Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa
/kushauriana
24. Mwenyekiti, Makamu na Katiba 134 (1)
Wajumbe wa Tume ya
Pamoja ya Fedha

25. Wajumbe wa Kumchunguza Katiba 144(3)


Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu

26. Kamishna wa Bima/ Naibu The Insurance Act, 2009 7(1), 8(1)
Kamishna wa Bima

27. Gavana wa Benki Kuu na The Bank of Tanzania Act, 8(1) & (3)
Manaibu wake watatu 2006

28. Mhasibu Mkuu wa Serikali The Public Finance Act, Cap 7(1)
348 [R.E 2002]

29. Katibu wa Tume ya The Planning Commission Act, 8(1) Baraza la


Mipango Cap 314 [R.E.2002] Chuo

30. Manaibu wa Katibu wa The Planning Commission Act, 9(1)


Tume ya Mipango Cap 314 [R.E.2002]

31. Mwenyekiti wa Bodi, TRA Tanzania Revenue Authority 10(1) (a) Waziri wa
Act Cap 339 [R.E 2002] Fedha

32. Mkurugenzi Mkuu, TRA Tanzania Revenue Authority 16(1) Waziri wa


Act, Cap 399 [R.E 2002] Fedha

92
Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa
/kushauriana
33. Kamishna wa Kitengo cha The Anti-Money Laundering 5(1)
Kupambana na Fedha Act, 2006
Haramu

34. Mtendaji Mkuu, Mamlaka The Public Procurement Act, 23(1)


ya Usimamizi wa Manunuzi
2011
ya Umma (PPRA)

35. Mwenyekiti wa Mamlaka ya The Public Procurement Act, 88(2) (a)


Kusikiliza Rufani za
2011
Migogoro ya Manunuzi ya
Umma (Public Procurement

Appeals Authority)

36. Katibu mtendaji wa The Public Procurement Act, 89(1)


Mamlaka ya Kusikiliza
2011
Rufani za Migogoro ya
Manunuzi ya Umma (Public
Procurement

Appeals Authority)

37. Mwenyekiti wa Bodi ya The Gaming Act, 2003 5(1)(a)


Bahati Nasibu ya Taifa

38. Katibu Mtendaji wa Baraza The National Examinations 6 (1)

93
Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa
/kushauriana
la Mitihani Tanzania(NECTA) Council of Tanzania, Cap 107
[R.E 2002]

39. Mwenyekiti wa Baraza la The National Council for 4(1) (a) Waziri wa
Taifa la Elimu ya Ufundi Technical Education Act, Cap Elimu
(NACTE) 129 [R.E 2002]

40. Kamishna wa Elimu Not yet identified

41. Mwenyekiti wa Bodi, The Education Fund Act, Cap 7(2) na Jedwali
Mamlaka ya Elimu Tanzania 412 [R.E 2002] la Kwanza, Kif
2(1) (a)

42. Wakuu wa Vyuo Vikuu vya The Universities Act, 2005. 35 (1)
Umma (Chancellors)

43. Mkuu wa Chuo, Chuo Kikuu The Universities Act, 2005 35(1), Baraza la
cha Dar es Salaam Chuo

44. Mwenyekiti wa Baraza la The Universities Act, 2005 44 (3) Waziri


Chuo, Chuo Kikuu cha Dar
es Salaam

45. Mkuu wa Chuo, Chuo Kikuu The Universities Act, 2005 35(1), Baraza la
cha Sokoine Chuo

46. Mwenyekiti wa Baraza la The Universities Act, 2005 44 (3) Waziri


Chuo, Chuo Kikuu cha
94
Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa
/kushauriana
Kilimo, Sokoine

47. Mkuu wa Chuo, Chuo Kikuu The Universities Act, 2005 35(1), Baraza la
Huria cha Tanzania Chuo

48. Mwenyekiti wa Baraza la The Universities Act, 2005 44 (3) Waziri


Chuo, Mwenyekiti wa Baraza
la Chuo, Chuo Kikuu Huria

49. Mkuu wa Chuo, Chuo Kikuu The Universities Act, 2005 35(1) Baraza la
Mzumbe Chuo

50. Mwenyekiti wa Baraza la The Universities Act, 2005 44 (3) Waziri


Chuo, Chuo Kikuu Mzumbe

51. Mkuu wa Chuo, Chuo Kikuu The Universities Act, 2005 35(1), Baraza la
cha Afya na Sayansi za Tiba, Chuo
Muhimbili

52. Mwenyekiti wa Baraza la The Universities Act, 2005 44 (3) Waziri


Chuo, Chuo Kikuu cha Afya
na Sayansi za Tiba,
Muhimbili

53. Mkuu wa Chuo, Chuo Kikuu The Universities Act, 2005 35(1), Baraza la
cha Ardhi Chuo

95
Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa
/kushauriana
54. Mwenyekiti wa Baraza la The Universities Act, 2005 44 (3) Waziri
Chuo, Chuo Kikuu cha
Ardhi

55. Mkuu wa Chuo, Chuo Kikuu The Universities Act, 2005 35(1) Baraza la
cha Dodoma Chuo

56. Mwenyekiti wa Baraza la The Universities Act, 2005 44 (3) Waziri


Chuo, Chuo Kikuu cha
Dodoma

57. Mkuu wa Chuo, Chuo Kikuu The Universities Act, 2005 35(1) Baraza la
cha Nelson Mandela Chuo

58. Mwenyekiti wa Baraza la The Universities Act, 2005 44 (3) Waziri


Chuo, Chuo Kikuu cha
Nelson Mandela

59. Makamu Mwenyekiti, Tume The Planning Commission Act, 4(4) Baraza la
ya Mipango Cap 314 [R.E.2002] Chuo

60. Mkurugenzi, Taasisi ya The Tanzania Institute of 9(1)


Elimu Tanzania Education Act, Cap 142 [R.E
2002]

61. Mwenyekiti wa Bodi, VETA The Vocational Education and 5(2)(a)


Training Act, Cap 82 [R.E

96
Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa
/kushauriana
2002]

62. Mwenyekiti wa Baraza la The Dar es Salaam Institute of 7(a)


Taasisi ya Teknolojia Dar es Technology Act, Cap 144 [R.E
Salaam 2002]

63. Mwenyekiti wa Bodi, Chuo The National Social Welfare 5(2) na


cha Ustawi wa Jamii Training Institute Act, Cap 110 Jedwali-kif 2(a)
[R.E 2002]

64. Katibu Mtendaji wa Baraza The National Examinations 6 (1)


la Mitihani Tanzania(NECTA) Council of Tanzania, Cap 107
[RE 2002]

65. Kamishna wa Elimu Not yet located

66. Mwenyekiti wa Bodi, The Education Fund Act, Cap 7(2) na Jedwali
Mamlaka ya Elimu Tanzania 412 [RE 2002]. la Kwanza, Kif
2(1) (a)

67. Mkuu wa Chuo, Chuo Kikuu The Universities Act, 2005 35(1), Baraza la
cha Dar es Salaam Chuo

68. Mwenyekiti wa Bodi, Taasisi The Mwalimu Nyerere Memorial 6(1)


ya Kumbukumbu ya Mwl Academy Act, 2005
Nyerere

97
Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa
/kushauriana
69. Mkuu wa Chuo, Taasisi ya The Mwalimu Nyerere Memorial 11(1) Waziri wa
Kumbukumbu ya Mwlimu Academy Act, 2005 Elimu
Nyerere

70. Mwenyekiti wa Baraza la The Institute of Accountancy 2 (a)


Chuo, Chuo cha Uhasibu Arusha Act, Cap 240 [R.E
Arusha 2002]

71. Mkurugenzi, Chuo cha The Institute of Rural 8 (1)


Mipango Development Planning Act, Cap
174 [R.E 2002]

72. Mwenyekiti wa Baraza la The Institute of Rural 5(2) na


Chuo, Chuo cha Mipango De.velopment Planning Act, Jedwali-kif 1(a)
Cap 174 [RE 2002]

73. Mwenyekiti wa Baraza la The Institute of Finance Jedwali la


Chuo, IFM Management Act, Cap 91 [R.E Kwanza kif 2(a)
2002]

74. Mwenyekiti wa Bodi, Chuo The College of Wildlife 4(3) na kif Mwenyekiti wa
cha Wanyama Pori Management Act, Cap 209 [R.E 2(1)(a) cha Bodi, Chuo
2002]. Jedwali cha wanyama
Pori

75. Mwenyekiti, Shirika la The Kibaha Education Centre 6(2) (a)


(Establishment) Order, G.N. No.

98
Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa
/kushauriana
Elimu, Kibaha 2 of 1970.

76. Mwenyekiti wa Bodi ya The Cereals and Other Produce 5(1)


Nafaka Act, 2009

77. Mkurugenzi Mkuu wa The Fertilizers Act, 2009 7(1) Waziri wa


Mamlaka ya Mbolea Kilimo

78. Mwenyekiti wa Bodi ya The Cashewnut Industry Act, 4(1) Waziri wa


Korosho 2009 Kilimo

79. Mwenyekiti wa Bodi ya The Crops Laws Miscellaneous 15(1)


Mazao Amendments) Act, 2009.

80. Mwenyekiti, Bodi ya Pamba The Tanzania Cotton Lint and 3(3) na Waziri wa
Seed Board Act, Cap 201 [R.E Jedwali- kif Kilimo
2002]. 1(1) (a).

81. Mkurugenzi, Taasisi ya The Tropical Pesticides 8


Utafiti wa Madawa ya Kuulia Research Institute Act, Cap
Wadudu 161 [R.E 2002]

82. Mwenyekiti wa Bodi, Taasisi The Tropical Pesticides 6(2) na Jedwali


ya Utafiti wa Madawa ya Research Institute Act, Cap –kif 1(a) (i)
Kuulia Wadudu 161 [RE 2002]

83. Mwenyeki wa Bodi, Kituo The Uyole Agricultural Centre 6(2)(a)


(Establishment) Order, G.N. No.
99
Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa
/kushauriana
cha Kilimo Uyole 70 of 1976.

84. Mkurugenzi na Naibu The Uyole Agricultural Centre 5(1)


Mkurugenzi, Kituo cha (Establishment) Order, G.N. No.
Kilimo Uyole 70 of 1976.

85. Mwenyekiti Mtendaji, The Tanzania Commission for 6(1)(a)


TACAIDS Aids Act, 2001

86. Mwenyekiti wa Bodi ya the Medical Stores Department 6(1)


Wadhamini, MSD Act, Cap 70 [RE 2002]

87. Mkurugenzi Mkuu, MSD The Medical Stores Department 9(1)


Act, Cap 70 [RE 2002]

88. Mwenyekiti wa Bodi ya The Ocean Road Cancer 6(1)(a)


Wadhamini, Taasisi ya Institute Act, Cap 86 [R.E
Saratani- Ocean Road 2002].

89. Mkurugenzi Mtendaji The Ocean Road Cancer 8(1)


Institute Act, Cap 86 [R.E
2002].

90. Mwenyekiti wa Bodi ya The Muhimbili National 6(2) na kif 1(a)


Udhamini ya Hospitali ya Hospital Act, 150 [R.E 2002]. cha Jedwali
Taifa ya Muhimbili

100
Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa
/kushauriana
91. Mkuu wa Majeshi(JWTZ) Katiba; The National Defence Ibara ya 148(2)
Act, Cap 192 [RE 2002] (a) ya Katiba;

Kifungu 15(1)
cha Sura ya
192

92. Makamanda wa vikosi The National Defence Act, Cap 16(1) Mkuu wa
mbalimbali vya JWTZ 192 [R.E 2002] Majeshi

93. Inspekta Jenerali wa Polisi Katiba 148(2) (a)

94. Makamishna mbalimbali wa Katiba 148(2) (a)


Jeshi la Polisi

95. Kamishna Jenerali wa Katiba 148(2) (a)


Magereza

96. Makamishana wa Magereza Katiba 148(2) (a)

97. Mkuu wa Jeshi la Kujenga The National Service Act, Cap 21


Taifa 193 [RE 2002]

98. Mkurugenzi Mkuu wa Idara The Tanzania Intelligence and 6(1)


ya Usalama wa Taifa Security Service Act, Cap 406
[R.E 2002].

101
Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa
/kushauriana
99. Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa The Parole Boards Act, Cap 400 3(2)(a)
ya Parole [R.E 2002]

100. Rais wa Mahakama Maalum The Special Tribunals Act Cap 4(1)
ya Kijeshi na wajumbe 126 [R.E 2002]
wengine wasiopungua wawili

101. Mwenyekiti wa Bodi ya The National Housing 5(2) na Kif 1(a)


Shirika la Nyumba la Taifa Corporation Act, Cap 295 [R.E cha Nyogeza ya
2002]. Kwanza.

102. Mkurugenzi Mkuu, Tume ya The Atomic Energy Act, 2003 7(1)
Nishati Mionzi

103. Kamishna wa Madini The Mining Act, 2010 19(1)

104. Kamishna wa Mafuta The Petroleum (Exploration and 8 (1)


(Commissioner for Petroleum Production) Act, Cap 328 [RE
Affairs) 2002].

105. Mwenyekiti, TPDC The Tanzania Petroleum 7(2)(a)


Development Corporation
(Establishment) Order, G.N. No.
90 of 1969

106. Meneja Mkuu,TPDC The Tanzania Petroleum 7(3)


Development Corporation

102
Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa
/kushauriana
(Establishment) Order, G.Ns.
Nos.140 of 1969 and

43 of 1985

107. Mwenyekiti wa Bodi, State Mining Corporation 6(2)(a)


STAMICO (Establishment) Order, G.N. No.
163 of 1972

108. Meneja Mkuu, STAMICO State Mining Corporation 6(3)


(Establishment) Order,
(Sections 3, 5 and 10), [R.E
2002]

109. Mwenyeki wa Bodi ya The Dar es Salaam Water and 21(1) (a)
DAWASA Sewerage Authority
(Amendment) Act, 2001

110. Mwenyeki wa Bodi ya The Surface and Marine 7(2)


SUMATRA Transport Regulatory Authority
Act, 2001

111. Mwenyekiti wa Bodi ya The Energy and Water Utilities 8(2)


EWURA Regulatory Authority Act, 2001

112. Mwenyekiti wa Bodi ya The Tanzania Trade 6(2) na kif 1 (a)


Mamlaka ya Biashara Development Authority Act, cha Nyongeza

103
Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa
/kushauriana
Tanzania 2009 ya Kwanza

113. Mkurugenzi Mkuu wa The Tanzania Trade 8(1)


Mamlaka ya Biashara Development Authority Act,
Tanzania 2009

114. Mwenyekiti wa Baraza la The Fair Competition Act, 2003 83(2)(a) Jaji Mkuu
Ushindani wa Kibiashara
(Fair Competition Tribunal)

115. Wajumbe sita wa Baraza la The Fair Competition Act, 2003 83(2)(b) Mwanasheria
Ushindani wa Kibiashara Mkuu

116. Mwenyekiti wa Bodi ya The Tax Revenue Appeals Act, 8(2) (a) Jaji Mkuu
Rufaa za Kodi (The Tax Cap 408 [R.E 2002]
Revenue Appeals Board)

117. Makamu wawili wa The Tax Revenue Appeals Act, 8(2)(b)


Mwenyekiti wa Bodi ya Cap 408 [R.E 2002]
Rufaa za Kodi (The Tax
Revenue Appeals Board)

118. Mwenyekiti wa Tume ya The Fair Competition Act, 2003 62(6)(a)


Ushindani wa kibiashara

119. Mwenyekiti wa Bodi, Kituo The Tanzania Investment Act, 7(2)(a)


cha Uwekezaji(TIC) Cap 38 [R.E 2002]

104
Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa
/kushauriana
120. Mkurugenzi Mtendaji, Kituo The Tanzania Investment Act, 10
cha Uwekezaji Cap 38 [R.E 2002]

121. Mkurugenzi Mkuu, Tume ya The Tanzania Commission for 6(1)


Sayansi and Teknolojia Science and Technology Act,
Cap 226 [R.E 2002].

122. Mkurugenzi Mkuu, Idara ya The Meteorology Act, Cap 157 5(2)
Hali ya Hewa [R.E 2002]

123. Mwenyekiti wa Bodi ya The Wildlife Conservation Act. 92(3)(a)


Wadhamini wa Mfuko wa 2009.
Ulinzi wa Wanyama Pori

124. Mwenyeti wa Bodi ya The National Parks Act, Cap 8 na kif 1(2)cha
Wadhamini ya Mbuga za 282 [R.E 2002]. Jedwali
Wanyama za Taifa

125. Wajumbe wa Bodi ya The National Parks Act, Cap 8 na kif 1(1) (b)
Wadhamini ya Mbuga za 282 [RE 2002] cha Jedwali
Wanyama za Taifa

126. Mkurugenzi Mkuu, Taasisi The Tanzania Wildlife Research 14(1)


ya Utafiti wa Wanyama Pori Institute Act, Cap 260 [RE
2002].

127. Mhifadhi Mkuu, Mamlaka ya The Ngorongoro Conservation 7(1)

105
Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa
/kushauriana
Hifadhi ya Ngorongoro Area Act, Cap 284 [R.E 2002]

128. Mkurugenzi wa The Wildlife Conservation Act, 3(1)


Uwindaji(Director of Game) Cap 283 [RE 2002]

129. Mwenyekiti wa Bodi, Shirika The Tanzania Wildlife 6(2)(a)


la Taifa la Wanyama Pori Corporation (Establishment)
Order, G.Ns. Nos.231 of 1974
and 389 of 1990

130. Meneja Mkuu, Shirika la The Tanzania Wildlife 6(3)


Taifa la Wanyama Pori Corporation (Establishment)
Order, G.Ns. Nos.231 of 1974
and 389 of 1990

131. Mwenyekiti na wajumbe The Public Service Act, 2002 9(1)


wote wa Tume ya Utumishi
wa Umma

132. Katibu wa Tume ya The Public Service Act, 2002 14(1)


Utumishi wa Umma

133. Kamishana wa Kazi na The Labour Institutions Act, 43(1)


Naibu wake 2004

134. Mwenyekiti wa Baraza la The Labour Institutions Act, 16(3)(a) Waziri wa Kazi
Usuluhishi na 2004

106
Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa
/kushauriana
Upatanishi(Commission for
Mediation and Arbitration)

135. Makamishna wawili wa The Labour Institutions Act, 16(3)(b) Waziri wa Kazi
Baraza la Usuluhishi na 2004
Upatanishi wanaowakilisha
maslahi ya waajiri

136. Makamishna wawili wa The Labour Institutions Act, 16(3)(c) Waziri wa Kazi
Baraza la Usuluhishi na 2004
Upatanishi wanaowakilisha
maslahi ya wafanyakazi

137. Makamishna wawili wa The Labour Institutions Act, 16(3)(d) Waziri wa Kazi
Baraza la Usuluhishi na 2004
Upatanishi wanaowakilisha
Serikali

138. Kamishna wa Maadili, Tume The Public Code of Ethics Act, 19(3)
ya Maadili ya Viongozi Cap 398 [RE 2002]

139. Mwenyekiti wa Bodi na The Social Security (Regulatory 7(1) & 12(1)
Mkurugenzi Mkuu wa Authority Act, 2008
Mamlaka ya Usimamizi wa
Mifuko ya Jamii (SSRA)

107
Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa
/kushauriana
140. Mkurugenzi Mkuu wa LAPF The Local Authorities Pension 8(1)
Fund Act, 2006

141. Mkurugenzi Mkuu, Mfuko The Workers’ Compensation 6(1)


wa Fidia Kwa Wafanyakazi Act, 2008

142. Mwenyekiti wa Bodi, Mfuko The Workers’ Compensation 12(3) na


wa Fidia Kwa Wafanyakazi Act, 2008 Jedwali la
Kwanza- kif
1(1) (a)

143. Mkurugenzi Mkuu, NSSF The National Social Security 4(2)


Act, Cap 50 [R.E 2002]

144. Mwenyekiti wa Bodi, NSSF The National Social Security 53 (3) na


Act, Cap 50 [R.E 2002] Jedwali la Pili-
kif 2 (1) (a)

145. Mkurugenzi Mkuu, PSPF The Public Service Pensions 34(1)


Fund Act, Cap 371 [R.E 2002]

146. Wakuu wa Mikoa Katiba 61(1) Waziri Mkuu (


bara), Rais
wa Zanzibar
(visiwani)

108
Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa
/kushauriana
147. Wakurugenzi watendaji wa The Public Service Act, 2002 5(1)(a)
Serikali za mitaa

148. Wakuu wa Mikoa na Wakuu The Public Service Act, 2002 5(1)(d)
wa Wilaya

149. Makatibu Tawala wa Mikoa The Public Service Act, 2002 5(1)(a)
yote

150. Watumishi wowote wa The Public Service Act, 2002 5(3)


Umma watajulikana kwa
vyeo vitakavyoamuliwa
kadiri ya mahitaji

151.

152. Mwenyekiti wa Baraza la The Environmental 19(2)(a)


Taifa la Mazingira (NEMC) Management Act, 2004

153. Mkurugenzi Mkuu wa The Environmental 21(2)


Baraza la Taifa la Mazingira Management Act, 2004
(NEMC)

154. Mwenyekiti wa Baraza la The Environmental 204(1) (a)


Rufaa la Mazingira (The Management Act, 2004
Environmental Appeals
Tribunal)

109
Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa
/kushauriana
155. Kamishna wa Ardhi The Land Act, Cap 113 [R.E 9(1)
2002]

156. Mkurugenzi Mkuu wa Tume The National Land Use 7(1)


ya Mipango ya Matumizi ya Planning Commission Act,Cap
Ardhi 116 [R.E 2002].

157.

158. Menyekiti wa Bodi, Shirika The Air-Tanzania Corporation 13(2)


la Ndege Tanzania (Re-organisation and Vesting of
Assets and Liabilities) Act,
2002

159. Mwenyekiti na Makamu wa The Tanzania Civil Aviation 7(2)


Bodi ya TCAA Authority Act, 2003

160. Mwenyekiti na Makamu wa The Tanzania Communications 7(2)


Bodi ya TCRA Regulatory

Authority Act, 2003

161. Mwenyekiti wa Bodi, The Kariakoo Market 5(1)(a)


Shirika la Soko la Kariakoo Corporation Act, Cap 132 [R.E
2002]

162. Meneja Mkuu, Shirika la The Kariakoo Market 5(4)


Corporation Act, Cap 132 [R.E
110
Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa
/kushauriana
Soko la Kariakoo 2002]

163. Mwenyekiti, Shirika la The Mzinga Corporation 6(2)(a)


Mzinga (Establishment) Order [RE
2002]

164. Meneja Mkuu, Shirika la The Mzinga Corporation 6(3)


Mzinga (Establishment) Order [R.E
2002]

165. Mwenyekiti wa Bodi, AICC The Arusha International 7(2)(a)


Conference Centre
(Establishment) Order, [RE
2002].

166. Mkurugenzi Mwendeshaji, The Arusha International 10(1)


AICC Conference Centre
(Establishment) Order, [R.E
2002].

167. Mwenyekti wa Bodi, NDC The National Development 5(2)(a)


Corporation (Establishment)
Order, G.N. No. 90 of 1969

168. Meneja Mkuu, NDC The National Development 5(3)


Corporation (Establishment)

111
Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa
/kushauriana
Order, G.N. No. 90 of 1969

169. Mkurugenzi Mkuu, CDA The Capital Development 5(1)


Authority (Establishment)
Order, G.Ns. Nos.230 of 1973,
230 of 1984 and 32 of 2001.

170. Mwenyekiti wa Bodi, Shirika State Motor Corporation 6(2) (a)


la Taifa la Magari (Establishment) Order, G.Ns.
Nos.72 of 1974 and 82 of 1975.

171. Meneja Mkuu, Shirika la State Motor Corporation 6(3)


Taifa la Magari (Establishment) Order, G.Ns.
Nos.72 of 1974 and 82 of 1975.

172. Mwenyekiti wa Bodi, The National Institute for 5(2) (a)


Shirika la Tija la Taifa Productivity (Establishment)
Order, G.N. No. 124 of 1974.

173. Mwenyekiti, Shirika la The Mzinga Corporation 6(2)(a)


Mzinga (Establishment) Order [RE
2002]

174. Wajumbe wa Tume ya Katiba 74(1)


Uchaguzi

175. Msajili wa Vyama vya Siasa The Political Parties Act, Cap 4(1)

112
Mf Kiongozi/Ofisa Sheria Ibara/kifungu Kuthibitishwa
/kushauriana
258 [R.E 2002]

176. Naibu Msajili wa Vyama vya The Political Parties Act, Cap 4(1)
Siasa 258 [R.E 2002]

177. Mkurugenzi, Uratibu wa The Non-Governmental 3(1)


Asasi Zisizo za Kiserikali Organisations Act, 2002

178. Mwenyekiti Bodi ya Uratibu The Non-Governmental 7(2) na Jedwali


wa Asasi Zisizo za Kiserikali Organisations Act, 2002 Kif 1(1) (a)

179. Wakuu wa idara na The Public Service Act, 2002 5(1)(a)


taasisi za Serikali
zisizochini ya wizara

113
SEHEMU YA NANE

8.1 MUHTASARI WA MAPENDEKEZO


8.1.1 Utangulizi

Sehemu hii inajumuisha mapendekezo yaliyotolewa katika sehemu


ya kwanza hadi ya saba. Mapendekezo yaliyoorodheshwa hapa ni
muhtasari wa mapendekezo yaliyotolewa katika matini kuu (main
text). Lengo la kuweka muhtasari huu ni kuwa na sehemu ya
kurejea kwa haraka lakini misingi na sababu za mapendekezo
zinapatikana kwenye matini.

8.1.2 Madaraka ya Rais na sababu zake

Pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa ni


Mkuu wa Nchi, Kiongozi wa Serikali na Amiri-Jeshi-Mkuu,
utamaduni wa chama tawala umekuwa pia ukimpa Rais kofia ya
kuwa ni Kiongozi Mkuu wa Chama chake. Kama tulivyoona
miongoni mwa majukumu ya Mkuu wa nchi ni pamoja na kuwa
nembo ya umoja na mshikamano wa wananchi wote (A symbol of
national unity and solidarity). Hivyo, ingawa utamaduni wa Rais
kuwa pia kiongozi wa chama unaweza kuwa ulifaa katika mfumo
wa chama kimoja, ndani ya mfumo wa vyama vingi, utaratibu
unaweza ukaathiri nafasi ya Rais kama alama ya umoja na
mshikamano wa wananchi wote. Mfano, Rais anapotembelea eneo
fulani la nchi huku akiwa amevaa nembo za chama chake, ni rahisi
kwa wananchi wasio wanachama wa chama chake kujisikia kuwa
siyo kiongozi wao. Kama Mkuu wa nchi Rais anapaswa kuwa alama
ya umoja na mshikamano wa kitaifa, na kiongozi wa wananchi wote
katika muda wote.

Pili, kwa kuwa Rais ni Mkuu wa nchi na Kiongozi wa Serikali, Rais


ana majukumu mengi, hivyo inafaa asiwe kiongozi wa chama ili
aweze kuelekeza nguvu na muda wake katika kuendesha serikali
na kuiongoza nchi. Siasa za chama zifanywe na watu wengine wa
chama chake. Mathalan, mfumo huu unatumika katika nchi ya
Marekani ambako taasisi ya Urais imekomaa. Hivyo,

114
inapendekezwa kuwa ingawa Rais atapendekezwa na chama chake,
Katiba imzuie kushika nafasi za uongozi wa chama.

8.1.3 Mamlaka Ya Kutoa Misamaha (Prerogative Of Mercy)

Mamlaka ya kutoa msamaha ni muhimu na kiongozi wa nchi


anastahili kuendelea kuwa na mamlaka ya aina hii. Inaelekea
malalamiko mengi yanasababishwa na matumizi yasiyo mazuri ya
madaraka ya aina hii kwa kuwasamehe watu ambao jamii huona
hawastahili kusamehewa. Hivyo basi, Katiba mpya iweke udhibiti
wa madaraka ya msamaha ili yasiweze kutumika vibaya. Ili
kufanikisha hili, tunatoa mapendekezo haya:
 Katiba mpya ianzishe Kamati ya Kumshauri Rais kuhusiana na
misamaha;
 Kamati ya Ushauri ijumuishe wajumbe huru ambao siyo
watumishi wa Serikali;
 Katiba mpya ieleze bayana mipaka ya Rais katika kutoa
misamaha. Isitoe tu mamlaka yasiyo na mipaka.
 Katiba iruhusu mwananchi yeyote kupinga msamaha
Mahakamani kupitia utaratibu wa mapitio (judicial review).
 Katiba iseme ni “lazima” Bunge litunge sheria ambayo
itaelekeza namna mamlaka ya kutoa msamaha
yatakavyotekelezwa.
 Ili Bunge liweze kutunga sheria inayosimamia misamaha,
Katiba isitoe mamlaka ya ujumla (absolute power) kwa Rais
kama ilivyo sasa ambapo Rais amepewa mamlaka ya
kumsamehe “mtu yeyote” anayetumikia “adhabu yeyote”
kuhusiana na “kosa lolote.”

8.1.4 Mamlaka ya kutangaza hali ya hatari

Rais ana madaraka makubwa ya kutangaza hali ya hatari. Hata


hivyo, madaraka hayo ni muhimu ili kumuwezesha kukabiliana na
hatari kubwa inayolikabili Taifa. Katika hali ya vita, Rais kama
Amiri-Jeshi-Mkuu anahitaji madaraka ya kutosha kuweza
kuchukua hatua zozote anazoona zinafaa kumshinda adui ili
kulinda usalama wa Raia na mali zao. Kwa vyoyote vile, kwa mfumo
uliopo, madaraka ya ulinzi wa Taifa hayawezi kuwekwa kwa mtu
mwingine isipokuwa Rais.

Hata hivyo, madaraka ya Rais katika kutangaza hali ya hatari na


kutangaza vita hayo ni lazima yadhibitiwe Kikatiba ili yasitumiwe
115
vibaya. Uzoefu wa zaidi ya miaka 200 ya Marekani unaonyesha
kuwa kuweka madaraka mengi kwa chombo kimoja inaweza kuleta
hatari kwa nchi. Hivyo, ni muhimu kuweka mfumo wa kudhibiti
utumiaji wa madaraka hayo ili kukabiliana na uwezekano wa
kutumia madaraka hayo vibaya. Kwa sababu hiyo inapendekezwa
hapa kuwa;

 Madaraka ya Rais kutangaza hali ya hatari yathibitiwe na


Bunge yasije yakatumiwa vibaya. Rais aombe kibali cha
kutangaza hali ya hatari Bungeni kadiri inavyowezekana.
Bunge liwe na mamlaka ya kuithinisha au kuzuia Rais
kutangaza hali ya hatari au kuliondoa tangazo la hali ya
hatari wakati wowote litakapoona kuna haja ya kufanya
hivyo;

 Jukumu la Mahakama la kulinda haki za watu na kudhibiti


matumizi mabaya ya madaraka ni muhimu yakatumika pia
kudhibiti matumizi mabaya ya madaraka ya kutangaza hali
ya hatari;

 Rais alazimike kushauriana na Bunge kabla ya kutangaza


vita. Kama alivyowahi kuonya Mwanafalsafa na Rais wa
zamani wa Marekani, James Madison kuwa kumpa Rais
madaraka ya kutangaza vita inaweza kuwa ni “ushawishi
mkubwa sana kwa mtu mmoja.”1 Rais asiruhusiwe
kutangaza vita bila ruhusa ya Bunge isipokuwa katika hali
ambayo nchi inaelekea kuvamiwa au tayari imeshavamiwa na
adui. Katika kushauriana na Bunge, Rais alazimike kutoa
taarifa muhimu ikiwemo kuhusu maslahi ya nchi yaliyo
katika hatari na sababu za kutumia njia ya vita kama njia
pekee ya kulinda maslahi hayo;

 Wakati wa vita Rais alazimike kutoa taarifa za mara kwa


mara kuhusu maendeleo ya vita.

8.1.5 Nafasi ya Rais wakati wa Uchaguzi

Inapendekezwa kuwa Katiba itamke kuwa Rais aendelee kuwa


madarakani kama ilivyo katika Katiba ya sasa. Lakini Katiba

1Nukuu kutoka barua ya Walter Jones, Mbunge wa Bunge la Marekani kwenda


kwa Rais wa nchi hiyo, Barack Obama ya tarehe 29 Agosti, 2012
116
inatakiwa kufanya yafuatayo ili kushughulikia matatizo
yaliyosababisha watu kusema asiwe madarakani wakati wa
uchaguzi.
 Sheria ya Uchaguzi, Kanuni za Uchaguzi (The Election Code of
Conduct) na Sheria ya Gharama za Uchaguzi zinazuia
matumizi ya rasilimali za Serikali katika uchaguzi. Rais ndiye
kiongozi nambari moja anayetakiwa kusimamia utekelezaji
wa sheria za nchi. Anapochaguliwa kuwa kiongozi wa nchi
ina maana anaaminiwa na wananchi kuifanya kazi hiyo kwa
uaminifu, na anaapa kuilinda Katiba na kufuata sheria.
Anatakiwa kuwahimiza viongozi wa juu, Mawaziri na
watumishi wegine wa Serikali kufuata sheria. Hivyo, akikiuka
kiapo chake Mahakama iwe na uwezo wa kuufuta uchaguzi.
Uchaguzi ukifutwa, Tume ya Uchaguzi iitishe uchaguzi
mwingine ambao hautamjumuisha Rais. Bila shaka, kurudia
uchaguzi ni gharama kubwa kwa nchi ambayo watu wake ni
maskini kama Tanzania. Hata hivyo, kupotea kwa haki ni
gharama kubwa zaidi kwa sababu watu wanaweza
kuchinjana na nchi kuingia kwenye machafuko makubwa;

 Endapo Mahakama itaona kwamba ukiukwaji uliofanywa


haukuwa mkubwa kiasi cha kuathiri matokeo ya uchaguzi
lakini kuna ushahidi kuwa Rais alielekeza au akifahamu
ukiukwaji husika basi Mahakama iliriarifu Bunge
kumfungulia mashtaka (impeachment) ili aondolewe
madarakani. Na kama ikitokea hivyo Makamu wa Rais ashike
madaraka. Hii itaepusha gharama kubwa ya kurudia
uchaguzi;

 Kuwe na Tume huru ya Uchaguzi ambayo itashughulikia


matatizo yanayotokea wakati wa uchaguzi bila kuegemea
upande wowote;

 Vyombo vya uwajibikaji kama TAKUKURU na Polisi


vinatakiwa kuwa huru ili kusimamia uchaguzi kwa mujibu
wa sheria.

117
8.1.6 Udhibiti wa Madaraka ya Rais na Uwajibikaji

Ili kuongeza uwajibikaji na kuongeza uthibiti wa madaraka ya Rais


mapendekezo inapendekezwa;

 Idadi ya wateule wa Rais ipunguzwe ili ibakie orodha fupi ya


viongozi na maofisa wa umma wakiwemo Mawaziri, Mabalozi,
wasaidizi wake, na watendaji wengine watakao wajibika
kwake moja kwa moja. Watendaji na viongozi wengine
wapatikane kwa utaratibu wa kuajiriwa, kupandishwa vyeo
au kuteuliwa na mamlaka na vyombo vingine kadiri
itakavyofaa;

 Kuwe na utaratibu wa Bunge kuidhinisha wateule wa Rais


kwa nafasi mbalimbali;

 kuwe na utaratibu wa Rais kufanya uteuzi wa maofisa


waandamizi wa umma kulingana na mapendekezo ya vyombo
mbalimbali vilivyoanishwa Kikatiba kama vile Tume za
Utumishi unafaa kuigwa. Utaratibu huo zaidi ya kupunguza
mianya ya kufanyika uteuzi usiozingatia sifa stahili, pia
unaongeza uwezekano mkubwa wa kupata watendaji walio
bora;

 Mawaziri wasitokane na Wabunge ili kuongeza urari; ili


Bunge liweze kufanya kazi ya kufanya kazi ya kumsimamia
Rais ipasavyo. Mawaziri wasipokuwa Wabunge kutaondoa
mgongano wa maslahi unaowakumba Mawaziri na Wabunge
kati ya wajibu waki Bunge na wajibu wa kiuWaziri. Mawaziri
pia wataweza kutumia muda wao na nguvu zao kwenye
wizara zao wakiondolewa mzigo wakushughulikia majimbo
yao. Pia, Mawaziri wasipokuwa Wabunge itampa Rais wigo
mpana wa kuteua Mawaziri wenye sifa zinazotakiwa.
Mawaziri watakuwa wanakutana na Wabunge kwenye kamati
zao na mbele ya Bunge kueleza sera zao na kujibu maswali
ya Wabunge;

 Rais asiwe na uwezo wa kuvunja Bunge pale Bunge


linaposhindwa kupitisha muswada ambao Rais

118
anaupendelea. Badala yake, swala husika lipelekwe
Mahakamani au kwenye kura za maoni (referendum) kadiri
itakavyofaa;

 Kusiwe na Wabunge wa kuteuliwa na Rais maana uwepo wao


unaongeza ushawishi wa Rais katika utendaji wa Bunge na
hivyo kushindwa kuathiri uwezo wa Bunge kumwajibisha
Rais. Hoja hii itakuwa na nguvu zaidi kama Mawaziri
watakuwa hawatokani na Wabunge maana moja ya malengo
ya kuwa na nafasi hii ni kumwezesha Rais kuwapata
wananchi wenye uwezo na sifa za kuwa Mawaziri lakini
hakuingia Bungeni kwa njia ya kuchaguliwa;
 Utamaduni wa nidhamu ya chama usiruhusiwe kuzuia
uhuru wa Wabunge kufanya kazi za kiBunge kama
ilivyowekwa Kikatiba. Utaratibu unaojulikana kama crossing
the floor, yaani kupiga kura kulingana na upande anaona
unafaa bila kupoteza nafasi yake ya Ubunge;

 Mahakama ziwe na uwezo wa kusikiliza malalamiko dhidi ya


uchaguzi wa Rais. Hata hivyo, ni muhimu kuwe na ukomo wa
kusiliza shauri la namna hiyo;

 Wabunge wasizuiliwe kuanzisha muswada inyohusiana na


masuala ya fedha na kodi au jambo lolote isipokuwa yale
yanayogusa maslahi yao binafsi.

8.1.7 Kinga ya Rais kushtakiwa

Ni muhimu wa Rais kama kiongozi wa nchi kupewa kinga ya


kushtakiwa kwa sababu majukumu yake ni mengi. Hivyo, kuna
mapendekezo kuhusiana na kinga ya Rais ya kutoshtakiwa:

 Inapendekezwa kuwa kinga ya Rais kutoshtakiwa ijengwe


katika misingi mikuu mitatu. Msingi wa kwanza ni “utendaji”
(functional necessity or theory). Msingi wa pili uwe ni
“uwajibikaji”(accountability). Msingi wa tatu wa kinga uwe ni
“utawala wa sheria” (Rule of Law);

 Dhana ya “kinga kamilifu” (absolute immunity) inafaa


kuepukwa na badala yake Rais apewe “kinga yenye ukomo”
(restrictive or limited immunity). Maana yake ni kuwa Rais

119
akitenda uhalifu au kuuhujumu uchumi akiwa madarakani
asiruhusiwe kujificha nyuma ya kivuli cha kinga,
awajibishwe. Hata hivyo, wakati wa kuandika Katiba inafaa
kuzingatia kuwa Rais ana kazi nyingi, anaongea na watu
wengi, na anapata changamoto nyingi. Inawezekana akafanya
kitendo fulani bila kujua kuwa kitendo hicho ni kinyume cha
sheria. Hivyo, ni vizuri Katiba ieleze bayana kuwa Rais
atawajibishwa kwa kufanya vitendo vile ambavyo “kiuwazi ni
kinyume cha sheria” (manifestly unlawful) tu. Mathalan,
haitokuwa utetezi kusema Rais hakujua kama kuua au
kutesa watu, au kuchukua fedha za umma kunazuiwa na
sheria;

 Inapendekezwa Rais awe na kinga kama ifuatavyo:

8.1.8 Kinga Inayopendekezwa


Inapendekezwa Rais awe na kinga kama ifuatavyo;
 Rais hatoshtakiwa kwa kosa la jinai kwa jambo alilolifanya
akiwa madarakani isipokuwa akitenda kosa la “kiuwazi” la
kihaini, kijinai, au uhujumu uchumi;

 Rais hatoweza kushtakiwa kwa kosa la “kiuwazi” la uhaini,


jinai au uhujumu uchumi hadi kwanza aondolewe
madarakani na Bunge au baada ya kumaliza muhula wake
wa uongozi;

 Rais atakuwa na kinga ya kutofunguliwa shauri la madai


kuhusiana na jambo alilolifanya kuhusiana na kazi yake na
kinga hii atakuwa nayo akiwa madarakani na itaendelea
katika maisha yake yote akiwa nje ya madaraka;

 Rais anaweza kufunguliwa shauri la madai kwa vitendo vyake


binafsi ambavyo havihusiani na majukumu yake ya umma
ama akiwa madarakani au baada ya kumaliza muhula wake
wa uongozi.

8.1.9 Mamlaka ya Uteuzi

Inapendekezwa kuwe na mabadiliko katika madaraka ya uteuzi ya


Rais kama ifuatavyo;
120
 Kutenganisha shughuli za Mkuu wa Nchi na kiongozi wa
Serikali ili Rais abaki zaidi na majukumu ya Mkuu wa Nchi
na Amiri-Jeshi-Mkuu na shughuli za Serikali ziwe kwa
kiwango kikubwa chini ya Waziri Mkuu. Ikiwa hivyo; Rais
atabaki na madaraka ya kumteua Waziri Mkuu , Mawaziri,
wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, Mabalozi,
watendaji na viongozi wengine ambao uteuzi wao unahitaji
mamlaka ya kipekee ya Mkuu wa Nchi na Amiri-Jeshi-Mkuu;

 Uteuzi mwingine wowote ufanywe na Serikali katika


mamlaka zake mbalimbali kama vile Tume za Utumishi kwa
kuzingatia sifa, uwezo na vigezo.

121
BIBLIOGRAFIA

Vitabu

Carroll, Alex, (2009), Constitutional and Administrative Law,


Pearson Education Limited, Harlow.

Clinton, R., (1948), Constitutional Dictatorship: Crisis Government in


the Modern Democracies, London, Oxford University Press.

Coulson, Andrew, (1982), Tanzania: A Political Economy, Oxford


University Press, New York.

Garner, Bryan A. (ed.), (2009), Black's Law Dictionary, 9th edn,


Thomson Reuters, St Paul, Minnesota.

Hatchard, J., Ndulo, M., Slinn, P., (2010). Comparative


Constitutionalism and Good Governance in the Commonwealth.
Cambridge: Cambridge University Press.

Hauss, C., (1999), Comparative Politics: Domestic Responses to


Global Challenges, 3rd Edition, and Wadsworth.

Locke, John, (1689), Two Treatises of Civil Government, Prentice Hall,


New Jersey.

Nwabueze, B.O., (1974), Presidentialism in Commonwealth Africa,


Hurst, London.

Oraa, J., (1992), Human Rights in States of Emergency in


International Law, Oxford, Clarendon Press.

Palmer, M., (1997), Comparative Politics, F.E. Peacock Publishers,


Florida.

Palmer, M., (1997), Comparative Politics: Political Economy, Political


Culture, and Political Interdependence, F.E. Peacock Publishers, Inc.

Patterson, Thomas E., (2004), We the People: A Concise Introduction


to American Politics, 5th edition, McGraw Hill, New York.

122
Makala

Barry, Herbert , “The King Can Do No Wrong”, in Virginia Law


Review, Vol. 11, No. 5 (Mar., 1925), pp. 349-371.

Bass, Peter Evans, “Ex-Head of State Immunity: A Proposed


Statutory Tool of Foreign Policy”, The Yale Law Journal, Vol.97, No
2 (Dec., 1987), pp.299-319.

Burgin, E., (1992), “Congress, the War Powers Resolution, &the


Invasion of Panama. Polity”, Vol. 25, No. 2 (Winter, 1992), pp. 217-
242.

Chemerinsky, Erwin, “Against Sovereign Immunity”, in Stanford


Law Review, Vol. 53, No. 5, Symposium: Shifting the Balance of
Power? The Supreme Court, Federalism, and State Sovereign
Immunity (May, 2001), pp. 1201-1224.

Chikawe, M. M., (2009), Statement by Hon. Mathias Meinrad


Chikawe (MP), Minister for Constitutional Affairs and Justice of the
United Republic of Tanzania during the consideration of Tanzania`s
Fourth Periodic Report on the International Covenant on Civil and
Political Rights (ICCPR) to the United Nations Human Rights
Committee Geneva, Switzerland, 13 - 14 July 2009.

Clark, R. (1990). Presidentail Emergency Powers : The Contribution


of Lindsay Rogers. Presidential Studies Quarterly, Vol.20.No.1 pp
13-30.

Currie, D. (2000).Rumors of Wars: Presidential and Congressional


War Powers, 1809-1829: The University of Chicago Law Review,
Vol. 67, No. 1 (Winter, 2000), pp. 1-40.

Damas, Phillipo, (2012), The Challenges of Enforcing the Election


Expenses Act, 2010: A Case Study of Bukoba District, LL.B.
Dissertation submitted to the University of Dar es Salaam.

Dinan, John, “The Pardon Power and the American State


Constitutional Tradition”, in Polity, Vol. 35, No. 3 (Apr., 2003), pp.
389-418.

Dinstein, "Diplomatic Immunity from Jurisdiction Rationae


Materiae"(1966) 15 I.C.L.Q. 76.

123
Ferguson, Margaret Robertson (2003). Chief Executive Success in
the Legislative Arena, State Politics & Policy Quarterly, Vol. 3, No. 2
(Summer, 2003), pp. 158-182.

Fombad, C.M., (2004), “Cameroon’s Emergency Powers: A Recipe for


(Un) constitutional Dictatorship?” in the Journal of African Law,
School of Oriental and African Studies.

Fox, Hazel , na wegine, “The Future of Former Head of State


Immunity after ex parte Pinochet”, in The International and
Comparative Law Quarterly, Vol. 48, No. 4 (Oct., 1999), pp. 937-
949.

Harris, B. V, “Judicial Review, Justiciability and the Prerogative of


Mercy”, in The Cambridge Law Journal, Vol. 62, No. 3 (Nov, 2003),
pp. 631-660.

Harrison, John , “Pardon as Prerogative”, in Federal Sentencing


Reporter, Vol. 13, No. 3-4, Pardon Power and Sentencing
Policy(November/December 2000 - January/February 2001), pp.
147-149, pp. 47 & 149.

Harrison, John, “Pardon as Prerogative”, in Federal Sentencing


Reporter, Vol. 13, No. 3-4, Pardon Power and Sentencing
Policy(November/December 2000 - January/February 2001), pp.
147-149.

Henckaerts, Jean-Marie and Louise Doswald-Beck, (2009),


Customary International Humanitarian Law, Vol 1, Cambridge
University Press, Cambridge.

Klieman, A.S., (1979). Preparing for the Hour of Need: Emergency


Powers in the United States in the Review of Politics, Vol. 41, No. 2
(Apr., 1979), pp. 235-255.

Krent, Harold J., “Conditioning the President's Conditional Pardon


Power”, in California Law Review, Vol. 89, No. 6 (Dec., 2001), pp.
1665-1720, pp.1666-1667.

Krent, Harold J., “Conditioning the President's Conditional Pardon


Power”, in California Law Review, Vol. 89, No. 6 (Dec., 2001), pp.
1665-1720.

124
Mazrui, Ali A., “Anti-Militarism and Political Militancy in Tanzania”,
in The Journal of Conflict Resolution, Vol. 12, No. 3 (Sep., 1968),
pp. 269-284.

Mkandawire, T.(2011). Running While Others Walk: Knowledge and


the Challenge of Africa’s Development in Africa Development, Vol.
XXXVI, No. 2, 2011, pp. 1– 36.

Montesquieu, 1748. L’Esprit des Lois, Book XI. The quotation is


from Finer, Herman, 1965. Theory and Practice of Modern
Government. London: Methuen & Co Ltd, pp 94-95.

Mubako S.V (1972). ‘The Constitution of the Republic of Zambia’,


unpublished paper.

Nyerere, Julius, “One-Party Government”, in Transition, No. 75/76,


The Anniversary Issue: Selections from Transition, 1961-1976
(1997), pp. 156-161.

Peter, C. M., (2000), “Constitution Making in Tanzania: The Role of


the People in the Process”, on

http://www.kituochakatiba.org/index2.php?option=com_docman&t
ask=doc_view&gid=179.

Pollock , F. & F. Maitland, (1909), History of English Law , 2nd edtn,


Liberty Fund, Indianapolis.

Pratt, Cranford, “Julius Nyerere: Reflections on the Legacy of His


Socialism”, in Canadian Journal of African Studies / Revue
Canadienne des Études Africaines, Vol.33, No. 1 (1999), pp. 137-
152.

Prempeh, K. (2008). Presidential Power in Comparative Perspective:


The Puzzling Persistence of Imperial Prseidency in Post-
Authoritarian Africa. 35 Hastings Constitutional Law Quarterly 761,
784-795.

Ritchie, Donald A., “Investigating the Watergate Scandal” in OAH


Magazine of History, Vol. 12, No. 4, Congressional History (summer,
1998), pp.49-53.

Shanor, Charles & Marc Miller “Pardon Us: Systematic Presidential


Pardons”, Federal Sentencing Reporter, Vol. 13, No. 3-4, Pardon

125
Power and Sentencing Policy(November/December 2000 -
January/February 2001), pp. 139-146.

Shanor, Charles & Marc Miller “Pardon Us: Systematic Presidential


Pardons”, Federal Sentencing Reporter, Vol. 13, No. 3-4, Pardon
Power and Sentencing Policy (November/December 2000 -
January/February 2001), pp. 139-146.

Sitta, S., Slaa, W., &Cheyo, J.M, (2008). Bunge Lenye Meno: A
Parliament with Teeth, for Tanzania. London. African Research
Institute.

Sykes, Patricia Lee, (1989). “The President as Legislator: A


"Superepresenator" Presidential Studies Quarterly, Vol. 19, No. 2,
Counsel for the New President (SPRING1989), pp. 301-315.

Tait, David, “Pardons in perspective: The role of forgiveness in


criminal justice”, on
http://www.canberra.edu.au/ncf/events/pardonsperspective.pdf.

Travis, M., “The Prerogative of Mercy in New Zealand”,


onhttp://homepages.ihug.co.nz/~ttpbst/me/writing/mercy.htm.

Usher, Roland G., “James I and Sir Edward Coke”, in The English
Historical Review”, Vol. 18, No. 72 (Oct., 1903), pp. 664-675.

Wambali, M. (2012). Paramount Issues for Consideration in the


Constitutional Review Process in Tanzania. The paper presented to
the Tanganyika Law Society (TLS) Annual Conference on “The
Lawyers’ Contribution to the Process of Constitutional Review” held
on 31st August, 2012 at the Arusha International Conference
Centre, Arusha, Tanzania.

Wambali, Michael K.B., “The Historical Overview of the


Constitutional Reforms towards Limited Leadership in Tanzania”, in
Commonwealth Law Bulletin, Vol. 34 No.2 (June 2008), pp.277-
296.

Watts, Sir Arthur, "The Legal Position in International Law of Heads


of States, Heads of Governments and Foreign Ministers" (1994) 247
Hague Recueil 9.

Cindy, Skach, (2007). The “ newest ” separation of powers:


Semipresidentialism . ICON, Oxford University Press and New York
University School of Law.Volume 5, Number 1, 2007, pp. 93–121.
126
Steven, Roper.(2002). Are All Semipresidential Regimes the Same?
A Comparison of Premier-Presidential Regimes. Comparative
Politics, Vol. 34, No. 3 (Apr., 2002), pp. 253-272

Taarifa Mbali mbali

Chama cha Mapinduzi, Mapendekezo ya Halmashauri Kuu ya Taifa


Juu ya Marekebisho ya Katiba ya Serikali, Waraka wa 1983.

Government of Tanganyika, Proposals of the Tanganyika


Government for a Republic, Government Printer, Dar es Salaam.

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Taarifa ya Kamati ya Kuratibu


Maoni Kuhusu Katiba, Kitabu cha Kwanza, 1999.

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Tume ya Rais ya Mfumo wa


Chama Kimoja au vyama vya siasa Tanzania, Kitabu cha Kwanza.

Jumuiya ya Madola, Taarifa ya Kundi la Waangalizi wa Uchaguzi la


Jumuiya ya Madola katika Uchaguzi wa Tanzania, 2010.

TEMCO, The 2010 Tanzania General Elections.

United Republic of Tanzania, The Report on the Commission on


Corruption, Volume 1 (Chapter 1-5), 1996.

127

S-ar putea să vă placă și